Maumbile ya Mahusiano kati ya Uingereza na Urusi
- Imepeperushwa katika Al-Rayah
- Kuwa wa kwanza kutoa maoni!
- |
Maumbile ya mahusiano kati ya Uingereza na Urusi yamekuwa makali na yenye taharuki tangu karne ya 18, na uadui wa wazi na dhahiri kati yao. Kwa mfano, Dmitry Medvedev, Naibu Mwenyekiti wa Baraza la Usalama la Urusi, alisema mnamo Aprili 21, 2023, "Uingereza daima imekuwa, na sasa, na itakuwa adui yetu wa milele. Angalau hadi wakati ambapo kisiwa chao chenye majivuno kitazama ndani ya shimo la bahari kutokana na wimbi lililochochewa na mfumo wa kivita wa Urusi."