Logo
Chapisha ukurasa huu

Afisi ya Habari
Wilayah Pakistan

H.  12 Jumada I 1444 Na: 1444 / 18
M.  Jumanne, 06 Disemba 2022

 Taarifa kwa Vyombo vya Habari

Pelekeni Mapambano kwa Adui, Kupitia Kusimamisha Tena Khilafah ambayo Itaikomboa Kashmir Iliyokaliwa kwa Mabavu na Kuunganisha Pakistan na Afghanistan kama Dola Moja

(Imetafsiriwa)

Kwa kujibu maneno ya Luteni Jenerali Upendra Dwivedi wa India na Waziri wa Ulinzi Rajnath Singh, ni wakati sasa wa uongozi wa kijeshi wa Pakistan kuchukua hatua madhubuti. Maneno matupu kamwe hayatoshi, wakati hatua ndizo zinazohitajika, kujibu vitendo vya adui. "Mafundisho ya Bajwa" yalizuia jeshi letu kutofanya kazi, wakati India ikiiteka Kashmir Iliyokaliwa kimabavu, ilichochea machafuko katika maeneo ya kikabila na kujitahidi kuongeza ushawishi nchini Afghanistan. Uongozi wa kijeshi lazima sasa uchukue hatua, kuhamasisha vikosi vyetu vilivyo tayari na vilivyo na uwezo, kupeleka vita kwa adui.

Enyi Waislamu wa Pakistan! Adui India alileta vita kwetu, katika miaka ya Bajwa, akibadilisha hadhi ya Kashmir Iliyokaliwa kimabavu, mbele ya macho ya bunduki na mizinga yetu. Uunganishwaji wa Kashmir na India mnamo Agosti 2019, ulimiminia maji furaha yetu mnamo Februari 2019, wakati maafisa wetu jasiri walipotia hofu nyoyoni mwa Mabaniani waoga, na kufichua uzito wao halisi kwenye uwanja wa vita. Tangu wakati huo, vita vimekuwa tofauti na hapo awali, huku Bajwa akiamuru kujizuia, kutuvunja moyo na kumpa ujasiri adui. Lazima turudishe vita kwa adui. Ikiwa tutaendelea na "kujizuia" kwa Bajwa, basi maneno yetu kuhusu Kashmir yatakuwa matupu kama yale ya wanasiasa wafisadi.

Enyi Maafisa wa Jeshi la Pakistan! Yakanyageni Mafundisho ya Bajwa chini ya miguu yenu, kwa kuvuka Mstari wa Udhibiti na kuchukua hatua katika Kashmir Iliyokaliwa kimabavu. Kupigana na madhalimu kunahamasisha jeshi letu, kurudisha heshima na hadhi yake. Mtume (saw) kamwe hakujibu uchokozi wa kijeshi kwa maneno pekee. Ni wajibu wa kila afisa wa Kiislamu kutenda kulingana na Sunnah ya Mtume, kutafuta ushindi au kuuawa shahidi. Kashmir inayokaliwa kimabavu haiwezi kuzikwa chini ya Dola ya Kibaniani, kwa sababu Ardhi za Kiislamu zinazokaliwa kimabavu lazima zikombolewe, kulingana na Hukm ya Mwenyezi Mungu (swt). Mwenyezi Mungu (swt) ameamrisha,

[وَاقْتُلُوهُمْ حَيْثُ ثَقِفْتُمُوهُمْ وَأَخْرِجُوهُم مِّنْ حَيْثُ أَخْرَجُوكُمْ وَالْفِتْنَةُ أَشَدُّ مِنَ الْقَتْلِ]

“Na wauweni popote mwakutapo, na muwatoe popote walipo kutoeni; kwani fitina ni mbaya zaidi kuliko kuuwa.” [Surah Al-Baqarah 2:191].

Enyi Maafisa wa Jeshi la Pakistan! Pelekeni vita kwa adui! Utakeni uongozi wenu uhamasishe ujasusi ili kuwakusanya tena mujahidina wa pande zote mbili za Mstari wa Udhibiti. Utakeni uongozi wenu uchukue fursa ya kikanda kukomboa Kashmir Iliyokaliwa kimabavu, katika wakati ambapo India inakabiliana na China, isiyo na uwezo wa kusimamia vita katika pande mbili. Takeni kwamba mkusanywe dhidi ya adui, kwa kumtegemea Allah (swt) kwa ajili ya ushindi, kama yalivyofanya majeshi mengi ya Kiislamu yasiyohesabika kabla yenu, yakipata ujira wa Mwenyezi Mungu (swt) na Dua ya Waumini. Amesema Mwenyezi Mungu (swt):

[قَاتِلُوهُمْ يُعَذِّبْهُمُ اللَّهُ بِأَيْدِيكُمْ وَيُخْزِهِمْ وَيَنْصُرْكُمْ عَلَيْهِمْ وَيَشْفِ صُدُورَ قَوْمٍ مُؤْمِنِينَ]

“Piganeni nao, Mwenyezi Mungu awaadhibu kwa mikono yenu, na awahizi na akunusuruni muwashinde, na avipoze vifua vya kaumu ya Waumini.” [Surah At-Tawbah 9: 14].

Enyi Maafisa wa Jeshi la Pakistan! Utakeni uongozi wenu wa kijeshi uchukue hatua ya kwanza ili kuhakikisha kushindwa kikamilifu kwa India. Utakeni uongozi wenu wa kijeshi utoe msaada wa kimada (Nusrah), kwa ajili ya kusimamisha tena Khilafah kwa Njia ya Utume. Ni Khilafah huko nyuma, ndiyo iliyomtuma Jenerali Salahudin (rh) kuwaunganisha Waislamu chini ya Khalifah mmoja, kabla ya kuikomboa Ardhi ya Waislamu iliyokaliwa kwa mabavu. Ni Khilafah leo ndiyo itakayounganisha majeshi ya Waislamu kuwa jeshi moja kubwa zaidi duniani. Khalifah, anayetutawala kwa Uislamu, ndiye ambaye hatapumzika, mpaka kila shubiri ya ardhi ya Waislamu isafishwe kutokana na kukaliwa kimabavu. Hizb ut Tahrir inasubiri Nusrah yenu, basi itikieni.

Afisi ya Habari ya Hizb ut Tahrir katika Wilayah Pakistan

Hizb-ut Tahrir: Afisi ya Habari
Wilayah Pakistan
Address & Website
Tel: 
https://bit.ly/3hNz70q

Template Design © Joomla Templates | GavickPro. All rights reserved.