Ijumaa, 10 Shawwal 1445 | 2024/04/19
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

بسم الله الرحمن الرحيم

 Wilayah Sudan: Kampeni Pana ya Kufichua Uhalifu wa Marekebisho Katika Bajeti ya Mwaka 2020

Hizb ut Tahrir / Wilayah Sudan ilianzisha kampeni pana ya kufichua uhalifu wa marekebisho katika bajeti ya mwaka 2020 na hilo ni kupitia amali za umma kadha wa kadha zilizofanywa iliyopita; ambapo mashababu wa Hizb katika mji wa Qadharif walianza kwa hotuba za halaiki na zilianza tangu siku ya Ijumaa sawia na tarehe 14/8/2020 M; ambapo hotuba ilifanya ubavuni mwa Msikiti wa Zamani na ilikuwa kwa anwani: "Utafutaji Nyuma ya Wamagharibi Hufisidi Dunia na Akhera". Katika soko la Swabirina eneo la Umdurman na eneo la Dukhainat jijini Khartoum, hotuba zilikuwa katika maudhui ya marekebisho katika bajeti ya 2020.

Kampeni nyingine ilizinduliwa, ambayo ni kufichua uhalifu wa kusawazishaji mahusiano na umbile la Kiyahudi ambalo lililonyakua ardhi ya Isra, ambapo kampeni hii ilianza kwa ugawanyaji toleo kwa anwani: "Serikali ya mpito, inahusika katika ajenda ya mkoloni makafiri, inataka kutangaza usawazishaji mahusiano na umbile la Kiyahudi", ambapo toleo hili liligawanywa katika sehemu nyingi za wilayah ya Sudan katika miji yake tofauti tofauti ndani ya misikiti, viwanja na masoko.

 Mwakilishi wa Afisi Kuu ya Habari ya Hizb ut Tahrir

Katika Wilayah Sudan

Andika maoni

Hakikisha umejaza (*) habari zinazohitajika palipoashiriwa. Kodi za HTML haziruhusiwi.

rudi juu

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu