Ijumaa, 04 Dhu al-Qi'dah 1446 | 2025/05/02
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Hizb ut Tahrir / Wilayah Pakistan: Tunahitaji Jeshi la Waislamu Kuinusuru Gaza, sio “Mbwa Mwitu walio Pweke”!

Video ya afisa mmoja kijana wa jeshi wa Pakistan akitaka kwenda Gaza imesambaa, na wakati huo huo, video nyingine ya afisa sawia wa Misri imesambaa. Enyi maafisa wa majeshi ya Waislamu! Ikiwa hamuwezi kuleta tama la maji au tembe ya tende mjini Gaza, mutawezaje kumleta afisa aliyebeba bunduki?!

Soma zaidi...

Hizb ut Tahrir / Sweden: Kisimamo “Mauaji dhidi ya Raia mjini Gaza hivi sasa! Simama kwa Heshima!”

Kwa kuzingatia mauaji ya kikatili (mauaji ya halaiki) ambayo yamekuwa yakiendelea kwa zaidi ya miezi 18, yanayofanywa na umbile halifu la Kiyahudi dhidi ya Waislamu wasio na ulinzi katika Ukanda wa Gaza uliozingirwa, ambayo yamesababisha kuuawa shahidi na kujeruhiwa kwa zaidi ya wanaume na wanawake wa Kiislamu 180,000 hadi sasa, Hizb ut Tahrir / Sweden iliandaa kisimamo mbele ya ubalozi wa Marekani katika mji mkuu, Stockholm, chenye kichwa “Risala kwa Majeshi ya Waislamu!”

Soma zaidi...

Hizb ut Tahrir / Wilayah Pakistan: Enyi Wanazuoni wa Kiislamu! Wachocheeni Maafisa wa Jeshi Kupindua Uongozi wa Kijeshi, Vibaraka wa ukoloni!

Mnamo tarehe 11 Aprili 2025, Mufti Muhammad Taqi Usmani, jaji wa zamani wa Mahakama ya Shirikisho la Sharia, alisema kwamba jihad dhidi ya “Israel” ni faradhi kwa serikali zote za Waislamu. Hata hivyo, licha ya kutangaza kuwa ni wajibu, uongozi wa kijeshi haukukusanya vikosi vya kijeshi kuinusuru Gaza.

Soma zaidi...

Farauni wa Washington Afanya Maangamizu Makubwa Gaza, Kwa Usaidizi Kamili wa Viongozi wa Kijeshi na Kisiasa wa Waislamu na Mayahudi. Jibu Pekee la Kisharia ni Uhamasishaji wa Majeshi ya Waislamu. Enyi Waislamu! Songeni kwa ajili ya Faradhi ya Kishar

Bila jeshi hata moja la Waislamu kumzuia, Trump alitimiza ahadi yake ya kufanya maangamizi makubwa Gaza. Kamera zimenasa picha za sehemu za miili ya waumini zikipaa angani, juu ya majengo marefu, kutokana na kukithiri kwa mashambulizi ya makombora. Madaktari wa uokoaji wanafunikwa macho na kupigwa risasi. Watoto, wanawake, wazee na waliojeruhiwa wanauawa shahidi kwa kulipuliwa mahema yao. Sera ya njaa ya Amerika, iliyotekelezwa na wafuasi wake, umbile la Kiyahudi, imeongeza mateso hadi kiwango cha baa la njaa. Sasa imedhihirika kwa kila mtu kwamba Firauni wa Washington anafanya maangamizi makubwa kwa Gaza, kwa usaidizi kamili wa kijeshi na uongozi wa kisiasa wa Waislamu na Mayahudi.

Soma zaidi...

Hizb ut Tahrir / Wilayah Tunisia: Kongamano la kila Mwaka la Khilafah: “Kufeli kwa Serikali ya Kisasa na Kutoepukika kwa Dola ya Khilafah”

Hizb ut Tahrir/Wilayat Tunisia ilifanya kongamano lake la kila mwaka la Khilafah mnamo siku ya Jumamosi, 26 Aprili 2025, katika ukumbi wa mikutano kwenye makao makuu ya Hizb katika makutano ya barabara ya Sakra katika mji mkuu, Tunis, chini ya kichwa: “Kufeli kwa Serikali ya Kisasa na Kutoepukika kwa Dola ya Khilafah” Kumbi mbili zilizotengwa kwa ajili ya wageni zilijaa idadi kubwa ya wanaume na wanawake waliofika kwenye kongamano hilo kutoka pande zote za ardhi ya kijani ya Tunisia.

Soma zaidi...

Hizb ut Tahrir / Kenya Yafanya Kisimamo cha kutoa Wito wa Amali ya Kijeshi dhidi ya Umbile la Mauaji ya Halaiki la Kiyahudi

Kufuatia mauaji ya halaiki yanayoendelea kufanywa na umbile la Kiyahudi dhidi ya watu wa Gaza, Hizb ut Tahrir/Kenya mnamo siku ya Ijumaa tarehe 18 Aprili, ilifanya ilifanya kisimamo baada ya Swala ya Jumaa jijini Mombasa na Nairobi. Katika Jiji la Pwani, kisimamo kilifanyika nje ya Masjid Nur huku Nairobi kikifanyika katika Masjid Hidaya mtaa wa Eastleagh. Mada kuu ya Kisimamo ilikuwa ni kuibua wito wa dhati kwa Majeshi katika nchi za Kiislamu kuvunja minyororo ambayo watawala wao wamewaweka katika kambi zao ili wasonge mara moja kuukomboa Msikiti uliobarikiwa wa Al-Aqsa kutoka katika makucha ya Mayahudi wanaoukalia kwa mabavu.

Soma zaidi...

Hizb ut Tahrir / Wilayah Pakistan: Wito Uelekezwe kwa Kambi za Kijeshi na Ulinganizi wa Kuwaondoa Madarakani Watawala!

Mnamo tarehe 3 Aprili 2025, Jumuiya ya Ushirikiano wa Kiislamu ilitangaza kwamba “inalaani vikali uvamizi unaoendelea na unaozidi kuongezeka wa Israel.” Shirika hilo linajisifu kama “sauti inayounganisha ulimwengu wa Kiislamu.” Lakini watu wa Gaza hawahitaji “sauti,” bali vitendo kutoka kwa majeshi ya Waislamu.

Soma zaidi...
Jiunge kwa hii RSS feed

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu