Jumamosi, 15 Safar 1447 | 2025/08/09
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Hizb ut Tahrir / Wilayah Sudan Yaandaa Kisimamo Mbele ya Msikiti Mkongwe jijini Port Sudan cha Kuinusuru Gaza

Hizb ut Tahrir / Wilayah ya Sudan imeandaa kisimamo mbele ya Msikiti Mkongwe jijini Port Sudan leo, Ijumaa, 7 Safar 1447 H sawia na tarehe 1 Agosti 2025 M, baada ya swala ya Ijumaa. Wanachama wa Hizb waliinua mabango yenye alama ishara: “Angusheni viti vya utawala vinavyozuia kusonga kwa majeshi kuinusuru Gaza.”

Soma zaidi...

Serikali ya Muungano Msingi ni Hatua ya Juu katika Kuharakisha Mpango wa Amerika wa Kutenganisha Darfur

Vikosi vya Msaada wa Haraka (RSF), kupitia muungano wao unaoitwa Muungano Msingi wa Sudan "Ta'sis," ulitangaza mnamo Jumamosi, 26/7/2025, uteuzi wa Rais na Makamu wa Rais wa Baraza la Rais, na Waziri Mkuu, ambayo ina maanisha kuundwa kwa serikali sambamba katika mamlaka inayoendeshwa na jeshi kutoka mji wa Port Sudan, mashariki mwa nchi.

Soma zaidi...

Yeyote Anayezuia Mkate Usifike Gaza Hapaswi Kuzungumzia kuhusu Utu, Ewe Waziri wa Mambo ya Nje Rafah: Imo ndani ya Tundu la Uvamizi... au imo Ndani Mshiko wa Serikali ya Misri?!

Katika mandhari ambayo hakuna jicho linaloweza kukosa kuiona, watoto wa Gaza wanasimama kwenye vifusi vya nyumba zao, wakikimbilia tama la maji, kipande cha mkate, au dozi ya dawa, wakati Waziri wa Mambo ya Nje wa Misri anajitokeza mbele yetu akizungumzia "nia ovu" na "heshima ya sera ya kigeni," katika jaribio la kuiondolea serikali ya Misri dori yake halisi katika mzingiro wenye kunyonga pumzi uliolazimishwa juu ya Ukanda wa Gaza.

Soma zaidi...

Pindi Milango Inapofungiwa wenye Njaa na Kunusuriwa Kukanyimwa, Sura Hasiri ya Serikali ya Misri na Wapambe wake Inafichuliwa

Katika wakati ambapo Gaza inastahamili moja ya nyakati kandamizi na za kikatili zaidi katika historia, ambapo, pamoja na kuuawa kwa mashambulizi ya mabomu, watoto wanakufa kwa njaa, wanawake kwa huzuni, na wazee kwa magonjwa, Meja Jenerali Khaled Mewaghar, Gavana wa Sinai Kaskazini, alitoa matamshi ambayo yanakinzana na matakwa rahisi zaidi ya  maadili ya kiakhlaki na ya kibinadamu matakwa ya udugu wa Kiislamu. Alisema: “Ikiwa watu wa Gaza watafikia kiwango fulani cha njaa, wana chaguzi tatu: ima kwenda upande wa Israel na kukabili milio ya risasi, kujitupa baharini, au kuelekea Misri—jambo ambalo haliwezekani.”

Soma zaidi...

Magereza ya Misri: Kati ya Mateso na Mauaji Pindi Heshima Inapokanyagwa Haki Huuawa!

Katika tukio jengine la mara kwa mara la uhalifu uliofichwa, kijana mmoja aitwaye Ayman Sabry alikufa ndani ya kituo cha polisi katika Jimbo la Dakahlia kutokana na mateso ya kikatili, ambayo yaliacha alama wazi kwenye mwili wake. Chini ya masaa 48 baadaye, kijana mwengine alikufa ndani ya Kituo cha Polisi cha Al-Saff katika Jimbo la Giza, huku kukiwa na ripoti thabiti za kutelekezwa kimakusudi, dhulma, na ukatili, na kuvigeuza vituo vya polisi kuwa sehemu za vifo cha polepole.

Soma zaidi...

Mustakabali wa Vita vya Kisasa na Dori Iliyokosekana ya Khilafah

Vita vinavyoendelea katika sehemu mbalimbali za dunia—hasa vita kati ya Urusi na Ukraine na mzozo kati ya Iran na umbile la Kiyahudi—vinaonyesha wazi kwamba ulimwengu umeingia katika awamu mpya na tofauti ya vita vya kijeshi na kijasusi. Mtazamo wa kale wa vita, uliopitwa na wakati, unaojengwa juu ya vikosi vikubwa vya askari wachanga, vifaru, na mizinga, unabadilika kwa kasi na kuporomoka. Leo, dola kama vile Marekani, China na Urusi zinatenga bajeti kubwa kwa viwanda vya juu vya kijeshi na zinafafanua upya mbinu mpya za kivita. Vita kwenye mstari wa mbele wa kisasa havikomei tena kwa risasi na bunduki – ni vita vya operesheni za kimahesabu (algorithms), akili ya bandia, droni, mtandao na mawimbi ya satelaiti.

Soma zaidi...
Jiunge kwa hii RSS feed

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu