Gazeti la Al-Raya: Vichwa Vikuu vya Toleo 554
- Imepeperushwa katika Al-Rayah
- Kuwa wa kwanza kutoa maoni!
- |
Trump alisema katika chapisho kwenye jukwaa la Kijamii la ‘Truth’: ["Iran na Israel wanapaswa kufanya makubaliano, na watafanya makubaliano, kama vile nilivyozifanya India na Pakistan kufanya." Aliendelea: "Vivyo hivyo, tutakuwa na AMANI, hivi karibuni, kati ya Israel na Iran! Miito mingi na mikutano inafanyika hivi sasa."(Sky News,15/6/2025). Mnamo Jumapili, msemaji wa jeshi la umbile la Kiyahudi alisema kupitia jukwaa la X kwamba "Israel ilitoa onyo kwa Wairan wanaoishi karibu na vinu vya nyuklia nchini Iran kuhama makaazi yao." Wakati huo huo, msemaji wa jeshi la 'Israel' alisema kuwa jeshi lilishambulia kituo cha nyuklia katika mji wa Isfahan, katikati mwa Iran. Tangu alfajiri ya Jumapili, Iran ilianza kurusha raundi mpya za makombora kwenye shabaha ndani ya 'Israel', na kusababisha vifo na makumi ya majeruhi, na kusababisha uharibifu mkubwa kwa nyumba na majengo. Kwa kujibu, Tehran imekuwa chini ya mashambulizi ya 'Israeli'. (Al Jazeera,15/6/2025).
Ni Dhambi Kubwa Kwa Ndege za Mayahudi Kuvuka Anga ya Tawala, Kuipiga Mabomu Iran na Kurudi Salama Bila Kutunguliwa na Tawala hizi Hata kwa Risasi Moja!
Pongezi kutoka kwa Hizb ut Tahrir / Amerika kwa mnasaba wa ujio wa Idd ul-Adha 1446 H.
Pongezi kutoka kwa Hizb ut Tahrir / Wilayah Tunisia kwa mnasaba wa Idd ul-Adha 1446 H.
Pongezi kote ulimwenguni kutoka kwa kundi la wabebaji Dawah kutoka Hizb ut Tahrir kwa mnasaba wa Idd ul-Adha 1446 H.
Afisi Kuu ya Habari ya Hizb ut Tahrir: Pongezi za Kitengo cha Wanawake kwa Mnasaba wa Idd ul-Adha 1446 H