Gazeti la Al-Raya: Vichwa Vikuu vya Toleo 598
- Imepeperushwa katika Al-Rayah
- Kuwa wa kwanza kutoa maoni!
- |
Mnamo Jumamosi 02 Mei 2026 M, Hizb ut Tahrir / Wilayah Tunisia iliandaa kongamano la kila mwaka la Khilafah katika ukumbi wa mikutano na makongamano ulio katika makutano ya Sakiet Ariana katika mji mkuu wa Tunis, lenye kichwa: “Kufeli kwa Dola ya Kisasa na Kutoepukika kwa Dola ya Khilafah”
Kwa kuamini qadhaa ya Mwenyezi Mungu Mtukufu, Hizb ut Tahrir / Wilayah Syria inamuomboleza kwa Waislamu jumla, na kwa wabebaji dawah haswa, Ndugu Omar Abdul Rahim Khatib (Abu Abdo Khatib), mmoja wa wanachama wake, kutoka kijiji cha Arhab katika vijiji vya magharibi mwa Aleppo, na ambaye alifariki akiwa na umri wa miaka 50, ambayo aliitumia kwa utiifu kwa Mwenyezi Mungu Mtukufu.
Katika siku ya tatu ya Idd al-Fitr Iliyobarikiwa, sawia na Jumamosi, 12 Machi 2026 M, mashababu wa Hizb ut Tahrir/Wilayah Sudan walikusanyika katika afisi ya hizb katikati mwa jiji la Khartoum ili kupeana salamu za Idd. Mkutano huo ulijumuisha mashababu kutoka kote Khartoum, Omdurman, Jabal Awliya, Kalakila, Nile Mashariki, na maeneo mengine. Walitoa pongezi zao kwa Idd iliyobarikiwa na kuelezea furaha yao ya kuonana baada ya miaka mingi ya vita.