Jumatatu, 14 Muharram 1448 | 2026/06/29
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Je, Sio Wakati wa Ummah Kuwekeza Utajiri Wake Katika Kujenga Maslahi na Nguvu Zake Wenyewe?

Utajiri na rasilimali za Ummah zinaendelea kufujwa ili kutajirisha Magharibi, huku ndani ya nchi, zikitumika kwa anasa zinazowaweka Waislamu mbali na mfumo wa maisha wa Kiislamu. Mnamo Alhamisi, 21/5/2026, Mamlaka Kuu ya Burudani ya Saudi Arabia ilitangaza muungano mpya wa Saudi Arabia na Misri unaolenga kujenga mfumo jumuishi wa matukio makubwa katika eneo hilo, unaounganisha nchi hizo mbili kwenye njia moja ya kuvutia wasanii na nyota wa kimataifa! Wakati huo huo, mnamo Jumatano, 20/5/2026, nchi za Baraza la Ushirikiano la Ghuba (GCC) na Uingereza zilitangaza makubaliano ya kihistoria na makubwa ya biashara huria yenye thamani ya takriban dolari bilioni 5, na kuifanya Uingereza kuwa taifa la kwanza la G7 kusaini makubaliano kama hayo na kambi ya Ghuba.

Soma zaidi...

Ujumbe kutoka Hizb ut Tahrir / Wilayah ya Sudan Ulikutana na Kiongozi (Amir) wa Makabila ya Hausa Mjini Port Sudan

Mnamo Alhamisi, 21/5/ 2026, ujumbe kutoka Hizb ut Tahrir/ Wilayah ya Sudan, ukiongozwa na Mkuu wa Kamati Kuu ya Mawasiliano ya Hizb ut Tahrir/ Wilayah ya Sudan, Ustadh Nasser Ridha, akifuatana na Ustadh Abdullah Ismail, Mratibu wa Kamati ya Mawasiliano, walikutana na Amiri wa makabila ya Hausa katika Wilayah ya Port Sudan, Ustadh Salih Abdul Rahman, nyumbani kwake.

Soma zaidi...

Umaskini Ulioenea na wa Kimuundo Nchini Afghanistan: Matokeo ya Kufeli Kutabikisha Mfumo wa Kiuchumi wa Uislamu—Na Uendelevu wa Fikra ya Kiuchumi ya Enzi ya Jamhuri

Ripoti za hivi karibuni—ikiwa ni pamoja na ripoti ya kushtua ya BBC kutoka mkoa wa Ghor, kujichoma moto kwa mhandisi jijini Kabul, na simulizi zinazorudiwa rudiwa za watu wanaouza figo—zimefichua janga la kibinadamu linaloumiza moyo wa kila Muislamu. Katika baadhi ya miji, foleni ndefu za watu wanaotafuta kazi, njaa, na umaskini zimekuwa uhalisia unaoonekana. Wengine, wakiwa wamekandamizwa na umaskini na madeni, wamelazimika kuwauza binti zao wadogo ili kuokoa maisha ya wanafamilia wengine. Ripoti za UNDP zinaonyesha kwamba watu watatu kati ya kila wanne nchini Afghanistan hawawezi kukidhi mahitaji yao ya msingi ya maisha, na zaidi ya asilimia kumi ya idadi ya watu wako ukingoni mwa njaa.

Soma zaidi...

Msikose Fursa ya Kuunda Mfumo Mpya wa Kimataifa, Enyi Waislamu — Nyinyi Ndio Watu Wake na Mnaliweza hilo Kupitia Itikadi Yenu Tukufu

Hivi majuzi, Rais wa Urusi Vladimir Putin alitembelea China, na mwishoni mwa ziara hiyo taarifa ya pamoja ya zaidi ya nukta arubaini ilitolewa. Ndani yake, nchi hizo mbili zilitangaza mikataba na makubaliano kadhaa. Hata hivyo, kinachoonekana katika taarifa hiyo ni wito wa nchi zote mbili wa mpangilio mpya wa ulimwengu wa nchi nyingi. Pia inaeleweka kwamba ziara ya Putin nchini China ilikuja baada ya ziara ya Rais wa Marekani Donald Trump nchini China, na baada ya ziara ya Putin kukamilika ilitangazwa kwamba rais wa China anakusudia kutembelea Korea Kaskazini.

Soma zaidi...

Kama Hujui, Hilo Ni Janga; Lakini Kama Unajua, Basi Janga Ni Kubwa Zaidi!

Wakati wanasiasa wa Iraq na kambi zao wakigombea nyadhifa, matukio yanajitokeza ambayo yanathibitisha tena kwamba nchi hii si tu kwamba haina ubwana, bali pia kwamba maamuzi yake, ardhi, na anga zake vinakiukwa waziwazi na mtu yeyote na kila mtu. Amri za Marekani zinatolewa waziwazi na bila kuficha kuhusu uundaji wa serikali. Uingiliaji kati wa Iran kupitia kamanda wa Kikosi cha Quds cha Iran na ziara zake za mara kwa mara pia ni uko hadharani na haujafichika. Suala jengine lilikuwa ni ufichuzi wa ‘New York Times’ wa kuwepo kwa kambi mbili za kijeshi za umbile la Kiyahudi wakati wa vita vya Marekani dhidi ya Iran: moja katika Jangwa la Al-Nukhaib na nyingine katika jangwa la magharibi.

Soma zaidi...

Msamaha Jumla; Uadilifu Nusu ni Dhulma, na Hakuwezi Kuwa na Msamaha Jumla wa Kibaguzi!

Mnamo Mei 19, 2026, tovuti ya Lebanon Debate ilichapisha kile ilichokiita toleo la mwisho lililorekebishwa la sheria ya msamaha wa jumla. Ilionekana wazi kwamba sheria hii haikuwa ya jumla, ikiwajumuisha raia wote, bali iliundwa kwa vipimo vya kimadhehebu, ubaguzi, na hesabu finyu, zisizo na uwazi. Inaonyesha mwendelezo wa enzi ya dhulma iliyowekwa na utawala wa Assad mhalifu na wafuasi wake nchini Lebanon, na mtazamo unaokataa kuhama kutoka wazo la udhalimu hadi wazo la haki na usawa. Zaidi ya hayo, ukiukwaji wa kisheria uliibuka katika kuingiliwa kwa kimabavu wakati wa uandishi wa sheria ya msamaha wa jumla! Ni chini ya kanuni gani za kisheria au mifumo ya kimataifa ambapo kitu kama hicho kipo?! Ni katika chombo hiki dhaifu tu, ambacho kinathibitisha kila siku kwamba ni mkusanyiko tu wa madhehebu ambayo nchi imeundwa, si nchi ya kawaida ambapo madhehebu huishi pamoja kama mataifa mengine, mradi tu yachague mfumo wa utawala unaoegemea msingi wa utunzaji wa haki wa raia wake, usio na ukandamizaji na unyanyasaji wa kiholela!

Soma zaidi...

Hakuna Mwisho wa Mauwaji kwa Watoto wa Palestina na Lebanon Bila Kuondolewa kwa Umbile la Kiyahudi

Mnamo tarehe 13 Mei, UNICEF iliripoti kwamba angalau watoto 59 waliuawa au kujeruhiwa nchini Lebanon katika wiki iliyopita kutokana na shambulizi la umbile la Kiyahudi nchini humo. Tangu kuanza kwa usitishaji mapigano mnamo tarehe 17 Aprili 2026, angalau watoto 23 wameuawa na 93 kujeruhiwa, na kufikisha jumla ya watoto 200 waliouawa na 806 waliojeruhiwa nchini Lebanon tangu tarehe 2 Machi. Mapema mwezi huu, iliripotiwa kwamba msichana wa miaka 12 na baba yake waliuawa huko Nabatieh baada ya Jeshi la Ulinzi la ‘Israel’ kumlenga kupitia droni kwa mashambulizi matatu ili kuhakikisha kwamba haishi.

Soma zaidi...

Mwaliko wa Kuhudhuria Kikao cha Kisiasa

Afisi ya Habari ya Hizb ut Tahrir katika Wilayah Sudan ina furaha kuwaalika wanahabari, wanasiasa, na wote walio nah amu na masuala ya umma kuhudhuria kikao kipya cha kisiasa, kinachomkaribisha Ustadh Ibrahim Mushrif, mwanachama wa Afisi ya Habari ya Hizb ut Tahrir katika Wilayah Sudan, chenye kichwa: “Dori Iliyopewa Nchi Jirani katika Vita vya Sudan”

Soma zaidi...

ACSA na GSOMIA: Watu Wenye Ufahamu na Wanasiasa Wenye Ikhlasi Wanapaswa Kujitokeza Kuilinda Nchi Isije Kuwa Nchi ya Kitumwa

Inatisha sana kwa watu wa Bangladesh, wakati vyanzo mbalimbali vinathibitisha kwamba Marekani na Bangladesh zinaendelea na mfululizo wa mikataba ya ulinzi na biashara chini ya ‘Mkataba wa Biashara wa Pamoja (ART)’ wa kikoloni. Kampeni ya Marekani ya GSOMIA ilihama kutoka fahamu dhahania hadi ramani halisi mnamo Machi 2022, wakati Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani wa wakati huo Victoria Nuland alipowasilisha rasimu ya Mkataba Mkuu wa Usalama wa Taarifa za Kijeshi (GSOMIA) ndani ya mfumo wa Mkakati wa Marekani wa Indo-Pacifiki (IPS) ulitarajiwa mnamo 2017 na kuandikwa mnamo 2019. Ingawa ziara ya Nuland ilikuwa alama muhimu kwa GSOMIA, Mkataba wa Upataji na Huduma Mtambuka (ACSA) uliinuliwa rasmi mnamo Aprili 2019 na kuitekelezwa wakati wa Mazungumzo ya 7 ya Usalama jijini Dhaka.

Soma zaidi...

Hali Imefikia Hatua Ambapo Watawala wa Waislamu Wanacheza Kamari na Hatari ya Nyuklia Katikati ya Ardhi za Waislamu!

Afisi ya Habari ya Abu Dhabi iliripoti kwamba timu maalum za kukabiliana na dharura mnamo Jumapili zilidhibiti moto uliozuka katika jenereta ya umeme iliyoko nje ya eneo la ndani la Kiwanda cha Nguvu za Nyuklia cha Barakah katika eneo la Al Dhafra, kufuatia shambulizi la droni kwenye eneo hilo, bila majeraha yoyote au uvujaji wowote wa mionzi uliorekodiwa. Wizara ya Ulinzi ya Imarati ilieleza kwamba uchunguzi bado unaendelea ili kubaini chanzo cha mashambulizi hayo, ikibainisha kuwa maendeleo yoyote yatatangazwa mara tu uchunguzi utakapokamilika.

Soma zaidi...

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu