Ajali za Barabarani nchini Misri: Ushahidi Tosha wa Kukosekana kwa Ustawi wa Jamii na Ufisadi wa Mfumo wa Kirasilimali
- Imepeperushwa katika Misri
- Kuwa wa kwanza kutoa maoni!
- |
Katika tukio ambalo limekuwa la kusikitisha, watu waliamka siku chache zilizopita na kushuhudia maafa mengine ambayo yalisababisha vifo vya watu tisa wasio na hatia katika ajali iliyotokea kwenye Barabara ya Kanda katika Jimbo la Monufia, chini ya wiki moja baada ya maafa ya kuhuzunisha ambapo wasichana wachanga kumi na nane waliangamia katika ajali sawia, ikitofautiana na ile ya awali tu na kwa idadi ya wahasiriwa. Barabara ya Kanda - ambayo serikali imekuwa ikiitangaza kwa muda mrefu kama "mafanikio ya kitaifa" - imekuwa shahidi wa kudumu wa upuuzi wa yale yanayodaiwa kuwa mafanikio yanayosifiwa na watawala huku wakijificha nyuma ya mabango ya vyombo vya habari vya uwongo na kupuuza haki msingi ya watu: kuishi kwa usalama kwenye barabara ambazo hazinyakui maisha yao.