Jumamosi, 24 Muharram 1447 | 2025/07/19
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Mwaliko wa Kuhudhuria Mkutano na Waandishi Habari

Kwa ndugu na dada zetu waheshimiwa katika vyombo vya habari, ikiwa ni pamoja na magazeti, redio, na runinga, sisi, katika Hizb ut Tahrir / Wilayah Sudan, tuna furaha kukualikeni kuhudhuria mkutano na waandishi wa habari wenye kichwa: Hakuna Serikali inayoweza Kutoa Matumaini Isipokuwa chini ya Uislamu na Dola yake ya Khilafah.

Soma zaidi...

Ziara ya Azerbaijan: Hatua kuelekea Kusukuma Uhalalishaji Mahusiano na Umbile la Kiyahudi Ambayo Itakuwa ni Mchomo wa Kisu ndani ya Moyo wa Ummah

Chanzo cha kidiplomasia jijini Damascus kilisema mnamo Jumamosi kwamba mkutano wa moja kwa moja utafanyika kati ya afisa mmoja wa Syria na afisa mwengine wa 'Israel' huko Baku kando ya ziara ya Rais wa Syria Ahmad Al-Shara nchini Azerbaijan, kulingana na shirika la habari la Agence France-Presse (AFP).

Soma zaidi...

Bwawa la An-Nahdha: Silaha Mpya ya Marekani ya Kuvunja Utashi wa Misri na Kuzuia Ukombozi Wake kutokana na Utiifu

Tangu Ethiopia ilipotangaza ujenzi wa Bwawa la Kuu la Ethiopia la An-Nahda Dam kwenye  Nile ya Samawati mwaka 2011, uhalifu mkubwa wa kisiasa na wa kimkakati umekuwa ukijitokeza. Wale wenye ufahamu wanaona sio tu kama jengo la maji au mradi wa maendeleo, lakini kama chombo kipya cha kikoloni kinachotumiwa na Amerika kutawala eneo hili - hasa Misri, kitovu cha ardhi za Kiislamu, ambayo inakusudiwa kubaki kudhalilishwa chini ya shinikizo la kiuchumi, kisiasa, na hata la maji, kama sehemu ya mtindo mpya wa vita visivyo vya moja kwa moja.

Soma zaidi...

Mashambulizi ya "Warefu Tisa" yatamalizwa tu kwa Utekelezaji wa Adhabu za Sharia chini ya Dola ya Khilafah

Habiba Al-Amin, mwandishi wa habari wa tovuti ya Kush News, alishambuliwa vikali na wanachama wa genge la "Warefu Tisa" katika eneo la kivuko kwenda Port Sudan alipokuwa akiregea kutoka kwenye uangaziaji wa habari akiwa na wenzake kadhaa. Hili ni moja tu ya matukio mengi ya uporaji, ujambazi na mauaji katika miji inayodaiwa kuwa salama, kama vile Omdurman, Khartoum, na sasa mji mkuu wa utawala, Port Sudan. Hii ni miji iliyo chini ya udhibiti wa serikali na vyombo vyake vya usalama.

Soma zaidi...

Mfuko wa Fedha wa Kimataifa: Chombo Mikononi mwa Makafari cha Kudhibiti Sera ya Ndani ya Nchi Inayokopa

Mnamo Jumatano, 9/7/2025, Mfuko wa Fedha wa Kimataifa (IMF) ulionya kwamba uchumi wa Iraq unakabiliwa na changamoto kubwa. Bodi ya IMF, katika taarifa yake ya kuhitimisha mashauriano ya Kifungu cha IV na Iraq, ilisema kuna nafasi ya kuimarisha mapato yasiyo ya mafuta kupitia ongezeko la kodi na ushuru wa forodha.

Soma zaidi...

Mauaji ya Kikatili ya Sohag katika eneo la Midford la Mji Mkuu Dhaka, ni Matokeo Yasiyoepukika ya Siasa za Kisekula na za Kiwendawazimu zisizomtambua Mungu

Katika eneo la Mitford la mji mkongwe wa Dhaka, baadhi ya viongozi wa eneo la Jubo Dal, wakiongozwa na chama kikuu cha kisekula cha kisiasa nchini humu BNP, walimuua kikatili mfanyibiashara wa vyuma vichakavu aitwaye Sohag (39) kwa kumdunga kisu na kumpiga na jiwe kubwa mfululizo kwa kukataa kulipa pesa za ulaghai. Walioshuhudia walisema kwamba wahalifu hao hawakuishia kumuua tu, bali waliendelea kuonyesha unyama kwenye mwili mfu wa Sohag hata baada ya kifo chake kuthibitishwa. Mwili uliojaa damu, ulioganda uliachwa katikati ya barabara na wauaji wakasimama juu ya mwili huo huku wakisherehekea kiwendawazimu.

Soma zaidi...

Jibu la Swali: Kuamiliana na Dola zilizo za Kivita Kivitendo

Ndugu mmoja aliniuliza kuhusu kufanya kazi katika kiwanda cha kutengeneza makontena katika makaazi ya Barkan. Hivi majuzi, sehemu ya kiwanda hiki iligeuzwa kwa manufaa ya jeshi la ‘Israel’, na kinatengeneza matrela ya kusafirisha majenereta ya umeme na vitu vyengine vinavyohusiana na jeshi. Je, inajuzu kufanya kazi katika sehemu hii inayotengeneza matrela kwa ajili ya jeshi?

Soma zaidi...

Kwa Maongezi Matamu, Yenye Sumu kuhusu Mustakabali wa Lebanon na Kanda! Mjumbe wa Marekani Tom Barrack yuko nchini Lebanon Kuimarisha Kukamilishwa kwa Makubaliano ya Amani na Uhalalishaji Mahusiano na Umbile la Kiyahudi!

Mnamo Julai 7, 2025, katika mkutano na waandishi wa habari katika Kasri la Rais, Mjumbe wa Marekani Tom Barrack alitoa taarifa akisema kwamba "Lebanon na kanda hii wana fursa nzuri ambayo lazima ichukuliwe," kwamba "wakati umefika wa kubadilisha kanda hii," na kwamba "kila mtu amechoshwa na kile kilichotokea," kama alivyoweka. Pia alisema kwamba "usalama utavutia uwekezaji kwa Lebanon," kwamba "Rais wa Marekani alithibitisha dhamira yake ya kuchangia kujenga amani na ustawi nchini Lebanon," na kwamba "fursa inapatikana kwa Walebanoni kuifanya nchi yao kuwa Lulu ya Mashariki kwa mara nyingine tena."

Soma zaidi...
Jiunge kwa hii RSS feed

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu