Gazeti la Al-Raya: Vichwa Vikuu vya Toleo 505
- Imepeperushwa katika Al-Rayah
- Kuwa wa kwanza kutoa maoni!
- |
Ushiriki wa Hizb ut Tahrir/Ubelgiji katika amali za kampeni ya kilimwengu iliyozinduliwa na Afisi Kuu ya Habari ya Hizb ut Tahrir yenye kichwa “Enyi Umma; Kilio Wanacholia Wafungwa wa Dhamiri nchini Uzbekistan!”
Kwa kuzingatia mauaji ya kikatili (mauaji ya halaiki) ambayo yamekuwa yakiendelea kwa muda wa miezi saba, yanayofanywa na umbile halifu la Kiyahudi dhidi ya Waislamu wasio na ulinzi katika Ukanda wa Gaza, ambayo yamesababisha kuuawa shahidi na kujeruhiwa kwa Waislamu zaidi ya elfu 130, wanaume na wanawake hadi sasa, Hizb ut Tahrir / Wilayah Uturuki inaandaa amali kubwa za halaiki kote nchini Uturuki kuwataka Waislamu waungane chini ya bendera ya Khalifa mmoja ambaye atakusanya mara moja majeshi ya kuwanusuru Waislamu wanaodhulumiwa katika Ardhi Iliyobarikiwa (Palestina).
Afisi ya Habari ya Hizb ut Tahrir ya Wilaya ya Tunisia inaomboleza kifo cha mmoja wa mashababu wa Hizb ut Tahrir, mbebaji Da’wah kutoka kizazi cha kwanza katika safu zake, mwanachuoni wa lugha, Mwenyezi Mungu amrehemu, inshaAllah: Al Arousi Bin Amara.
Lau kama fikra za Hizb ut Tahrir zisingeenea sana nchini Uzbekistan, zisingekumbana na kiwango hiki cha kukamatwa na kuteswa, kwani maiti hapigwi vita.
Mnamo Juni 25, wawakilishi wa Oliy Majlis ya Jamhuri ya Uzbekistan walipitisha katika usomaji wa kwanza mswada unaokataza wazazi kupeleka watoto wao kusoma katika mashirika ya kidini ambayo hayajasajiliwa au kwa watu binafsi bila kibali kinachofaa. Mswada huo ulianzishwa na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Jamhuri ya Uzbekistan.
Licha ya mateso tunayoyapata kutokana na yale yanayowapata ndugu zetu wa Gaza na madhehebu ya Mayahudi ambao wamekuwa wabaya kwa muda mrefu, dhalimu wa Uzbekistan anajitokeza dhidi yetu kwa kuwakamata mashababu wa Hizb ut Tahrir na kuwatishia kwa vitendo vya ukandamizaji ni yale yale waliyoshtakiwa kwayo na Karimov aliyekufa, na ambayo walifungwa kwa karibu miaka ishirini, mashtaka ya kubuni ambayo hayana ushahidi.
Kalima kutoka kwa Ustadh Mahmut Kar, Mkuu wa Afisi ya Habari ya Hizb ut Tahrir katika Wilayah Uturuki, akiwawajibisha wahalifu waliowasha moto wa ufisadi katika mji wa Uturuki wa Kayseri baina ya wahamiaji wa Syria na wakaazi wa Uturuki ambao umeenea hadi miji mingi ya Uturuki.
Kauli za maafisa nchini Uturuki kuhusiana na maridhiano na utawala uliopitiliza na kufunguliwa kwa mipaka kwa ajili ya maandalizi ya uhalalishaji mahusiano na utawala huo, na vitendo vinavyouandama vya ubaguzi wa rangi dhidi ya watu wa Syria hasa wa Kayseri ni matokeo ya kimaumbile ya maneno ya uchochezi dhidi ya watu wa Syria, wakimbizi wanaoukimbia utawala wa Assad, na wanasiasa nchini Uturuki, wawe wenye mamlaka au wa upinzani, yote haya si lolote bali ni kuonyesha sura halisi ya utawala wa Uturuki, ambao unatekeleza mpango wa Marekani katika eneo hilo kufikia kile wanakiita suluhisho la kisiasa na kurudisha yale mabaki ya mji uliokombolewa kwenye kumbatio la utawala wa kihalifu.