Jumatatu, 30 Rajab 1447 | 2026/01/19
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Barua ya Wazi kwa Mkurugenzi Mkuu wa ASIO Mike Burgess kutoka Hizb ut Tahrir / Australia

Kuhusu Khilafah, jaribio lako la kutia matope maji lilionekana wazi zaidi ulipopotoka wakati wa majadiliano yako ya baada ya muhadhara. Kwanza, ombi lako la mila za chuki dhidi ya Uislamu linawachora Waislamu kama daraja za tano katika nchi hii, inayothibitishwa kupitia kuwepo kwao tu, inazidi mipaka yote ya usawa na kutokuwa na upendeleo. Muhadhara huu kamwe haukuwa kuhusu kuwasilisha ukweli bali kuhusu kuendeleza ajenda.

Soma zaidi...

Hizb ut Tahrir / Wilayah Lebanon: Kongamano la Khilafah la kila Mwaka “Kuhalalisha Mahusiano na Kujisalimisha au Ahadi ya Mwenyezi Mungu na Dola ya Kiislamu?!”

Hizb ut Tahrir / Wilayah Lebanon yaandaa kongamano lake la kila mwaka kwa kichwa: “Kuhalalisha Mahusiano na Kujisalimisha au Ahadi ya Mwenyezi Mungu na Dola ya Kiislamu?!” Kwa mnasaba wa kumbukumbu uchungu ya miaka 105 ya kuvunjwa kwa dola ya Khilafah mnamo 28 Rajab 1342 H sawia na 3 Machi 1924 M

Soma zaidi...

Hizb ut Tahrir / Wilayah Sudan Ilifanya Kisimamo na Hotuba ya Hadhara huko Nile Mashariki jijini Khartoum

Mashababu wa Hizb ut Tahrir / Wilayah Sudan huko Nile Mashariki jijini Khartoum walifanya, mnamo Jumamosi, 10/01/2026, kisimamo na hotuba ya hadhara ya kisiasa huko Souq Sitta. Hotuba hiyo ilitolewa na Ustadh Hammad Al-Dayi, mwanachama wa Hizb, ambapo alielezea ubora wa Ummah huu, ambao ulitimiza wajibu wake katika kuwaongoza wanadamu chini ya Dola ya Khilafah, hadi ilipovunjwa na mkoloni kafiri mnamo Rajab 1342 H. Aliukumbusha Ummah kuhusu tukio hili uchungu, na jinsi, kwa kuvunjwa Khilafah, ulivyompoteza Imam ambaye ni ngao, umoja wake na kuchanika vipande vipande, na mkoloni kafiri akapata udhibiti juu yake ili kugawanya ardhi zake.

Soma zaidi...

Mwaliko wa Kuhudhuria Kongamano kwa Mnasaba wa Kumbukumbu ya Kuvunjwa Khilafah katika Hoteli ya Al-Busayri Plaza

Kwa mnasaba wa tukio la kupita miaka 105 ya hijriya tangu kuvunjwa kwa Dola ya Waislamu, Khilafah mnamo 28 Rajab 1342 H, na kama mwendelezo wa kuwakumbusha Waislamu faradhi ya kufanya kazi ya kuiregesha kama Dola ya Khilafah Rashida kwa njia ya Utume, Hizb ut Tahrir / Wilayah Sudan yatoa heshima kukualikeni kuhudhuria kongamano lenye kichwa: “Sudan Kati ya Sera ya Mipaka ya Damu na Sera ya Kuwaunda Watu Kuwa Ummah Mmoja”

Soma zaidi...

Mkutano na Hotuba katika Mji wa El Obeid

Kwa mnasaba wa kumbukumbu ya miaka 105 ya kuvunjwa kwa Khilafah, wanachama wa Hizb ut Tahrir walifanya mkutano na hotuba ya hadhara katika mji la El Obeid, mji mkuu wa Kordofan Kaskazini, mnamo Jumatano, 18 Rajab 1447 H, sambamba na 7 Januari 2026 M, katika uwanja wa Msikiti wa Soko la Al-Salihin.

Soma zaidi...

Hizb ut Tahrir / Wilayah Sudan Yafanya Visimamo Kadhaa katika Miji Tofauti Tofauti kote nchini Sudan

Ndani ya muundo wa mnasaba wa kumbukumbu ya miaka 105 ya kuvunjwa kwa Dola ya Khilafah mnamo Rajab 1342 H, na kama ukumbusho kwa Ummah wa tukio hili chungu, si kwa lengo la kulia juu ya historia tukufu iliyopotea, bali ili kuchochea azma ili Ummah uweze kutimiza wajibu wake wa kusimamisha Khilafah ili kuishi chini ya sheria za Mola wa Mlezi Walimwengu na kuondoa dhambi ya kifo cha Jahiliyyah kutoka shingoni mwake, Mashababu wa Hizb ut Tahrir katika Wilayah Sudan walifanya matembezi kadhaa katika miji tofauti kote Sudan, kufuatia swala ya Ijumaa mnamo 20 Rajab 1447 H, sawia na 9 Januari 2026 M

Soma zaidi...
Jiunge kwa hii RSS feed

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu