Jumapili, 05 Jumada al-awwal 1447 | 2025/10/26
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Uzbekistan iko katika Hali Tete!

Uchumi wa Uzbekistan uliporomoka baada ya kuvunjika kwa Muungano wa Kisovieti na uhuru wake. Mamilioni ya Wauzbeki waliondoka nchini mwao kutafuta kazi, hasa Urusi, ambapo wakawa wafanyikazi wahamiaji, na wakabaki kwa miaka mingi. Dola hii ilishindwa kuwapa fursa za kazi, au kurekebisha uchumi. Ilishindwa kujenga viwanda na mitambo mipya, na badala yake ikabomoa vile vilivyokuwepo tangu enzi ya Usovieti.

Soma zaidi...

Mambo Muhimu Kuhusu Ziara ya Rais wa Syria, Ahmad al-Shara, jijini Moscow

Rais wa mpito wa Syria, Ahmad al-Sharaa, akifuatana na ujumbe rasmi uliojumuisha waziri wake wa mambo ya nje, Asaad Al-Shaibani, walizuru mji mkuu wa Urusi, Moscow, mnamo 15 Oktoba 2025. Walikutana na Rais wa Urusi Putin katika ziara yao ya kwanza rasmi tangu kuanguka kwa utawala wa Assad, mwishoni mwa mwaka jana.

Soma zaidi...

Hotuba ya Msemaji Rasmi wa Hizb ut Tahrir / Wilayah Sudan Katika Mkutano na Waandishi wa Habari mnamo Jumamosi 26 Rabi’ al-Akhir 1447 H sawia na 18/10/2025 M Anwani: “Mkanganyiko wa Serikali katika Jinsi ya Kudhibiti Miamala ya Dhahabu na Athari Zake

Baada ya kujitenga kwa Sudan Kusini mwaka wa 2011, na Sudan kupoteza zaidi ya 75% ya mauzo yake ya nje ya mafuta, dhahabu iliibuka kama njia badali kuu ya kufidia hasara hii na kupata faida kwa fedha za kigeni. Uchimbaji madini ulikuwa umeenea sana nchini Sudan baada ya karibu mwaka wa 2008, na uzalishaji wa dhahabu wa Sudan ukawa mkubwa, na kufikia tani 73.8 mwaka wa 2024, na kushika nafasi ya tano barani Afrika. (AlJazeera.net). Hata hivyo, uzalishaji huu mkubwa haukuinufaisha serikali wala watu; uliporwa na watu binafsi, na makampuni ya kigeni na ya ndani, na hata kile kinachozalishwa kupitia uchimbaji wa jadi hununuliwa na kutolewa kimagendo na baadhi ya makampuni na mashirika. Ili kuthibitisha kile tulichosema kuhusu hili, tunahakiki migodi mikubwa zaidi ya dhahabu nchini Sudan, kwa njia ya mfano na sio kipekee, na jinsi serikali inavyoshughulikia migodi hii!

Soma zaidi...

Mwaliko wa Kuhudhuria Mkutano na Waandishi wa Habari

Sisi, katika Hizb ut Tahrir / Wilayah Sudan, tunafuraha kuwaalika ndugu wanahabari, wanasiasa, na wale wanaopenda masuala ya umma kuhudhuria mkutano na waandishi wa habari ambapo msemaji rasmi wa Hizb ut Tahrir katika Wilayah Sudan atazungumza, wenye kichwa: Mkanganyiko wa Serikali Kuhusu Jinsi ya Kudhibiti Miamala ya Dhahabu.

Soma zaidi...

Mwaliko wa Kuhudhuria Kikao cha Kisiasa

Afisi ya Habari ya Hizb ut Tahrir katika Wilayah ya Sudan inafuraha kuwaalika ndugu zetu wanahabari, wanasiasa, na wote wanaopenda masuala ya umma kuhudhuria na kushiriki katika kikao kipya cha kisiasa, ambacho kitamkaribisha Ustadh Muhammad Jami’ (Abu Ayman), Msaidizi wa Msemaji Rasmi wa Hizb ut Tahrir katika Wilayah ya Sudan, chenye kichwa: Msimamo wa Serikali kuhusu Kufutwa kwa Kadhia ya Palestina na Hukmu ya Sharia juu yake.

Soma zaidi...

Muungano na Amerika hauruhusiwi kwa Pakistan, wala Muungano na India hauruhusiwi kwa Afghanistan

Waziri wa Ulinzi wa Pakistan Khawaja Asif mnamo Jumatatu (20 Oktoba 2025) alitupilia mbali madai ya Afghanistan kwamba Islamabad inatenda kwa niaba ya Marekani ili kuunda mabadiliko ya serikali jijini Kabul, akielezea madai hayo kama “upuuzi mtupu”. Islamabad imesema kwa muda mrefu kwamba India, hasimu wake wa muda mrefu, inafanya kazi pamoja na Afghanistan kusaidia Tehreek-e-Taliban Pakistan (TTP), ambayo inajulikana kama Taliban ya Pakistan, na wanamgambo wengine dhidi ya Pakistan. New Delhi inakanusha madai hayo.

Soma zaidi...

Watu Wapendao Uislamu wa Nchi Wameukataa Mkataba wa Julai, ambao umejengwa juu ya Msingi wa Usekula na Demokrasia Batili ya Magharibi, Na Wanataka Mkataba wa Madina uliojengwa juu ya Msingi wa Imani yao Safi ya Kiislamu

Mnamo 17 Oktoba 2025, kipote cha wanasiasa wenye uchu wa madaraka nchini humu walitia saini ‘Mkataba wa Julai - suluhisho la kisiasa lililoandikwa kwa kuzingatia imani potofu za kidemokrasia ya kisekula na mfumo wa Wakoloni makafiri wa Magharibi hasa Marekani-Uingereza, na kuweka mfano mwengine wa kuchukiza wa usaliti kwa Uislamu na Waislamu, na utiifu kwa nchi za Magharibi. Mfumo huu wa kisekula wa kibepari uliotungwa na wanadamu umefeli katika nchi zote duniani. Jambo hili ni la kweli mithili ya mwangaza wa mchana kwamba, mfumo huu wa ukandamizaji unalinda maslahi ya tabaka tawala, mabepari wachache na wakoloni wa Magharibi, na kuwanyonya watu wengi zaidi. Mnashuhudia kwamba kizazi cha vijana (Gen-Z) katika nchi nyingi wanaasi tabaka tawala la kibepari moja baada ya jengine na kuwaangusha watawala.

Soma zaidi...
Jiunge kwa hii RSS feed

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu