Afisi ya Habari
Wilayah Pakistan
H. 3 Rabi' II 1447 | Na: 09 / 1447 |
M. Alhamisi, 25 Septemba 2025 |
Taarifa kwa Vyombo vya Habari
“Khiyana ya ‘Ruwaibidha’ (watawala wasiostahiki) na kuidhinishwa kwa mpango wa Trump kwa gharama ya damu ya mashahidi wa Palestina”
(Imetafsiriwa)
Baada ya hotuba ya rais wa Marekani kwenye Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa – ambayo asili ilikusudiwa kuhakiki kadhia ya Palestina – na katika wakati ambapo, kwa msimamo mmoja kutoka zaidi ya dola 150 kati ya dola 193 za Umoja wa Mataifa, “dola ya Palestina” tayari imetambuliwa, Rais Trump aliikejeli jumuiya ya kimataifa kwa kuyaita maneno ya “viongozi” kama “domo tupu.” Pia alikejeli makubaliano ya kimazingira, akaiichukulia mikataba ya uhamiaji kuwa ya kudharauliwa, na akakashifu mchakato wa Ulaya wa kuitambua Palestina kwa kuiita udhaifu. Hotuba yake ilionekana kama dua ya mwisho ya mazishi (fatiha) iliyosomwa juu ya makubaliano ya kimataifa, madai ya mtazamo wa upande mmoja wa Amerika katika masuala ya kimataifa, na tangazo la kulazimisha rai yake juu ya Mashariki ya Kati – haswa suala la Palestina.
Baada ya hapo, huyu “Firauni mpya” alikutana na watawala wake watiifu na wanyenyekevu sana kwenye Baraza Kuu ili aweze kulazimisha maoni yake juu ya Umma wa Kiislamu kuhusu mustakabali wa ardhi iliyobarikiwa ya Palestina na kutoa maagizo kwa wale “Ruwaibidha” (watawala wasiostahiki) kuhusu kile wanachopaswa kufanya ili kutimiza azma yake na kutimiza ndoto ya dola ya Kiyahudi. Miongoni mwa aliokutana nao ni watawala wa Saudi Arabia, Qatar, Imarati, Misri, Jordan, Uturuki, na Indonesia, pamoja na Waziri Mkuu wa Pakistan Shehbaz Sharif. Kabla ya mkutano huu, katika mkutano wa video na wale wale “Ruwaibidha” (watawala wasiostahiki), Trump alikuwa ameweka wazi kile alichotaka kutoka kwa mkutano huu na kile ambacho wangelazimika kufanya. Alisisitiza kwamba muhimu kwake ni mateka, sio watu wa Gaza, ambao wanauawa kwa idadi kubwa zaidi kila siku. Alisema: “Lazima tuwarudishe mateka... na, ikilinganishwa na watu wengine ulimwenguni, watu wa hapa wanaweza kufanya kazi hii vizuri zaidi... kwa hiyo kuwa pamoja nanyi ni fahari kwangu.” Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani Marco Rubio pia alithibitisha hilo katika mahojiano na Fox News alipousifu mkutano huu wa kimataifa kama “juhudi za mwisho” za kumaliza mzozo wa Gaza na kuhakikisha kuachiliwa huru kwa wafungwa wa Kiyahudi waliosalia. Taarifa za Ikulu ya White House zinaweka wazi kuwa mpango wa Trump unajumuisha uondoaji wa hatua kwa hatua wa vikosi vinavyokalia kimabavu kutoka Gaza, kutumwa kwa vikosi vya kulinda amani vya kieneo, na mchakato unaoungwa mkono kimataifa wa mpito na ujenzi mpya. Washington inataka nchi za Kiarabu na Kiislamu kutuma vikosi vya kijeshi mjini Gaza ili kuwezesha uondoaji wa serikali inayokalia kwa mabavu na kudhamini rasilimali za kifedha kwa programu za mpito na ujenzi mpya.
Kutambuliwa kwa “dola ya Palestina” na dola nyingi za ulimwengu – ambayo, kiuhalisia, hakuna ardhi inayopakana nayo iliyobaki kwenye ardhi takatifu ya Palestina ambayo dola kama hiyo inaweza kuanzishwa – ni kutozingatia ukweli msingi ulioko uwanjani. Sio kwamba mambo haya yamefichika kwa wale wanaoitambua Palestina; wanajua kwamba umbile linalokalia kimabavu limebadilisha jiografia kiasi kwamba, hata kulingana na madai yao wenyewe, haiwezekani kuanzisha dola huru na yenye uwezo. Pia wanajua kwamba mvamizi tayari ana mamlaka na udhibiti wa vitendo juu ya ardhi nyingi, isipokuwa kwa miji michache mikubwa kwenye Ukingo wa Magharibi; hata kwenye ramani maeneo ya “Palestina” yanaonekana kama visiwa vidogo vilivyotawanyika baharini. Kwa hivyo, katika kadhia hii lengo halisi la kuitambua Palestina ni kurusha vumbi machoni mwa watu tu na kuiondolea jumuiya ya kimataifa jinai ya kuwahadaa watu wa ardhi iliyobarikiwa ya Palestina na damu inayomwagika usiku na mchana na majeshi yanayoikalia kimabavu – huku vikosi vinavyoikalia kimabavu vikipata msaada wa kijeshi, kiuchumi na kisiasa kutoka nchi hizo hizo. Ama kuhusu mwitikio wa Marekani na umbile linaloikalia kwa mabavu kutambuliwa kwa Palestina, ingawa haya ni mafanikio ya kidiplomasia kwa Marekani na umbile linaloikalia kimabavu ambayo wasingeweza kuyatazamia, inaonekana ilikusudiwa kuwasilisha tangazo la dola hii dhahania kama ushindi mkubwa kwa Wapalestina, faraja kwa wahasiriwa na maelfu ya waliouawa shahidi. Hivyo, kuhalalisha mahusiano na umbile linalokalia kimabavu kutathibitishwa kama utiifu wa watawala, na itatoa kisingizio chengine kwa nchi ambazo bado hazijafanya hivyo – kama vile Pakistan, Saudi Arabia na nchi zengine za ulimwengu wa Kiislamu – kufuata mkondo huo.
“Ruwaibidha” hawa waliokutana na Trump ni dola zinazoongoza na Ummah ambao uliundwa kama taifa bora kwa wanadamu. Sehemu ndogo ya wanajeshi wa nchi hizi ingetosha kuangamiza umbile la Kiyahudi na kumaliza minong'ono yake ya kishetani. Pakistan, ikiwa kama dola yenye nguvu za nyuklia, ina uwezo kamili wa kuwasaidia wapendwa wetu wanaokandamizwa mjini Gaza, na inamiliki nguvu za kuikomboa ardhi iliyobarikiwa ya Palestina na msikiti wa tatu mtukufu (Msikiti wa Al-Aqsa). Lakini maafa yanayoikumba Pakistan na kwengineko katika ulimwengu wa Kiislamu ni watawala hawa wa khiyana, wanaotumia uwezo wa nchi hizo kubwa kutumikia maslahi ya Marekani na kutimiza ndoto za Mayahudi katika ulimwengu wa Kiislamu. Hivyo basi, ni wazi kama muangaza wa mchana kwamba barabara ya kuelekea Msikiti wa Al-Aqsa inapitia kwenye makasri ya hawa “Ruwaibidha” (watawala wasiostahiki)—yaani, ni lazima wapinduliwe na Khilafah Rashida nyengine isimamishe kwa njia ya Utume, ambayo, kwa kufuata nyayo za mkombozi Salah al-Din al-Ayyub, itaitakasa Al-Aqsa kutoka na uchafu wa Mayahudi na washirika wao wa makruseda.
Hivyo basi, tunawalingania wanachama wenye nguvu wa Jeshi la Pakistan kuipatia Hizb ut Tahrir nasr (ushindi), ili kwamba bishara njema ya mtume inayohusiana na kuuawa kwa Mayahudi na kukombolewa kwa eneo la tatu takatifu iweze kutimia. Kupitia hilo, Ummah utaachwa huru kutokana na fedheha na udhalifu ambao ulilazimika kuonja mikononi mwa “maghdhubi alayhim” (waliokasirikiwa juu yao) na “ad-dhaalin” (waliopotea) na kupitia hilo mabustani ya Pepo yatapatikana.
[إِنَّ فِي ذَلِكَ لَذِكْرَى لِمَنْ كَانَ لَهُ قَلْبٌ أَوْ أَلْقَى السَّمْعَ وَهُوَ شَهِيدٌ]
“Hakika katika hayo upo ukumbusho kwa mwenye moyo au akatega sikio naye yupo anashuhudia.” [Surah Qaf 50:37]
Afisi ya Habari ya Hizb ut Tahrir Wilayah Pakistan
Hizb-ut Tahrir: Afisi ya Habari Wilayah Pakistan |
Address & Website Tel: +(92)333-561-3813 http://www.hizb-pakistan.com/ |
Fax: +(92)21-520-6479 E-Mail: htmediapak@gmail.com |