Jumamosi, 11 Shawwal 1445 | 2024/04/20
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Wanawake na Watoto wa Kiislamu Wanakumbwa na Njaa Hadi Kufa Nchini Somalia huku Watawala wa Waislamu Wakiunga Mkono Ukandamizaji Ulimwenguni

Mnamo tarehe 5 Oktoba 2022, BBC iliripoti kuwa Somalia inakabiliwa na baa la njaa inayotokana na ukame mbaya zaidi kuwahi kutokea katika kipindi cha miaka 40. Hadithi ya dada mmoja Muislamu inayofichuliwa na waandishi wa habari, ni ile ya Fatima Omar ambaye alimzika mtoto mmoja wa kiume kutokana na njaa na tayari alikuwa ameshamzika bintiye wa miaka 3 ambaye alifariki huku akitembea kwa siku 10 kutafuta msaada. Anawaambia waandishi wa habari kwamba hakuwa na nguvu za kumzika mtoto wake na alilazimika kuuacha mwili wake kando ya barabara huku akijua kuwa Fisi walikuwa wanakaribia kuingia ndani.

Soma zaidi...

Al-Waqiyah TV: Je, Tunapaswa Kujibu Vipi Maandamano ya Iran ya Kupinga Hijab?!

Katika muda wa wiki mbili zilizopita, kumekuwa na maandamano kote nchini Iran na katika sehemu zengine za dunia kujibu kifo cha Mahsa Amini, mwanamke wa Kikurdi mwenye umri wa miaka 22, ambaye inasemekana alikamatwa na polisi wa maadili wa Iran kwa kutofinika nywele zake ipasavyo kwa Hijab na kupigwa hadi kufa akiwa chini ya ulinzi wao.

Soma zaidi...

Afisi Kuu ya Habari / Kitengo cha Wanawake: “Je, Tunapaswa Kujibu Vipi Maandamano ya Iran ya Kupinga Hijab?”

Katika muda wa wiki mbili zilizopita, kumekuwa na maandamano kote nchini Iran na katika sehemu nyingine za dunia kujibu kifo cha Mahsa Amini, mwanamke wa Kikurdi mwenye umri wa miaka 22, ambaye inasemekana alikamatwa na polisi wa maadili wa Iran kwa kutofinika nywele zake ipasavyo na Hijabu na kupigwa hadi kufa akiwa chini ya ulinzi wao.

Soma zaidi...

Uadilifu Hupelekea kwenye Kutii Kanuni bila ya Haja ya kutumiwa Nguvu

Mnamo Ijumaa, 16 Septemba 2022, BBC iliripoti juu ya kifo cha mwanamke mmoja wa Iran mwenye umri wa miaka 22 baada ya kukamatwa na polisi wa maadili kwa madai ya kutofuata sheria kali za kufinika kichwa. Kukamatwa kwake kulisababisha apelekwe hospitalini kwa jeraha la kichwa lililomsababishia kukosa fahamu kwa siku kadhaa.

Soma zaidi...

Marufuku Iyopendekezwa ya Hijab katika Shule za Denmark ni Shambulizi kwa Kitambulisho cha Kiislamu

Mnamo tarehe 24 Agosti, tume inayoitwa "Tume ya mapambano ya wanawake yaliyosahaulika" iliyopewa kazi na serikali ya Denmark, ilichapisha mambo tisa ya kupambana na kile ambacho kimeanzishwa katika siasa za Denmark kama "udhibiti hasi wa kijamii". Pendekezo, lililopata mjadala mkali zaidi katika vyombo vya habari vya Denmark na kwenye mitandao ya kijamii, lilikuwa ni pendekezo la kupiga marufuku hijab za Kiislamu katika shule za msingi.

Soma zaidi...

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu