Alhamisi, 18 Ramadan 1445 | 2024/03/28
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Afisi ya Habari
Wilayah Pakistan

H.  19 Jumada II 1442 Na: 1442 / 45
M.  Jumatatu, 01 Februari 2021

 Taarifa kwa Vyombo vya Habari

Mshikamano Pamoja na Waislamu wa Kashmir Inayokaliwa Unahitaji Uhamasishaji wa Khaleefah Rashid wa Majeshi Yetu Matukufu

(Imetafsiriwa)

Mola wa nafsi zetu, Mwenyezi Mungu (swt) asema,

(وَإِنِ اسْتَنْصَرُوكُمْ فِي الدِّينِ فَعَلَيْكُمُ النَّصْرُ)

“Lakini wakiomba msaada kwenu katika Dini, basi ni juu yenu kuwasaidia.” [Surah Al-Anfal 8:72]. Siku ya Mshikamano na Kashmir ya mwaka huu, 5 Februari, inaangukia katika hali mbaya ya mambo, ambapo ni lazima tutimize wajibu wetu kwa Mwenyezi Mungu (swt). Tangu 5 Agosti 2019, Waislamu wa Kashmir Iliyokaliwa wametelekezwa kwa majambazi wa Hindutva, kwa sababu ya sera ya uzuiaji iliyopitishwa na serikali ya Pakistan. Hapo awali, kwa sababu ya msaada wa vikosi vyetu vya kijeshi, wapiganaji wa Kiislamu huko Kashmir Iliyokaliwa waliizuia Dola ya Kibaniani kutokana na kuiunganisha Kashmir Iliyokaliwa, kwa miongo mingi. Lakini, tangu 5 Agosti 2019, kwa kujisalimisha kwa matakwa ya Amerika, watawala wa Pakistan wamekuwa wakiwawinda wale wanaounga mkono Jihad katika Kashmir Iliyokaliwa. Imran Khan hata alitangaza mnamo 18 Septemba 2019, "Ikiwa mtu kutoka Pakistan atakwenda India na akafikiria atapigana huko Kashmir ... mtu wa kwanza atakayemfanyia ukatili ni Wakashmiri. Atakuwa ametenda kama adui wa Wakashmiri." Imran alifanya hivyo ingawa Mtume wa Mwisho wa Mwenyezi Mungu (saw) alionya Ummah wake dhidi ya kupuuza Jihad, akisema,

«مَا تَرَكَ قَوْمٌ الْجِهَادَ إلاّ ذُلّوا» “Watu hawataiacha Jihad isipokuwa watadhalilika.” [Ahmad].

Kwa sababu ya sera ya serikali ya kuzuia, wanajeshi wetu wamenyimwa fursa ya kupatiliza mapigano ya Indo-China huko Ladakh, wakibaki kutazama tu huku raia wakiendelea kuuawa kwa kudumu uchokozi wa Dola ya Kibaniani, katika Mpaka wa Kazi na Mstari wa Udhibiti. Hata wakati silaha za Amerika zenye nyuso mbili vikosi vya jeshi la Dola ya Kibaniani, kwa kujisalimisha kwa upofu kwa Amerika, serikali ya Pakistan inadai kwamba vikosi vyetu vizuiliwe kuvunja taya la adui huko Kashmir Iliyokaliwa. Mbawa za ujasusi za vikosi vyetu vya jeshi ziliipigisha magoti dola kuu ya wakati huo, Urusi ya Usovieti, kupitia kuunga mkono Jihad nchini Afghanistan. Kwa hivyo wanaweza kuifanya nini Dola ya Kibaniani kwa kuunga mkono kikamilifu Jihad huko Kashmir? Mwewe wetu wa jeshi la anga waliivuruga mashine ya vita ya Mabaniani, kwa shambulizi lao dogo lililodhibitiwa mnamo Februari 2019. Kwa hivyo wanaweza kufanya nini endapo watafunguliwa kikamilifu kujibu mwito wa Mwenyezi Mungu (swt) na Mtume wake (saw)? Wakiunganishwa na udugu wa Kiislamu, simba wetu wa jeshi hupenda kufa mashahidi zaidi kuliko Mabaniani waliogawanyika vibaya wanavyopenda maisha. Kwa hivyo wanaweza kufanya nini wanapoongozwa na Khaleefah Rashid katika vita vya kuikomboa Kashmir Iliyokaliwa?!

Enyi Waislamu wa Pakistan! Kataeni waziwazi sera ya kihalifu ya serikali ya kuzuia, ili simba wetu katika vikosi vyetu vya kijeshi waweze kunali viwango vya juu zaidi vya Pepo, kwa jasho lao, damu, moto na chuma. Takeni waziwazi kusimamishwa kwa Khilafah kwa Njia ya Utume, ili hatimaye tuwe na Imam anayetulinda na kuyaongoza majeshi yetu vitani. Mtume wa Mwenyezi Mungu (saw) amesema,

«إِنَّمَا الْإِمَامُ جُنَّةٌ يُقَاتَلُ مِنْ وَرَائِهِ وَيُتَّقَى بِهِ» “Hakika, Imam (Khalifah) ni ngao, watu hupigana nyuma yake na hujihami kwayo.” [Muslim].

Enyi Waislamu wa Jeshi la Pakistan! Toeni Nussrah yenu kwa ajili ya kusimamishwa tena Khilafah kwa Njia ya Utume (saw), ili muweze kutimiza wajibu wenu, bila kizuizi. Kuweni kama Maanswar ambao walimpa Nussrah Mtume wa Mwenyezi Mungu (saw), kiasi ya kuwa Mwenyezi Mungu (swt) aliwasifu katika Aya zake na malaika wakakimbilia kwenye mazishi ya kamanda wao, Sa’ad bin Muadh (ra). RasulAllah (saw) alisema kuhusu mazishi ya Sa’ad bin Muadh (ra),

«إِنَّ الْمَلَائِكَةَ كَانَتْ تَحْمِلُهُ» “Hakika, Malaika walikuwa wanambeba.” [Tirmidhi]

Afisi ya Habari ya Hizb ut Tahrir

katika Wilayah Pakistan

Hizb-ut Tahrir: Afisi ya Habari
Wilayah Pakistan
Address & Website
Tel: 
https://bit.ly/3hNz70q

Andika maoni

Hakikisha umejaza (*) habari zinazohitajika palipoashiriwa. Kodi za HTML haziruhusiwi.

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu