Logo
Chapisha ukurasa huu

بسم الله الرحمن الرحيم

 Vichwa vya Habari 11/08/2021

Vichwa vya Habari:

  • Vita vya Kupigania Miundombinu
  • Mazoezi ya Kijeshi ya Pamoja ya China na Urusi
  • Ukandamizaji wa Saudia

Maelezo:

Vita vya Kupigania Miundombinu

Waziri wa Kigeni Antony Blinken alisema Jumatatu tarehe 9 Agosti kwamba Amerika lazima iwekeze zaidi katika miundombinu ili kushindana kiulimwenguni na China na nchi zengine wakati Seneti inajiandaa kupitisha sheria ya miundombinu ya $ 1 trilioni. Wakati wa hotuba katika Chuo Kikuu cha Maryland, Blinken alisema uwekezaji katika miundombinu ya umma nchini Amerika umekuwa ukipungua huku nchi zengine zikiongeza matumizi ya ndani. "Kwa mfano, China inatumia mara tatu zaidi yetu ya miundombinu ya tunavyofanya kila mwaka," alisema. Blinken alisema kuwa "ujadidishaji wa ndani" ni jambo "muhimu zaidi" Washington inaloweza kulifanya ili kuendeleza ajenda zake za sera za kigeni. Alionyesha uhusiano wa China pamoja na Urusi kama mashindano ya kimataifa kati ya demokrasia na tawala za kimabavu. "Hii ni muhimu sana haswa sasa, kwa sababu sio siri kwa yeyote kati yetu kwamba serikali za China na Urusi, kati ya zengine, zinatoa hoja hadharani na faraghani kwamba Amerika inaporomoka - kwa hivyo ni bora kuchagua na ruwaza zao za kimabavu kwa ulimwengu kuliko ile yetu ya kidemokrasia, "alisema. "Hakuna kitu kinachoweza kumaliza kwa haraka hoja yao ya uwongo kuhusu siku bora za Amerika kuwa zilishapita kwetu kuliko ikiwa Amerika itafanya uwekezaji mkubwa katika ujadidishaji wetu wa nyumbani hivi sasa." Rais Biden amekuwa akishinikiza mswada mkubwa wa miundombinu tangu aingie afisini na pia ameuweka kama muhimu mno ili kushindana na China. Katika hotuba yake ya kwanza kwa bunge la Congress, huku akiweka mpango wa miundombinu, Biden alisema Amerika ilikuwa katika mashindano na China ili "kushinda karne ya 21."

Mazoezi ya Kijeshi ya Pamoja ya China na Urusi

Urusi na China zimefanya mazoezi makubwa ya kijeshi ya pamoja katika mkoa wa Ningxia wa kaskazini ya kati wa China, mazoezi yanayojiri wakati wawili hao wakipambana na Washington na washirika wake wa Magharibi juu ya maswala anuwai, pamoja na haki za binadamu na wasiwasi wa usalama wa kieneo. Mazoezi ya Sibu / Ushirikiano-2021 yalizinduliwa Jumatatu na yataendelea hadi Ijumaa. Yatahusisha zaidi ya wanajeshi 10,000 wa ardhini na vikosi vya anga. Jeshi la Urusi limesema kwamba lilikuwa limetuma ndege za kivita aina ya Su-30SM, vitengo vya bunduki za magari na mifumo ya ulinzi wa anga kwenda China kama sehemu ya zoezi hilo. Mazoezi hayo yanaashiria mara ya kwanza kwa wanajeshi wa Urusi kutumia silaha za Kichina, na wawili hao wamefanya mazoezi ya pamoja tangu 2005, gazeti la Urusi la Kommersant liliripoti. Mazoezi hayo yanalenga "kuimarisha ... operesheni za pamoja za kupambana na ugaidi" na "kuonyesha dhamira thabiti na nguvu ya nchi hizo mbili kwa pamoja kulinda usalama wa kimataifa na kikanda na utulivu", Shirika la Habari la China Xinhua liliripoti, akitoa mfano wa maafisa wa China na Urusi. Richard McGregor, mtaalam wa China katika taasisi ya ufikiriaji mikakati ya Lowy Institute ya Australia, alisema uhusiano unaozidi kuongezeka kati ya Beijing na Moscow ulikuwa zaidi ya "ndoa ya manufaa". [Ibara] hiyo inadharau kina cha maslahi yao ya pamoja, na kwa kweli kubwa zaidi ni kuipinga Amerika na kuidhoofisha Amerika na Magharibi," McGregor aliiambia Al Jazeera.

Ukandamizaji wa Saudia

Mahakama nchini Saudi Arabia imetoa hukumu dhidi ya Wapalestina na Wajordani 69, ikitoa kifungo cha hadi miaka 22 kwa wengine huku pia ikiwaachilia huru idadi isiyojulikana mnamo Jumapili. Kundi hilo lilizuiliwa mnamo Machi 2018 wakati wa wimbi la ukamataji wa mamlaka za Saudi Arabia wa kundi la wakaazi wa muda mrefu wa Kipalestina na Jordan katika ufalme huo kwa madai ya uhusiano na kundi la "kigaidi" ambalo halikutajwa jina, kwa mujibu wa ripoti ya 2020 ya shirika la Human Rights Watch ( (HRW). Mahakama hiyo ya Saudia ilimhukumu mwakilishi wa Hamas nchini Saudi Arabia Mohammed al-Khudairi  miaka 15 gerezani. Mwanawe, Hani, alihukumiwa miaka mitatu. Al-Khudairi, 82, alikuwa kiongozi mkongwe wa Hamas aliyehusika na kusimamia uhusiano na Saudi Arabia kwa miongo miwili. Inaonekana hakuna chochote kisichoweza kufikiwa katika Saudi Arabia mpya, iwe ni matamasha yake, mbuga za mandhari au upigaji marufuku Hajj huku matamasha ya muziki yakifanyika. Kisiasa pia wale waliokuwa waungaji mkono wa ufalme huo kwa haraka wanajikuta sasa hawaipendelei tena.

Template Design © Joomla Templates | GavickPro. All rights reserved.