Alhamisi, 09 Shawwal 1445 | 2024/04/18
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

بسم الله الرحمن الرحيم

 [إِنَّ الَّذِينَ يُحَادُّونَ اللَّهَ وَرَسُولَهُ أُولَئِكَ فِي الْأَذَلِّينَ * كَتَبَ اللَّهُ لَأَغْلِبَنَّ أَنَا وَرُسُلِي إِنَّ اللَّهَ قَوِيٌّ عَزِيزٌ]

 “Hakika wanao mpinga Mwenyezi Mungu na Mtume wake, hao ndio miongoni mwa madhalili wa mwisho * Mwenyezi Mungu ameandika: Hapana shaka Mimi na Mtume wangu tutashinda. Hakika Mwenyezi Mungu ni Mwenye nguvu, Mwenye kushinda.” [Al-Mujadala: 20-21]

Kupitia Khilafah na Jihad katika Njia ya Mwenyezi Mungu,
Tutamnusuru Mtume wa Mwenyezi Mungu (saw) na Tutaukomboa Msikiti wa Al-Aqsa
(Imetafsiriwa)

Enyi Waislamu kote duniani:

Hakika mumeona chuki na sumu nyeusi ya Macron na wapambe wake dhidi ya Mtume wa Mwenyezi Mungu (saw). Hivi, wanachukia nini kuhusu Muhammad, Mtume wa Mwenyezi Mungu (saw)?! Wanaichukia dini ya Mwenyezi Mungu, dini ya haki, dini ya imani ya Mungu mmoja (Tawhid), kwa sababu hadhara ya Kifaransa na Kimagharibi ni hadhara ya kikafiri; ni batili na iliyopotoka, wanamchukia Mtume wa Mwenyezi Mungu (saw) anayelingania usafi na adabu na kuhifadhi heshima, pesa na damu; Kwa sababu hadhara yao ni hadhara ya uasherati, uchafu na upotovu. Wanamchukia Mtume wa Mwenyezi Mungu (saw), Nabii wa rehema, uongofu na mwangaza kwa walimwengu wote; Kwa sababu hadhara ya Kifaransa na Kimagharibi ni hadhara ya kikoloni yenye umwagaji damu ambayo imewaua watu na kupora bidhaa zao. Uhalifu wa Ufaransa dhidi ya Waislamu ni mwingi, kwa kuwa ilikuwa ndio kiongozi katika Vita vya Msalaba, na kuwaua takriban mashahidi milioni mbili nchini Algeria pekee.

Enyi Waislamu: Ni nini kilichompa ujasiri muovu, mdanganyifu Macron kumshambulia Nabii wetu na Dini yetu?!

Je! Angesubutu kutushambulia lau kama mtawala wetu angekuwa As-Siddiq au al-Faruq!! Au al-Rasheed au al-Mu'tasim!! Au Salahuddin au Sultan Abdul Hamid?! Je! Angesubutu lau kama Waislamu wangekuwa na dola?! Hapana, Wallahi, bali alipewa ujasiri na ugumu wa watawala wetu waovu, ambao wanaiona kejeli dhidi ya Mtume wetu na Dini yetu, ilhali hawateteleki wala kusema chochote!!! Mwenyezi Mungu na awachukie enyi watawala wa Waislamu, enyi wadhalilifu enyi waovu, kwani nyinyi ni washirika wa Macron katika uhalifu wake kwa kunyamaza kimya kwenu, na haitoshi kutoka kwenu kulaani na kukemea pekee, ama kuhukumu kwenu kinyume na yale yaliyoteremshwa na Mwenyezi Mungu, na kuwafanya vipenzi Mayahudi na Manaswara na kujitolea kwenu kwao, na kuyazuia majeshi ya Umma kutokana na Jihad katika njia ya Mwenyezi Mungu, na kuuangamiza Umma na kuufarakanisha ndio uhalifu na kosa kubwa zaidi, na hivi karibuni, Mwenyezi Mungu akipenda, ni siku ambayo tutapindua viti vyenu vya enzi, na kuwatupeni kwenye vumbi la historia.

Enyi Waislamu kote ulimwenguni, Enyi majeshi ya Waislamu:

Kumtukana Mtume wa Mwenyezi Mungu (saw) ni kuutukana Ummah na Dini yake, na jibu kwa Ufaransa na rais wake sio tu kwa kukemea, kushutumu na kususia bidhaa, lakini kwa kufunga mabalozi, kuhamasisha majeshi na kutangaza Jihad katika njia ya Mwenyezi Mungu (swt), na kwetu sisi kile ambacho Sultan Abdul Hamid alikifanya wakati alipozuia tamthilia ambayo ingemtusi Mtume wa Mwenyezi Mungu (saw) baada ya Ufaransa kutishia kutangaza vita dhidi yake ni shahidi bora, na kwa hili ni kosa kwa majeshi kukaa kimya na kutowajibu huku Waislamu binafsi binafsi wasio na ulinzi ndio wanao jibu, na inajulikana; Sio watu binafsi tu wanaostahiki kuwajibu maraisi wa dola; Badala yake, jibu lazima litoke kwa serikali kwa njia inayowafanya wanaomtusi Mtume wa Mwenyezi Mungu (saw) kudhalilika na kufedheheka.

Kutoka kwa Ardhi Iliyobarikiwa ya Palestina tunamwambia Macron, adui wa Mwenyezi Mungu na Mtume wake:

Chukua bishara ewe adui wa Mwenyezi Mungu na Mtume Wake, kwa kile kinacho kuchukiza zaidi, kwani uhalifu wa Ufaransa na Magharibi nyuma yake hautafutika kutoka kwa kumbukumbu ya Umma huu, na Khilafah inayokuja na Ufaransa na Magharibi kutakuwa na jambo kubwa mno, kwani sisi tuna miadi na Khilafah Rashida kwa njia ya Muhammad (saw) Vikosi vyake vitasonga kwa takbir na tahlil kuivamia Ufaransa na kuifungua Roma, ili kutanguliza ndani yake haki na kusambaza taa pembeni yake ... Hivi karibuni, ewe Macron, hebu tutaiondoa hadhara yako fisidifu, na tuisafishe ardhi kutokana na uchafu wa urasilimali wenu, hivi karibuni, Mwenyezi Mungu akipenda, tutakuhukumu kwa uaduilifu wa Uislamu na hadhara yake tukufu, ili watu wa Ulaya watambue jinsi walivyodanganywa na Mapinduzi ya Ufaransa na fikra zake zilizoporomoka, na jinsi walivyonyimwa haki na huruma ya Uislamu.

]وَسَیَعْلَمُ الْكُفَّارُ لِمَنْ ‌عُقْبَى الدَّارِ]

“…Na makafiri watajua ni ya nani nyumba ya mwisho Akhera!” [Ar-Ra’d: 42].

Enyi Waislamu: Pazeni sauti juu:

Enyi majeshi ya Waislamu, sisi tunakuiteni; Hakika nyinyi ni miongoni mwa Umma wa Muhammad (saw) Taifa bora lililoletwa kwa watu, na nyinyi ndio wenye nguvu, kwa hivyo nyinyi ndio mnastahili zaidi katika watu kumnusuru Mtume wa Mwenyezi Mungu (saw). Hakika tunakuombeni kuinusuru Dini ya Mwenyezi Mungu na kusimamisha Khilafah. Na hakika tumekuiteni kutokea Msikiti wa Al-Aqsa tunaomba nusra ya himaya yenu ili kuukomboa, na leo tunakuiteni tena kutoka Ardhi Iliyobarikiwa ya Palestina kuja kumnusuru Mtume wa Mwenyezu Mungu (saw), tokeni huku mkiwa mumejihami kwa wepesi na kwa uzito kuukomboa Msikiti wa Al-Aqsa, tunakusihini msikilize wito wa Mwenyezi Mungu na Mtume Wake (saw), na muwe wenye kumnusuru (maanswari) Mwenyezi Mungu na Mtume Wake, na fanyeni kazi na Hizb ut-Tahrir na muipe ahadi ya utiifu (bay'ah) kwake kusimamisha Khilafah ili isimamishe Dini ya Mwenyezi Mungu ardhini,

[قُلْ إِنْ كُنْتُمْ تُحِبُّونَ اللَّهَ فَاتَّبِعُونِي يُحْبِبْكُمُ اللَّهُ وَيَغْفِرْ لَكُمْ ذُنُوبَكُمْ وَاللَّهُ غَفُورٌ رَحِيمٌ]

“Sema: Ikiwa nyinyi mnampenda Mwenyezi Mungu basi nifuateni mimi, Mwenyezi Mungu atakupendeni na atakufutieni madhambi yenu. Na Mwenyezi Mungu ni Mwenye kufuta madhambi na Mwenye kurehemu.” [Al-i-Imran: 31]

H. 13 Rabi' I 1442
M. : Ijumaa, 30 Oktoba 2020

Hizb-ut-Tahrir
Ardhi ya Baraka-Palestina

Andika maoni

Hakikisha umejaza (*) habari zinazohitajika palipoashiriwa. Kodi za HTML haziruhusiwi.

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu