Jumamosi, 11 Shawwal 1445 | 2024/04/20
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Vichwa vya Habari 6/12/2022

Vita nchini Ukraine vimefichua udanganyifu mkubwa katika udhibiti mpya wa hifadhi za silaha baada ya Vita Baridi, na kuacha baadhi ya nchi zikijitahidi kukabiliana na mahitaji ya ulinzi. Ujerumani imekuwa ikikabiliwa na shinikizo la kudumisha dhamira yake ya ulinzi kwa NATO huku ikiipa Ukraine silaha zinazohitajika ili kukabiliana na Urusi.

Soma zaidi...

Pelekeni Mapambano kwa Adui, Kupitia Kusimamisha Tena Khilafah ambayo Itaikomboa Kashmir Iliyokaliwa kwa Mabavu na Kuunganisha Pakistan na Afghanistan kama Dola Moja

Kwa kujibu maneno ya Luteni Jenerali Upendra Dwivedi wa India na Waziri wa Ulinzi Rajnath Singh, ni wakati sasa wa uongozi wa kijeshi wa Pakistan kuchukua hatua madhubuti. Maneno matupu kamwe hayatoshi, wakati hatua ndizo zinazohitajika, kujibu vitendo vya adui.

Soma zaidi...

Mfumo Katili Nchini India Waongeza Chumvi Mauaji ili Kuidhinisha Mashini yake ya Uovu Inayoyumbayumba?

Huku India ikipitia baadhi ya maonyesho muhimu ya uchaguzi katika majimbo yake tofauti tofauti kama Himachal Pradesh, Gujarat na uchaguzi mkuu wa ndani lakini wenye hisa nyingi kwa Mashirika ya Manispaa ya Delhi, inakuwa chanzo cha masuala machafu, yenye uvundo na ugomvi ambayo ni sarafu za uchaguzi zenye uwezo wa kununua tena kura ili kusaidia kuunga mkono mfumo uliofeli.

Soma zaidi...

Kutii Maagizo ya IMF ya Kuongeza Bei ya Mafuta ni kwa ajili tu ya Kudumisha Uhai wa Utawala wa Fisadi wa Hasina pekee, lakini ni Kujiua kwa Uchumi wetu

Katikati ya mateso ya wananchi kutokana na kupanda kwa bei ya bidhaa muhimu na kuzorotesha uzalishaji viwandani kutokana na tatizo la umeme, serikali ya Hasina danganyifu imeamua kuongeza bei ya umeme kwa asilimia 19.92 hadi Tk6.20 kWh kutoka bei ya awali ya Tk5.17 kWh. kwa kutii agizo la Mfuko wa Fedha wa Kimataifa (IMF).

Soma zaidi...

Unyanyasaji wa Watoto Umefikia Kiwango cha Juu sana nchini Ufilipino, huku nchi za Magharibi zikiwa ndio Wahalifu Wanaoongoza

Ufilipino ndiyo nchi yenye uzalishaji mkubwa zaidi wa nyenzo za unyanyasaji wa watoto. Mashirika ya kutoa misaada yamekadiria kwamba mtoto 1 kati ya 5 hudhulumiwa, na kwa kawaida wazazi na watu wa ukoo hufaidika kutokana na unyanyasaji huo. Kufungwa kwa miji wakati wa Janga la maambukizi kuliwaacha watoto walio hatarini wakiwa wamenaswa na watu wazima walio na tamaa ya kifedha.

Soma zaidi...

Kamanda wa Jeshi Tunayemhitaji

Pamoja na mabadiliko katika amri ya jeshi la sita kwa ukubwa duniani, mjadala ulizushwa ndani, nchini Pakistan, na kiulimwengu, juu ya dori ya taasisi yenye nguvu ya kijeshi na mkuu wake wa jeshi. Mengi yamejadiliwa kuhusu urithi wa wakuu wa jeshi, waliomtangulia Jenerali Syed Asim Munir, Mkuu wa Jeshi wa Kumi na Saba wa jeshi la nyuklia, la tisa kwa nguvu zaidi duniani.

Soma zaidi...

Siasa za Kidemokrasia zina Faida Sana kwa Wanasiasa

Mwaka mmoja baada ya kashfa ya mbunge wa Uingereza Owen Paterson kupelekea ahadi za udhibiti mkali, wanasiasa wamevuna £5m kutokana na kazi ya pembeni, gazeti la ‘The Observer’ limeripoti.

Kwa ujumla, wabunge walipata zaidi ya £5.3m kutokana na kazi za nje kuanzia Oktoba 2021 na Septemba 2022, huku wengi, wakiwemo mawaziri wa zamani, wakichukua majukumu mapya kama washauri na wasio watendaji katika mwaka uliopita kwa makampuni ambayo katika kesi kadhaa yaliendeshwa na wafadhili wakuu wa vyama.

Soma zaidi...
Jiunge kwa hii RSS feed

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu