Jumamosi, 16 Jumada al-thani 1447 | 2025/12/06
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Uingereza, kupitia Wafuasi wake na Mabwege wake, Imarati na Serikali ya Al-Alimi, Yamezea Mate Aden na Bahari Nyekundu, Lakini Je, Kuna Mtu Yeyote Aliye Tayari Kuifukuza?

Vyombo vya habari ndani na nje ya Yemen vilisambaza, mnamo Jumanne, 18/11/2025, habari za kuwasili kwa Waziri wa Mambo ya Nje wa Uingereza anayeshughulikia Masuala ya Mashariki ya Kati na Afrika Kaskazini, Hamish Falconer, mjini Aden; ambapo alikutana na Rashad Al-Alimi, Mwenyekiti wa Baraza la Rais lenye wanachama wanane, na waziri huyo wa Uingereza pia alikutana na Waziri Mkuu Salem bin Buraik na Waziri wa Mambo ya Nje Dkt. Shaya Zindani, na mawaziri kadhaa, na Mwewe huyo aliandamana na Balozi wa Uingereza mjini Aden, Abda Sharif.

Soma zaidi...

Enyi Watu wa Sudan, Amerika Inaharakisha Kuvuna Matunda ya Vita vyake nchini Sudan, Kwa hivyo Msiiruhusu Itenganishe Darfur

Wakati wa hotuba yake katika Kikao cha Uwekezaji kati ya Marekani na Saudi Arabia, Rais wa Marekani Donald Trump alisema kwamba Mfalme Mtarajiwa Mohammed bin Salman alikuwa ameomba azimio la mgogoro nchini Sudan, akiongeza kwamba alianza kusoma suala hilo nusu saa tu baada ya maelezo ya Mwanafalme huyo. Trump pia aliandika kwenye tovuti yake ya Kijamii ya Truth kwamba atatumia mamlaka ya urais kusimamisha vita mara moja.

Soma zaidi...

Waislamu Maskini Wanastahili Zaidi Uwekezaji wa Watawala Wapumbavu Kuliko Amerika

Mfalme Mtarajiwa wa Saudi Arabia alifanya ziara nchini Marekani mnamo Jumanne, 18/11/2025, ambapo alionyesha kiwango cha upumbavu wake katika kufuja utajiri wa Ummah, kiwango cha utiifu wake kwa bwana wake Amerika, pamoja na kiwango cha usaliti wake kwa Ummah wa Kiislamu, njama yake dhidi yake, na vita vyake dhidi ya Mwenyezi Mungu (swt) na Mtume Wake (saw) kwa kukubali kujiunga na Makubaliano ya Abraham, yaliyowekwa katika usaliti mwingine ambao unahakikisha njia iliyo wazi ya suluhisho la dola mbili.

Soma zaidi...

Gaza Inavuna Mavuno Uchungu ya Baraza la Usalama na Uamuzi wa Baraza la Amani

Siku chache baada ya uamuzi wa Baraza la Usalama, watu wa Gaza walianza kuvuna hasara yake; katika muda usiozidi masaa 24, mashahidi 34—wengi wao wakiwa watoto na wanawake—walikuwa wamepanda daraja hiyo hadi kufikia Alhamisi asubuhi, 20/11/2025, pamoja na makumi ya waliojeruhiwa kutokana na uzito wa njaa na kwenye makucha ya baridi kali. Damu hizi safi zilikuwa maana halisi ya uamuzi ulioipa Amerika usimamizi na mamlaka juu ya Ukanda wa Gaza, ikiruhusu kukata vichwa kama ilivyotaka. Ni uamuzi uliopuuza damu, utajiri, na ardhi za watu wa Palestina katika Ukingo wa Magharibi na kuachilia mkono wa Mayahudi kutumbukia ndani ya damu yetu, ambayo ilienea zaidi ya Gaza hadi Kambi ya Ain al-Hilweh nchini Lebanon.

Soma zaidi...

Trump, Kupitia Azimio la Umoja wa Mataifa na kwa Msaada wa Watawala Waislamu, Anajiandaa Kuiweka Gaza na Eneo la Ash-Sham Chini ya Udhibiti wa Moja kwa Moja wa Kikoloni

Wakati wowote Amerika inaposhindwa kufanya jambo peke yake, hutumia mwavuli dhalimu wa Umoja wa Mataifa. Azimio la kishetani nambari 2803, lililoundwa kukandamiza upinzani wa Palestina, ni hila ya hivi karibuni ya Farauni wa leo, Trump. Kulingana na azimio hili ovu lililopitishwa tarehe 17 Novemba, ambalo serikali ya Pakistan ililipigia kura kwa aibu chini ya amri ya Trump, utawala wa Gaza utawekwa chini ya “Bodi ya Amani (BoP),” inayoongozwa binafsi na Farauni Trump. Azimio hilo hilo lililopitishwa tarehe 17 Novemba linatoa mamlaka kwa “Kikosi cha Kimataifa cha Utulivu,” kinachojumuisha wanajeshi kutoka nchi za Kiislamu, kulinda umbile la Kiyahudi na kupokonya silaha upinzani wa Palestina. Kivitendo, hili litakigeuza kuwa “Kikosi cha Ulinzi cha Israel” kinachofanya kazi chini ya amri ya Trump. “Bodi hii ya Amani (BoP)” na muundo wake wa usalama unaoambatana nayo itasimamia Gaza hadi tarehe 31 Disemba 2027, pamoja na uwezekano wa kuongezwa muda.

Soma zaidi...

Mauaji Mapya Yatekelezwa na Umbile Halifu la Kiyahudi katika Kambi ya Ain Al-Hilweh!

Katika muktadha wa kile ambacho Amerika inaendesha katika suala la amani na uhalalishaji mahusiano nchini Lebanon na eneo hili—ambapo kiuhalisia ni kusalim amri na kujisalimisha—umbile halifu nyakuzi la Kiyahudi, pamoja na silaha za Marekani, risasi za Ulaya, mikono ya Kiyahudi, na ushirika rasmi wa Waarabu, lililipua uwanja wa michezo na klabu ya michezo katika kambi ya Ain al-Hilweh katika mji wa Sidon kusini mwa Lebanon mnamo Jumanne, 18/11/2025. Mashahidi kumi na tano waliauwawa katika shambulizi hili la kikatili, na makumi ya watoto na raia walijeruhiwa, katika shambulizi baya linalothibitisha uhalifu wa umbile la Kiyahudi na uadui wake dhidi ya Waislamu.

Soma zaidi...

Ukosefu wa Masuluhisho ya Kudumu kwa Mgogoro wa Rohingya

Gazeti la ‘South China Morning Post’ liliripoti mnamo tarehe 10 Novemba kwamba Umoja wa Mataifa umeonya kwamba Kusini-mashariki mwa Asia kuna hatari ya “janga jengine la kibinadamu” ikiwa uvukaji wa bahari wa wakimbizi waliokata tamaa utaendelea bila kudhibitiwa. Vifo vya watu wasiopungua 21, wakiwemo watoto kadhaa, katika ajali ya boti karibu na pwani ya Malaysia vimeibua hofu ya kuongezeka tena kwa uvukaji hatari wa bahari wa wakimbizi wanaokimbia mzozo nchini Myanmar na hali mbaya katika nchi jirani ya Bangladesh. Kulikuwa na miili 12 iliyopatikana nchini Malaysia na tisa katika nchi jirani ya Thailand – kulingana na mkuu wa eneo wa shirika la bahari la Malaysia, Romli Mustafa.

Soma zaidi...

Ni Khilafah Rashida pekee kwa Njia ya Utume ndiyo itakayong'oa Mizizi ya Ukoloni wa Magharibi kutoka Ardhi Zetu

Kwa mwaliko wa Balozi wa Uingereza, Kumar Iyer, pamoja na Ujerumani, Ireland, Uholanzi, na Norway, Baraza la Haki za Binadamu la Umoja wa Mataifa lilifanya kikao mnamo Ijumaa, 14/11/2025, kuhusu ukiukaji katika mji wa El-Fasher. Baraza hilo lilipitisha kwa kauli moja azimio linaloiamuru Misheni Huru ya Kutafuta Ukweli, ambayo Baraza lilikuwa limeianzisha mnamo 11/10/2023, kuchunguza ukiukaji uliofanywa katika mji huo, ambapo Baraza liliamuru kuwatambua wote waliohusika, ili kusaidia kuwafikisha mbele ya sheria. Na kama mwendelezo wa mbinu yake ya kukataa misheni hii tangu kuanzishwa kwake, Waziri wa Sheria, Abdullah Darf, alitangaza katika mahojiano na tovuti ya habari ya uchunguzi jana, Jumapili 16/11/2025, kwamba “Sudan inakataa kupeleka uchunguzi kuhusu uhalifu wa Vikosi vya Msaada wa Haraka huko Al-Fashir kwa Kamati ya Kutafuta Ukweli.”

Soma zaidi...

Pakistan, Nchi Safi, Haiwakaribishi Wala Haiwasalimu Vizazi vya Khiyana vya Wasaliti

Baada ya kimya cha wafu makaburini cha serikali za vibaraka zinazobebesha mzigo ardhi za Waislamu, kuhusu mauaji ya Kiyahudi mjini Gaza kwa zaidi ya miaka miwili, vibaraka wa Amerika na Uingereza, washirika wa Mayahudi, walianza kuchukua hatua na kuwa wachangamfu katika kutekeleza mpango wa Trump wa kufilisi kile kilichobaki cha upinzani huko Palestina, kukandamiza na kuua watu mjini Gaza, na kubomoa kile ambacho Mayahudi hawakubomoa cha mawe. “Jenerali anayependwa zaidi wa Trump” Asim Munir alitembelea Jordan mnamo 26 Oktoba, na kwa badali yake, mnamo 16 Novemba 2025, Mfalme Abdullah II bin Al-Hussein, Mfalme wa Ufalme wa Hashimiya wa Jordan na Kamanda Mkuu wa Vikosi vya Wanajeshi wa Jordan, alitembelea Pakistan, akifuatana na binti yake Salma binti Abdullah II bin Al-Hussein, na ujumbe wa maafisa wa kiraia na kijeshi wa Jordan.

Soma zaidi...

Hotuba ya Msemaji Rasmi wa Hizb ut Tahrir / Wilayah ya Sudan katika Mkutano na Waandishi wa Habari yenye kichwa: Makubaliano ya Nchi Nne (Quartet) ya Kusitisha Mapigano na Hatari ya Mazungumzo kwa Msingi wa Hadhara ya Kimagharibi

Tangu Quartet—ambayo inajumuisha sambamba na Amerika, Saudi Arabia na Misri na Imarati, ilipotangaza taarifa yake mnamo 12/9/2025 kuhusu mgogoro wa Sudan, watu wengi nchini Sudan wamegawanywa katika mikondo miwili: mkondo unaounga mkono taarifa ya Quartet inayotaka mazungumzo na suluhisho la kisiasa, kwa kisingizio kwamba inaleta amani, na mkondo mwengine unaosema unakataa kile kilichokuja katika taarifa ya Quartet, na kutaka kuendelea kwa vita. Na ijapokuwa pande zote mbili ni Waislamu, hawakuufanya Uislamu kuwa ndio msingi wa kutoka kwao katika kubainisha misimamo yao, wakati ilitakiwa hapo awali jambo hili litokee

Soma zaidi...

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu