Ijumaa, 19 Ramadan 1445 | 2024/03/29
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Afisi ya Habari
Wilayah Bangladesh

H.  16 Safar 1444 Na: 1444 H / 04
M.  Jumatatu, 12 Septemba 2022

 Taarifa kwa Vyombo vya Habari

Hasina Alikamilisha Ushirikiano wa Ulinzi wa Nchi Mbili Pamoja na Dola ya Kishirikina-India ambao ni usaliti dhidi ya Waislamu na Uislamu; kuomba Ushirikiano kama huo wa Kijeshi ni Ukiukaji wa Dhahiri wa Onyo la Mtume wetu (saw):

«لَا تَسْتَضِيئُوا بِنَارِ الْمُشْرِكِينَ»

Musitafute Mwangaza kupitia Moto wa Washirikina

(Imetafsiriwa)

Huku watu wakipima uzito ziara ya Sheikh Hasina nchini India katika suala la kutoa na kuchukua, wengi huikosa kadhia nyeti ambauo alipiga pigo kubwa kwa vikosi vyetu vya jeshi na kuvifanya dhaifu kwa kile kinachoitwa Ushirikiano wa Ulinzi wa Nchi Mbili pamoja na India. Hasina alimwomba Modi kuharakisha utekelezaji uliocheleweshwa wa Njia ya Mkopo ya ulinzi ya Dolari milioni 500 (LoC) iliyopanuliwa na India hadi Bangladesh mwaka wa 2018. Anataka kulemaza majeshi yetu kwa kununua zana mbalimbali za viwango vya chini za India, kama vile meli ya mafuta, meli ya vifaa, kizimbani kinachoelea kwa Jeshi la Wanamaji la Bangladesh, na vifaru vya safu ya daraja, madaraja ya chuma yanayohamishika, magari ya ulinzi wa migodi, nk. kwa Jeshi la Bangladesh ingawa, kiuhalisia, jeshi la India linajulikana kwa zana zake za kizamani za kijeshi, risasi duni na utafiti na maendeleo yasiyo ya kutosha kutokana na kuegemea kupita kiasi uagizaji wa nje. (https://ukdefencejournal.org.uk/68-of-indian-military-equipment-is-vintage-say-officials/). Kuanzia kulichoma kisu cha mgongo jeshi letu kupitia kupanga mauaji ya Pilkhana hadi kulilemaza kwa kulifanya tegemezi kwa zana na vifaa duni vya Dola adui ya Kishirikina, Hasina ameendelea kuhujumu vikosi vyetu vya jeshi na kuharibu ari yake kwa kila njia. Tangu achukue mamlaka mwaka wa 2008, Hasina amekuwa akikabidhi mamlaka ya Ummah na mali ya kimkakati kwa India ili tu kukwamia mamlakani. Sio tu kwamba anatafuta usaidizi kutoka kwa dola hii adui yenye chuki ili kudhoofisha jeshi letu, bali pia anawalazimisha maafisa wetu wa kijeshi wanyofu na wapenda Uislamu kwenda kinyume na amri ya kukatikiwa ya kipenzi chetu Mtume wa Mwenyezi Mungu (saw):

«لَا تَسْتَضِيئُوا بِنَارِ الْمُشْرِكِينَ»

Musitafute Mwangaza kupitia Moto wa Washirikina (Ahmad na An-Nasai).

Tunajua India na watawala wake wa Hindutva ndio waliojitangaza kuwa maadui wa Waislamu. Walipanga njama ya mauaji ya maafisa wa jeshi huko Pilkhana, na kamwe hawajawacha kuwaua raia wasio na silaha mpakani mara kwa mara. Hata wakati wa ziara ya Hasina nchini India, hawakumwacha mvulana wa shule (“mvulana wa shule wa Bangladeshi auawa kwa kupigwa risasi na BSF”, Newage, 08 Septemba, 2022). Isitoshe, wanajitoa kimasomaso kumtukana Mtume wetu kipenzi (saw) na kuivunjia heshima Quran ya Mwenyezi Mungu. Uadui wao unadhihirika kwa kauli zao na vitendo vyao na Mwenyezi Mungu (swt) anatuonya kuhusu wao katika Kitabu chake,

[لَتَجِدَنَّ أَشَدَّ النَّاسِ عَدَاوَةً لِلَّذِينَ آمَنُوا الْيَهُودَ وَالَّذِينَ أَشْرَكُوا]

“Hakika utawakuta walio shadidi kuliko watu wote katika uadui kwa walio amini ni Mayahudi na washirikina.” [Surah Al-Ma'idah: 82]. Na ni kweli kwamba Wakoloni wa Makafiri kama vile Uingereza na Marekani wamekuwa wakipatiliza chuki hii dhidi ya Waislamu na kuikabidhi India dori ile ile katika Asia ya Kusini kama waliyoipa umbile haramu la Kiyahudi huko Mashariki ya Kati.

Enyi Waislamu, sisi, Umma wa Muhammad (saw), ni umma bora duniani ambao haustahiki kubaki chini ya aibu na udhalilifu usio na kifani. Tunahitaji kuwaondoa watawala na wanasiasa hawa wasaliti wa kisekula ambao uwepo wao ndio kizuizi pekee cha ukombozi wetu. Vibaraka hawa wanalelewa na maadui Makafiri-Washirikina ili kwamba sisi daima tubaki tumenaswa ndani ya mtego wao mbaya. Ndio maana tuliona hata vyama vya kisiasa vya upinzani vya kisekula kama BNP vilikaa kimya kuhusu mkataba wa kijeshi na India huku navyo vinaomba uungwaji mkono wa India katika uchaguzi ujao wa kitaifa. Hatuwezi kusubiri tena kurudisha makaazi yetu ya kweli ya heshima na adhama - Khilafah Rashida ya pili iliyoahidiwa kwa njia ya Utume. Historia inashuhudia kwamba ni Khilafah pekee ndiyo iliyozalisha watawala na viongozi ambao hawakuwahi kuomba usaidizi kutoka kwa Makafiri-Washirikina ili waingie madarakani tofauti na watawala wa kisekula wa leo wa nchi za Kiislamu. Badala yake ilitoa viongozi kama Musa bin Nusayr na Tariq bin Ziyad ambao walisaidia kurejesha heshima ya hata wasiokuwa waumini wa Uhispania na kuwaokoa kutoka kwa mtawala wao dhalimu Mfalme Roderic, mtawala wa mwisho wa Visigothi wa Hispania. Gavana wa wakati huo wa mji wa Ceuta wa Uhispania, Count Julian, alimwomba gavana wa Umawiyya Musa bin Nusayr msaada katika kulipiza kisasi cha udhalimu wa Mfalme Roderic kwa watu na kwa kutekwa nyara na kubakwa binti yake kwani alitaka kumuondoa madarakani. Kwa kujibu maombi hayo, jenerali wa Bani Umayya Tariq Ibn Ziyad na jeshi lake la askari 7,000 waliivamia Hispania mwaka 711 M, na wakaanzisha udhibiti wa Andalus kama Wilayah (gavana) chini ya Khilafah Umawiyya. Waislamu mara nyengine tena wanahitaji kuunganishwa chini ya uongozi shupavu wa Khilafah Rashida ambao hawataomba usaidizi wa Makafiri ili wawe madarakani, badala yake watawaondoa watawala madhalimu madarakani kama inavyohitajika ili kusimamisha uadilifu na usawa katika nchi za makafiri.

Mwenyezi Mungu (swt) asema,

[وَقَاتِلُوهُمْ حَتَّى لَا تَكُونَ فِتْنَةٌ وَيَكُونَ الدِّينُ لِلَّهِ]

“Na piganeni nao mpaka isiwepo fitna na mateso, na Dini yote iwe kwa ajili ya Mwenyezi Mungu.” [Al-Anfal: 39].

Afisi ya Habari ya Hizb ut Tahrir
katika Wilayah Bangladesh

Hizb-ut Tahrir: Afisi ya Habari
Wilayah Bangladesh
Address & Website
Tel: ‎+88 01798 367 640‎
www.ht-bangladesh.info
E-Mail: contact@ht-bangladesh.info, htmedia.bd@outlook.com Skype: htmedia.bd

Andika maoni

Hakikisha umejaza (*) habari zinazohitajika palipoashiriwa. Kodi za HTML haziruhusiwi.

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu