Logo
Chapisha ukurasa huu

بسم الله الرحمن الرحيم

 Kwa Wanajeshi Wenye Ikhlasi wa Mwenyezi Mungu (swt), Kutoka kwa Ummah wa Muhammad (saw)

(Imetafsiriwa)

Enyi maafisa wa Kiislamu wa majeshi ya Waislamu! Tunajua nyoyo zenu zinauma, mnapoiona nchi yenu ikiwa katika hali ya kukata tamaa kiuchumi, chini ya minyororo ya wakoloni wa IMF, huku raia wengi wakishuka chini ya mstari wa umaskini, wakishindwa kukidhi mahitaji ya chakula kwa familia zao.

Tunajua nyoyo zenu zinavuja damu, mnapoiona Quran Tukufu ikinajisiwa na nchi za Magharibi, ambao hutengeneza vikaragosi vya kipenzi chetu Mtume Muhammad (saw).

Tunajua munahisi uchungu pindi ndugu Waislamu wanapopigwa mabomu huko Gaza au Peshawar.

Tunajua kila mmoja wenu anajihisi mnyonge kama mtu ambaye anajiuliza, nifanye nini ili kubadili hali ya Ummah? Je, ninaweza kufanya nini peke yangu?

Ifahamike, hamuko peke yenu katika hisia zenu, bali shirikini hisia za Ummah huu uliobarikiwa.

Musikate tamaa na kuvunjika moyo kusikulemeeni. Haifai kwa muumini kukosa matumaini katika nyakati ngumu, achilia mbali mwanajeshi muumini.

Enyi wanajeshi wenye ikhlasi wa Mwenyezi Mungu (swt), hamko peke yenu katika hisia zenu kwamba Umma huu unahitaji kuunganisha watu na rasilimali zake, na kuhuisha izza yake, Khilafah iliyoufanya kutawala ulimwengu uliojulikana kwa zaidi ya miaka elfu moja.

Songeni mbele na muchukue hatua mikononi mwenu.

Washawishini wenzenu na wale walio mamlakani kutoa Nussrah kwa ajili ya kusimamisha tena Khilafah kwa Njia ya kipenzi chetu Muhammad (saw).

Mukifanya hivyo, mutafuata Sunnah ya Mtume (saw), na mifano inayong'aa ya Khulafaa Rashidin (ra).

Musipofanya hivyo, tutaendelea kukukumbusheni kiapo na wajibu wenu kwa Mwenyezi Mungu  (swt)!

Amesema Mwenyezi Mungu (swt):

[إِنَّ اللَّهَ اشْتَرَى مِنَ الْمُؤْمِنِينَ أَنفُسَهُمْ وَأَمْوَلَهُمْ بِأَنَّ لَهُمُ الّجَنَّةَ يُقَـتِلُونَ فِى سَبِيلِ اللَّهِ فَيَقْتُلُونَ وَيُقْتَلُونَ وَعْدًا عَلَيْهِ حَقًّا فِي التَّوْرَاةِ وَالإِنجِيلِ وَالْقُرْءانِ وَمَنْ أَوْفَى بِعَهْدِهِ مِنَ اللَّهِ فَاسْتَبْشِرُواْ بِبَيْعِكُمُ الَّذِى بَايَعْتُمْ بِهِ وَذَلِكَ هُوَ الْفَوْزُ الْعَظِيمُ]

“Hakika Mwenyezi Mungu amenunua kwa Waumini nafsi zao na mali zao kwa kuwa wao watapata Pepo. Wanapigana katika Njia ya Mwenyezi Mungu - wanauwa na wanauwawa. Hii ni ahadi aliyo jilazimisha kwa Haki katika Taurati na Injili na Qur'ani. Na nani atimizae ahadi kuliko Mwenyezi Mungu? Basi furahini kwa biashara yenu mliyo fanya naye. Na huko ndiko kufuzu kukubwa.” [Surah At-Tawba 9:111].

Imeandikwa kwa Ajili ya Afisi Kuu ya Habari ya Hizb ut Tahrir na
Umar Tariq – Wilayah Pakistan

Fuatilia na Usambaze Alama Ishara za Kampeni:

#Time4Khilafah

#EstablishKhilafah

#ReturnTheKhilafah

#TurudisheniKhilafah

#KhilafahBringsRealChange

#بالخلافة_يحصل_التغيير_الحقيقي

أقيموا_الخلافة#

كيف_تقام_الخلافة#

#YenidenHilafet

 #HakikiDeğişimHilafetle

Template Design © Joomla Templates | GavickPro. All rights reserved.