Gazeti la Al-Raya: Vichwa Vikuu vya Toleo 606
- Imepeperushwa katika Al-Rayah
- Kuwa wa kwanza kutoa maoni!
- |
Tunawajulisha kwamba Mkuu wa Afisi ya Habari ya Hizb ut Tahrir / Wilayah Syria sasa ni Ustadh Ali Mustafa Al-Bakri, kuanzia 1 Muharram 1448 H, sawia na 16/06/2026 M, pamoja na shukrani za dhati kwa Ustadh Ahmad Abdul Wahhab kwa juhudi zake na kujitolea kwake katika miaka yake uongozi wa afisi hii.
Mwaka Mpya wa Hijri unatujia tarehe 1 Muharram 1448 H, sawia na 16/06/2026 M. Hii ndiyo tarehe iliyochaguliwa na Al-Faruq Umar ibn Al-Khattab na Maswahaba watukufu (ra) kama kalenda ya Waislamu. Alichagua tarehe hii kwa sababu iliashiria kuzaliwa kwa Dola ya kwanza ya Kiislamu iliyosimamishwa na Mtume wetu (saw) mjini Al-Madinah Al-Munawwarah.
Harakati maarufu katika majiji na miji kadhaa ya Syria, zinazojirudia kwa zaidi ya mnasaba mmoja baada ya kuanguka kwa utawala wa kihalifu uliokufa, hivi karibuni zaidi vuguvugu maarufu dhidi ya wale wanaoitwa Shabiha (majambazi), zinathibitisha ukweli kadhaa ambao haupaswi kusahaulika na watu wetu nchini Syria
Ghadhabu na hasira ziliongezeka nchini Tunisia wiki iliyopita kufuatia ajali nyingine mbaya, wakati huu katika wilaya ya Mazouna katika jimbo la Sidi Bouzid. Ajali hiyo iliwaacha wafanyikazi kadhaa wa kike wa shambani wakiwa wamejeruhiwa na wawili wakiwa wamekufa katika eneo la tukio. Tunisia inashuhudia kujirudia kwa matukio kama hayo kutokana na serikali kushindwa kukomesha usafiri usiodhibitiwa na kuboresha hali mbaya ya wafanyikazi wa kike wa mashamba! Bila shaka, serikali hii inakwepa kutoa tarakimu na takwimu sahihi zinazoonyesha ukubwa wa janga hilo!
Hizb ut Tahrir / Wilayah ya Sudan iliandaa amali katika afisi yake ya Khartoum kusherehekea Idd al-Adha kwa mwaka 1447 H (2026 M). Wakati wa amali hiyo, Ustadh Ibrahim Othman (Abu Khalil), msemaji rasmi wa Hizb ut Tahrir katika Wilayah ya Sudan, alitoa hotuba na kujibu maswali kutoka kwa waliohudhuria.
Ujumbe kutoka Hizb ut Tahrir Malaysia (HTM) uliwasilisha hati ya pingamizi kwa Wizara ya Mawasiliano huko Putrajaya kuhusu kuandaliwa kwa tamasha la “KL Headline Msimu wa 2026”. Hatua hii ilichukuliwa ili kuihimiza serikali kufuta tamasha hilo mara moja, kutokana na madhara makubwa ambayo lingesababisha kwa jamii na ukiukaji wake wa wazi wa sheria ya Kiislamu. Hati hiyo ilipokelewa na Bi. Wan Saidatul Shafina binti Mohamed Amin, Katibu wa Idara ya Mawasiliano ya Kimkakati na Masuala ya Taasisi, kwa niaba ya Wizara. Pia alitenga muda wa kusikiliza maelezo kamili na ya kina ya sababu za pingamizi zilizowasilishwa na Hizb ut Tahrir Malaysia.
Hizb ut Tahrir / Wilayah Lebanon: Maoni ya kila Wiki: “Udanganyifu wa Mazungumzo ya Fedheha!”
Kuala Lumpur iko tayari kuibuka kama mahali mwanana pa ziara za matamasha ya kimataifa barani Asia kupitia “KL Headline Msimu wa 2026,” ambao unakutanisha maonyesho 25 ya wasanii wa kimataifa katika mwaka mzima wa 2026. Mji mkuu wa Malaysia umepangwa kuwa mwenyeji wa maonyesho 25 ya wasanii wa kimataifa katika maeneo sita, yakiwalenga zaidi ya mashabiki 500,000 kutoka pwani za ndani na nje ya nchi - kulingana na mratibu, Live Nation Malaysia.