Logo
Chapisha ukurasa huu

بسم الله الرحمن الرحيم

 Hizb ut Tahrir / Wilayah Uturuki

Kisimamo cha Kulaani katika Mji wa Gaziantep Kuwazuia Mashoga Kuandaa Shughuli Zao!

Hizb ut Tahrir / Wilayah Uturuki ilitoa wito kwa Waislamu wenye ghera na dini yao kukusanyika katika uwanja wa Yeşilsu ili kuwazuia mashoga wanaojipa lakabu ya (LGBT) kuandaa shughuli ambayo hapo awali walitangaza nia yao ya kuandaa na kutoa kalima wakati huo huo katika uwanja huo huo.

 Shukrani kwa Mwenyezi Mungu na fadhila zake, Waislamu wa Gaziantep walikusanyika katika uwanja huo, wakiitikia wito wa Hizb ut Tahrir, na Ustadh Zinil Ak Demir akatoa kalima ambapo aliwataka kushirikiana na kusimama kama mwili mmoja dhidi ya kundi hili linataka kuleta ufisadi katika ardhi. Kwa shukrani na fadhila za Mwenyezi Mungu, watu wenye ghera miongoni mwa watoto wa Gaziantep waliweza kuwazuia mashoga kuandaa shughuli zao, na baada ya kuhakikisha kwamba walikuwa wamefikia lengo lao, umati ukatawanyika, huku ukipiga takbira na kumtukuza Mwenyezi Mungu (swt).

Kwa Mengi zaidi Bonyeza Hapa

Jumapili, 27 Dhul-Qa’adah 1443 H sawia na 26 Juni 2022 M

Kwa Maelezo Zaidi Zuru Mitandao ya Hizb ut Tahrir / Wilayah Uturuki:

Tovuti Rasmi ya Hizb ut Tahrir / Wilayah Uturuki

Ukurasa wa Facebook wa Hizb ut Tahrir / Wilayah Uturuki

Ukurasa wa Twitter wa Hizb ut Tahrir / Wilayah Uturuki

Akaunti ya Instagram ya Hizb ut Tahrir / Wilayah Uturuki

Chaneli ya YouTube ya Hizb ut Tahrir / Wilayah Uturuki

Tovuti ya Jarida la Kokludegisim

Template Design © Joomla Templates | GavickPro. All rights reserved.