Jumatatu, 13 Jumada al-awwal 1447 | 2025/11/03
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Watawala wa Pakistan, Watu wa Trump, Wawateka nyara Mashababu wa Hizb ut Tahrir ili Kuhakikisha Kujisalimisha kwa Palestina

“Jenerali kipenzi cha Trump,” Asim Munir, amejibu kwa udhalimu kampeni yenye nguvu ya Hizb ut Tahrir katika Wilayah Pakistan, ambayo kwayo inataka uhamasishwaji wa haraka wa Vikosi vya Jeshi la Pakistan ili kuikomboa Palestina. Majambazi wa Asim Munir wamewateka nyara matetezi watano, kutoka Lahore, Karachi na Peshawar, na mahali walipo hapajulikani. Udhalimu wa Asim Munir unatarajiwa. Asim Munir hawezi kutenda, sembuse kufikiria, nje ya maagizo ya Trump katika suala lolote, iwe kuhusu Gaza, Kashmir, Afghanistan au rasilimali kubwa za madini za Pakistan.

Soma zaidi...

Ziara ya Asim Munir jijini Cairo ni Hatua ya Kutekeleza Ruwaza ya Trump kwa Mashariki ya Kati

Katika utekelezaji wa ruwaza ya Trump kwa Mashariki ya Kati, ambayo inatazamia kupandishwa cheo kwa umbile la Kiyahudi ndani ya ulimwengu wa Kiislamu baada ya usawazishwaji mahusiano, na kujumuishwa kwa serikali zote zilizopo katika ulimwengu wa Kiislamu ndani ya kile kinachoitwa ruwaza ya Mikataba ya Abraham, uhusiano wa hivi karibuni kati ya vibaraka wa Amerika katika ulimwengu wa Kiislamu umefanyika, kwa lengo la kutimiza ndoto za Trump katika eneo hilo.

Soma zaidi...

Watawala wa Pakistan wanaogopa mwamko wa Kiislamu unaoongezeka miongoni mwa Waislamu wa Pakistan na, kupitia utekelezaji wa Mpango wa Kitaifa wa Utendakazi, wanajaribu—bila mafanikio—kuusimamisha kwa kuigeuza Pakistan kuwa “dola ngumu zaidi.”

Mwenendo mkali na wa kikatili wa watawala dhidi ya mkutano wa TLP umesababisha mawimbi ya wasiwasi katika duara za kidini za Pakistan na kumshangaza kila Muislamu mwenye ufahamu. Hata hivyo, mbinu hii ya kiimla ya watawala wa Pakistan si kitendo cha pekee au kisicho cha kawaida; bali ni sehemu ya msururu wa hatua mfululizo ambazo watawala wamechukua katika siku za hivi karibuni, hatua zilizozidi wakati watawala wa Pakistan walipokubali kutekeleza mpango wa Trump pamoja na watawala wa nchi za Kiarabu na zengine za Kiislamu, mpango ambao lengo lake ni kulinda uwepo wa Mayahudi kutokana na upinzani wa Waislamu wa Palestina.

Soma zaidi...

Kuongezeka kwa Umwagaji damu kwenye Mpaka wa Pakistan na Afghanistan na Kushindwa kwa Pande zote mbili Kushikamana na Hukmu ya Mwenyezi Mungu

Mbali na sera ya “kujizuia” iliyotabanniwa na serikali za sasa za Pakistan na Afghanistan kwa maadui wa Umma – Mayahudi, Mabaniani, na Waamerika – Pakistan pamoja na Afghanistan zilitangaza kwamba makumi ya wanajeshi kutoka kila upande walikuwa wameuawa katika mapigano ambayo yalizuka kwenye mpaka wao wa pamoja. Makabiliano hayo yalianza mnamo Jumamosi jioni kwa operesheni iliyoanzishwa na vikosi vya Taliban, na kusababisha Islamabad kuapa kutoa jibu kali. Kabul, kwa upande wake, ilitangaza kuwa vikosi vyake vilifanya operesheni dhidi ya vikosi vya usalama vya Pakistan ili kulipiza kisasi kwa ukiukaji wa mara kwa mara na uvamizi wa anga unaofanywa na jeshi la Pakistan katika eneo la Afghanistan.

Soma zaidi...

“Khiyana ya ‘Ruwaibidha’ (watawala wasiostahiki) na kuidhinishwa kwa mpango wa Trump kwa gharama ya damu ya mashahidi wa Palestina”

Baada ya hotuba ya rais wa Marekani kwenye Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa – ambayo asili ilikusudiwa kuhakiki kadhia ya Palestina – na katika wakati ambapo, kwa msimamo mmoja kutoka zaidi ya dola 150 kati ya dola 193 za Umoja wa Mataifa, “dola ya Palestina” tayari imetambuliwa, Rais Trump aliikejeli jumuiya ya kimataifa kwa kuyaita maneno ya “viongozi” kama “domo tupu.” Pia alikejeli makubaliano ya kimazingira, akaiichukulia mikataba ya uhamiaji kuwa ya kudharauliwa, na akakashifu mchakato wa Ulaya wa kuitambua Palestina kwa kuiita udhaifu. Hotuba yake ilionekana kama dua ya mwisho ya mazishi (fatiha) iliyosomwa juu ya makubaliano ya kimataifa, madai ya mtazamo wa upande mmoja wa Amerika katika masuala ya kimataifa, na tangazo la kulazimisha rai yake juu ya Mashariki ya Kati – haswa suala la Palestina.

Soma zaidi...

Mayahudi Wanachimba Makaburi kwa Mikono Yao Wenyewe Huku Watawala wa Waarabu na Waislamu Wakiuzuia Ummah wa Kiislamu Usiwazike

Katikati ya milipuko ya mabomu na makombora ya umbile la Mayahudi, ikinyesha moto juu ya vichwa vya watu wetu mjini Gaza, ambapo wanalenga ghorofa za makaazi, vyuo vikuu, shule, hospitali na misikiti, hata kuangusha mahema chini, kiasi kwamba mifupa ya watoto na nyama zao inachanganyika na vifusi, “mkutano wa aibu na waovu” ulikusanyika na kufanywa. Ilikuwa ni mkutano wa kilele wa watawala Ruwaibidha duni, waovu kutoka miongoni mwa Waarabu na wasio Waarabu.

Soma zaidi...

Iwe ni Suala la Mafuriko au Kashmir, Suala la Uchumi au Kukaliwa Kimabavu kwa Mito Yetu na Dola ya Kibaniani —Je, Tutaendelea Kungoja ‘Jumuiya ya Kimataifa’ Mpaka Lini Kutatua Matatizo Yetu?

Baada ya mafuriko makubwa katika majimbo ya kaskazini ya Khyber Pakhtunkhwa, hasa katika Buner na maeneo ya karibu, ambapo mamia ya watu walipoteza maisha na nyumba, mifugo, mali na magari kusombwa na maji, mafuriko mapya sasa yanapitia Punjab na baadaye yataelekea Sindh. Hapo awali, Karachi pia ilikumbwa na mvua kubwa. Tunamuombea Mwenyezi Mungu Mtukufu usalama na kheri, kwani pamoja na utabiri zaidi wa mvua, watawala wetu wameinua mikono juu tu na kuliacha suala zima kwa rehema ya jumuiya ya kimataifa. Wanaendelea kuwasilisha suala hili zima kwa namna ambayo ni kana kwamba haya ni mabadiliko ya tabianchi ambayo hayawezi kudhibitiwa kabisa na wao, na ikiwa ‘jumuiya ya kimataifa’ haitaingilia kati, wataachwa bila msaada kabisa – kana kwamba ulinzi wa maisha na mali ya watu wao sio jukumu lao bali ni la mfumo wa kimataifa!

Soma zaidi...

Hali Baada ya Mvua na Mafuriko kwa Mara Nyingine Tena Imeweka Wazi Kuwa Waislamu Wanahitaji Mchungaji Khalifah

Tangu Juni 26, mafuriko katika maeneo mbalimbali ya Khyber Pakhtunkhwa, Punjab, na Karachi yamesababisha vifo vya zaidi ya watu 650 na kujeruhi zaidi ya elfu moja. Maelfu ya nyumba zimesombwa na maji, pamoja na akiba za maisha yote za watu, mali za nyumbani, na magari. Dada na mabinti zetu—ishara za staha na heshima—wamenyimwa nyumba na faragha zao, wakilazimishwa kuishi chini ya anga wazi.

Soma zaidi...

Ukosoaji wa Trump wa India ... Maslahi ya Amerika, Sio Urafiki na Pakistan

Mnamo 30 Julai 2025, Rais wa Marekani, Donald Trump alitangaza msururu wa ushuru wa kulipiza kisasi dhidi ya India, akiikosoa kwa kuwa na “vizuizi vizito na visivyo vumilika vya biashara visivyo vya ushuru” na kutoza ushuru wa forodha wa 25% pamoja na faini. Huku Trump alkikiri “urafiki” na India, aliikosoa vikali kwa kununua vifaa vya kijeshi vya Urusi na mafuta ya bei nafuu wakati Marekani ilikuwa ikiishinikiza Urusi kumaliza vita nchini Ukraine. Katika karipio la hadharani lisilo la kawaida, Trump aliusifu uchumi wa Urusi na India kuwa “umekufa” na akamuonya Rais wa zamani wa Urusi Medvedev “kuchunga mdomo wake.”

Soma zaidi...

“Siku ya Uhuru” ya 78 Pakistan Itakuwa Huru Kupitia Kuanzishwa kwa Khilafah Rashida

Chini ya mfumo wa sasa wa kimataifa, kile kinachoitwa uhuru si kitu zaidi ya usanii wa mchezo wa kuigiza, kwan maana ukombozi wa kweli (tahrir) uko pale tu dola inapoweza kupanga mambo yake ya ndani na mahusiano ya nje kwa mujibu wa itikadi yake. Watu wanaoamini “La ilaha illa Allah Muhammadur RasulAllah” kamwe hawatakombolewa kikweli mpaka watabikishe katika ardhi yao mfumo wa Kiislamu wa utawala, uchumi, jamii, elimu, na mahakama, pamoja na sera ya kigeni yenye msingi wa Da‘wah na Jihad. Hii ndiyo maana halisi ya uhuru, na katika suala hili, Pakistan bado haijakombolewa!

Soma zaidi...

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu