Jumatatu, 07 Muharram 1448 | 2026/06/22
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Mtoto Aliyeuawa Shahidi, Kuhesabiwa kwa Waathiriwa Kutaisha Lini? Watu wa Damu hiyo Watainuka Lini Kuwalipiza Kisasi?

Wizara ya Afya ya Palestina ilisema kwamba vikosi vya uvamizi vilifyatua risasi kwenye gari moja lililokuwa limebeba raia wa Palestina katika mji wa Hebron katika Ukingo wa Magharibi wa kusini unaokaliwa kimabavu, na kusababisha kifo cha kishahidi cha mtoto mchanga wa miezi saba Sam Abu Hikal huku akiwa mikononi mwa mamake. Mamake na babake pia walijeruhiwa.

Soma zaidi...

Enyi Ummah wa Kiislamu na Majeshi Yake: Ikiwa Hamkasirishwi kwa ajili ya Mwenyezi Mungu na Mambo Yake Matakatifu, Basi Mtakasirishwa na Kuchukua Hatua kwa ajili ya Nini?!

Mnamo Jumatano, 27/5/2026, vyombo vya habari na mitandao ya kijamii vilirusha picha zinazoonyesha vikosi vya umbile la Kiyahudi vikimshambulia kikatili mwanamke mchanga wa Kipalestina huko Bab Hutta, moja ya malango ya Msikiti mtukufu wa Al-Aqsa, vikimnyang'anya kitambaa chake cha kichwani kwa nguvu kabla ya kumkamata. Tukio hili linajiri huku kukiwa na ongezeko la ukiukwaji wa sheria na hatua za usalama ulioongezeka kutoka kwa vikosi vya uvamizi katika milango ya kuingia katika Jiji la Kale la Al-Quds na malango ya Msikiti wa Al-Aqsa, sanjari na Idd al-Adha. Waliweka vituo vya ukaguzi na kuchunguza vitambulisho vya wapita njia, wakizuia idadi kubwa ya watu kuingia msikitini.

Soma zaidi...

Jibu kwa Mwandishi wa Makala (Usekula na Ugumu wa Historia ya Uislamu Iliyoghushiwa)

Uislamu ni itikadi ya kiroho na kisiasa ambayo ilikuja kushughulikia matatizo ya wanadamu, kwa kutambua kwamba wanadamu wana silika (ghariza) na mahitaji ya kimwili ambayo yanahitaji kushibishwa. Uislamu umebainisha jinsi mahitaji haya yanavyopaswa kukidhiwa bila ya ziada au upungufu, kupitia hukmu kutoka kwa Mwenye hekima, Mjuzi wa yote. Yeye aliyewaumba wanadamu anajua kipi kuna manufaa na kipi kina madhara kwao! Ukosefu wa elimu wa mwandishi juu ya hukmu hizi haumwondolei jukumu; badala yake, unasisitiza kutoujua kwake Uislamu.

Soma zaidi...

Mwaliko wa Kuhudhuria na Kushiriki katika Kikao cha Kadhia za Umma

Tunafuraha, kama Hizb ut Tahrir / Wilayah Sudan, kuwaalika wanahabari, wanasiasa, na wote walio na hamu na masuala ya umma kuhudhuria na kushiriki katika Kikao cha kila mwezi cha Kadhia za Umma, ambacho mwezi huu kitafanyika katika afisi ya Hizb jijini Khartoum baada ya kukatizwa kwa muda mrefu kwa zaidi ya miaka mitatu kutokana na vita.

Soma zaidi...

Vikosi vya Msaada wa Haraka Vinafanya Mauaji Dhidi ya Watu Wasio na Silaha, na Serikali Haiwezi Kuwalinda!

Mnamo Alhamisi na Ijumaa, Mei 28 na 29, 2026, Vikosi vya Msaada wa Haraka (RSF) vilizindua mashambulizi kwenye vijiji vilivyo magharibi mwa mji wa Bara katika Jimbo la Kordofan Kaskazini, na kusababisha vifo vya raia kadhaa wasio na silaha. Mtandao wa Madaktari wa Sudan ulithibitisha katika taarifa mnamo Ijumaa, Mei 29, 2026, kwamba RSF ilifanya mauaji makubwa katika mji wa Al-Marra na vijiji vinavyozunguka, na kuwaua raia 27. Katika ripoti yake ya hivi karibuni mnamo Jumamosi, Mei 30, 2026, Al-Arabiya TV ilisema: “Idadi ya vifo kutokana na mauaji ya Vikosi vya Msaada wa Haraka katika eneo la Al-Marra huko Kordofan Kaskazini imeongezeka hadi 58.” Wakati Vikosi vya Msaada wa Haraka vinafanya mauaji haya katika vijiji vya Kordofan, serikali inalaani tu na kuhesabu waliokufa, bila kuchukua hatua zozote kali kuzuia mauaji haya kutokea.

Soma zaidi...

Ulaya Yahangaika Siku Chache Tu Bila Mafuta na Gesi ya Waislamu: Vipi Basi Ikiwa Ummah Ungeamka?!

Waziri wa Fedha wa Ufaransa Roland Lescure alisema kwamba serikali haziwezi kuamua kama zitoe akiba ya ziada ya mafuta ya kimkakati ili kupunguza usumbufu unaosababishwa na vita vya Iran hadi muda unaowezekana wa mzozo huo utakapokuwa wazi. Katika muktadha huo huo, mashambulizi ya awali ya makombora ya Iran kwenye kituo cha gesi cha Ras Laffan nchini Qatar, mojawapo ya vituo vikubwa zaidi vya gesi asilia vilivyoyeyushwa duniani, yalisababisha kupungua kwa kasi kwa akiba ya gesi ya Uingereza. Akiba ya gesi asilia nchini Uingereza ilishuka hadi viwango vya kutosha kukidhi matumizi ya ndani kwa muda usio zidi  masaa 48.

Soma zaidi...

Je, Sio Wakati wa Ummah Kuwekeza Utajiri Wake Katika Kujenga Maslahi na Nguvu Zake Wenyewe?

Utajiri na rasilimali za Ummah zinaendelea kufujwa ili kutajirisha Magharibi, huku ndani ya nchi, zikitumika kwa anasa zinazowaweka Waislamu mbali na mfumo wa maisha wa Kiislamu. Mnamo Alhamisi, 21/5/2026, Mamlaka Kuu ya Burudani ya Saudi Arabia ilitangaza muungano mpya wa Saudi Arabia na Misri unaolenga kujenga mfumo jumuishi wa matukio makubwa katika eneo hilo, unaounganisha nchi hizo mbili kwenye njia moja ya kuvutia wasanii na nyota wa kimataifa! Wakati huo huo, mnamo Jumatano, 20/5/2026, nchi za Baraza la Ushirikiano la Ghuba (GCC) na Uingereza zilitangaza makubaliano ya kihistoria na makubwa ya biashara huria yenye thamani ya takriban dolari bilioni 5, na kuifanya Uingereza kuwa taifa la kwanza la G7 kusaini makubaliano kama hayo na kambi ya Ghuba.

Soma zaidi...
Jiunge kwa hii RSS feed

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu