Ijumaa, 09 Muharram 1447 | 2025/07/04
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Maumbile ya Mahusiano kati ya Uingereza na Urusi

Maumbile ya mahusiano kati ya Uingereza na Urusi yamekuwa makali na yenye taharuki tangu karne ya 18, na uadui wa wazi na dhahiri kati yao. Kwa mfano, Dmitry Medvedev, Naibu Mwenyekiti wa Baraza la Usalama la Urusi, alisema mnamo Aprili 21, 2023, "Uingereza daima imekuwa, na sasa, na itakuwa adui yetu wa milele. Angalau hadi wakati ambapo kisiwa chao chenye majivuno kitazama ndani ya shimo la bahari kutokana na wimbi lililochochewa na mfumo wa kivita wa Urusi."

Soma zaidi...

Ongezeko la Wanamgambo nchini Sudan Linasonga Kaskazini!

Tangu Ijumaa, tarehe 27/6/2025, vyombo vya habari vimeripoti kuwa Rais wa Eritrea Isaias Afwerki amekubali kutoa mafunzo kwa wapiganaji elfu 50 kutoka majimbo ya Kaskazini na Mto Nile katika mafunzo ya juu ya kijeshi, kulingana na ombi lililowasilishwa na mkuu wa Jimbo la Kaskazini, Mohamed Sayed Ahmed Al-Jakoumi, mkuu wa Upande wa Kaskazini wa Makubaliano ya Juba ya Amani ya Sudan.

Soma zaidi...

Jibu la Swali: Uvamizi wa Umbile la Kiyahudi dhidi ya Iran na Athari zake

Al Arabiya ilichapisha kwenye tovuti yake mnamo tarehe 27/6/2025: "Vyanzo vinne vyenye taaarifa vilisema kuwa utawala wa Rais Donald Trump ulijadili uwezekano wa kuisaidia Iran kufikia hadi dolari bilioni 30 ili kujenga mpango wa nyuklia kwa ajili ya uzalishaji wa nishati ya kiraia. Vyanzo hivyo viliongeza kuwa majadiliano haya yaliendelea wiki hii baada ya kufikiwa kwa makubaliano ya kusitisha mapigano. Maafisa wa utawala wa Trump walithibitisha kwamba mapendekezo kadhaa yamewsilishwa, ya awali pamoja na yaliyoboreshwa, yakiwa na kifungu kimoja kisichobadilika, kisichoweza kujadiliwa : “kukomeshwa kabisa kwa urutubishaji wa urania ya Iran.”

Soma zaidi...

Kuibuka kwa Miungano Miwili Mipya ya Kijeshi katika Mashariki ya Kati, Caucasus, na Asia ya Kusini

Muungano kati ya Pakistan, Uturuki na Azerbaijan umekuwa ukichukua umbo kwa utaratibu uliopangwa, tangu viongozi wa nchi hizo tatu walipokutana kwenye mkutano wa kilele katika msimu wa kiangazi wa 2024. Mkutano huo uliwaleta pamoja Rais wa Uturuki Erdogan, Waziri Mkuu wa Pakistan, Shehbaz Sharif, na Rais wa Azerbaijan, Ilham Aliyev. Uliangazia mahusiano ya kisiasa kati ya dola hizo tatu, na kushughulikia masuala ya kikanda na kimataifa kama vile Gaza, Cyprus, Kashmir, na suala la chuki dhidi ya Uislamu.

Soma zaidi...

Bajeti Mpya ya Misri ni Kati ya Tarakimu Zinazopotosha na Ukweli Usiokuwepo

Mnamo tarehe 16 Juni 2025, Mbunge wa Misri Diaa El-Din Dawood alipinga rasimu ya bajeti kuu ya mwaka wa fedha wa 2025/2026, akionyesha kuwa serikali inadai kupunguza deni la umma, wakati takwimu zinaonyesha kinyume chake. Alibainisha kuwa deni la ndani na nje limeongezeka kwa kiasi kikubwa tangu mwaka 2018, na kufikia jumla ya pauni trilioni 11.5 za Misri mwezi Juni 2024. Alieleza kuwa mikataba iliyotangazwa na serikali haitafsiri matokeo yanayoonekana kwa wananchi, akikosoa kuendelea kwa matumizi ya sera hizo hizo za kiuchumi. Pia alieleza kuwa mapato ya deni na malipo ya awamu pekee katika bajeti mpya yanafikia karibu pauni bilioni 4,382.6 za Misri.

Soma zaidi...

Kuna Tofauti Kubwa kati ya Utu chini ya Uislamu na Udhalilifu chini ya Ukandamizaji wa Tawala za Kitumwa

Kamati ya Kuu ya Mitihani ya Cheti cha Sudan ilitoa wito kwa jumuiya ya kimataifa na mashirika husika kuendelea kuunga mkono juhudi za Wizara ya Elimu na kusaidia kuwawezesha wanafunzi wote wa Sudan kufanya mitihani, hasa katika maeneo yaliyoathiriwa na vita na hali ngumu ya kibinadamu. (SUNA, Juni 26, 2025)

Soma zaidi...

Tanzia ya Mbebaji Ulinganizi: Ustadh Yusuf Dhiab Al-Shalabi (Abu Diya')

Kwa imani kamili juu ya qadhaa ya Mwenyezi Mungu na kutaka malipo kutoka Kwake, Afisi ya Habari ya Hizb ut Tahrir / Wilayah ya Jordan inaomboleza kwa kuondokewa na mmoja wa wabebaji wake wa Da’wah: Ustadh Yusuf Dhiab Al-Shalabi (Abu Diya'), ambaye alifariki dunia kwenda kwenye rehema za Mwenyezi Mungu Mtukufu mnamo Alhamisi, tarehe 1 Muharram 1447 H sawia na 26 Juni 2025 M, akiwa na umri wa miaka 89, baada ya kuugua kwa muda mrefu ambapo alikuwa na subira na kwa kutarajia malipo ya Mwenyezi Mungu.

Soma zaidi...

Jinsi Dola Kubwa Zinavyozaliwa Utotoni mwao

Ni kweli kwamba dola kubwa hazizaliwi ghafla mara moja, lakini hakuna shaka kwamba zinajengwa juu ya itikadi ambayo kwayo mfumo huchipuka. Wakati wa kuzaliwa kwake, fikra yake ilijumuishwa katika kundi ambalo lilijitolea mhanga mali zake za thamani zaidi na kuiunga mkono kivitendo ndani yake. Hili lilizaa dola yake, ambayo ilijizatiti kujitengenezea njia kuelekea uongozi wa kimataifa kwa msingi wa itikadi yake, kufikia haki na rehema kulingana na viwango vya asili ya kimungu katika miongo michache tu. Ni lazima kwa Ummah ambao kwa hakika unataka kurudisha nafasi yake ya hadhi miongoni mwa mataifa, si tu duniani kote, kuregea kubeba ujumbe wake kwa ulimwengu na kulazimisha uongozi wake wa kifikra na utawala wake juu ya fikra za dhulma, ubabe, na utumwa, na kufikia ukombozi wa kifikra na wa kimada. Umma huu lazima uvuke hisia, mambo ya kijuujuu, na lugha ya maneno hadi vitendo.

Soma zaidi...

Wilayah Tunisia Tanzia ya Mbebaji Ulinganizi: Ndugu Basheer Qassila

Hizb ut Tahrir katika Wilayah ya Tunisia inaomboleza mmoja wa watu wake waliojitolea na wabebaji wa da'wah: mzee na kaka, simba wa da'wah, Basheer Qassila, ambaye alifariki mnamo Jumapili, tarehe 26 Dhul-Hijjah 1446 H, sawia na 22 Juni 2025 M, baada ya kupambana na maradhi yaliyomdhoofisha mwili wake lakini katu hayakuzima moto wa ujumbe wake wala azma yake ya kufanya kazi pamoja na safu akijitahidi kurudisha mfumo kamili wa maisha wa Kiislamu kwa kusimamisha Khilafah Rashida kwa njia ya Utume.

Soma zaidi...

Hizb ut Tahrir / Wilayah Tunisia: Matembezi ya Ukombozi: “Msafara wa Uthabiti Umesonga, Msafara wa Askari na Uanze!”

Matembezi yaliyohudhuriwa na umati mkubwa wa watu yalioandaliwa na Hizb ut Tahrir / Wilayah ya Tunisia yalitoka katika mji mkuu wa Tunis, baada ya swala ya Ijumaa, mnamo tarehe 20 Juni 2025 M kuanzia Msikiti wa Al-Fath chini ya kichwa: “Msafara wa Uthabiti Umesonga, Msafara wa Askari na Uanze!”

Soma zaidi...
Jiunge kwa hii RSS feed

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu