Alhamisi, 05 Rajab 1447 | 2025/12/25
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Wanawake wa Sumatra: Sio Tu Wahanga wa Mafuriko

Maafa ya mafuriko katika kisiwa cha Sumatra yamesababisha vifo vya watu 1,071 kufikia 19 Disemba kulingana na Abdul Muhari, Mkuu wa Kituo cha Data, Taarifa, na Mawasiliano ya Maafa katika Shirika la Kitaifa la Usimamizi wa Majanga la Indonesia (BNPB). Katika majanga, wanawake na watoto mara nyingi huwa waathiriwa mara mbili kutokana na udhaifu wa kimuundo, ikiwemo kupuuzwa kwa mahitaji ya afya ya uzazi ya wanawake. Taasisi ya Msaada wa Kisheria ya Banda Aceh (LBH) imesisitiza kwamba katika kila janga, wanawake ndio kundi linaloathiriwa zaidi lakini lisiloonekana sana—mpangilio ambao umethibitishwa tena katika mgogoro wa sasa.

Soma zaidi...

Utawala wa Uovu na Ghasia Utadumu kwa Muda Apendao Mwenyezi Mungu Uwepo!

Muhula wa bunge ulitarajiwa kuisha Novemba 2026, lakini rais alivunja bunge baada ya wabunge wanaounga mkono rais kuanzisha uchaguzi wa mapema wa bunge mnamo 25 Septemba. Uchaguzi ulifanyika dhidi ya mazingira ya kuzuiliwa kwa watu mashuhuri wa upinzani. Mnamo 24 Novemba wanachama wa chama cha upinzani cha Social Democratic Party Temirlan Sultanbekov na Ermek Ermatov, mwana wa rais wa zamani Kadyrbek Atambayev, na wengine walikamatwa. Zhaparov alifanya ujanja kama huo ili kuwaondoa wabunge wasiohitajika bungeni mnamo 2021.

Soma zaidi...

Kongamano la 2025 la Hizb ut Tahrir / Australia ‘Uislamu: Mabadiliko Ambayo Ulimwengu Inahitaji Sana’ Lahitimishwa kwa Mafanikio Makubwa

Hizb ut Tahrir / Australia ilikamilisha kwa mafanikio Kongamano lake la 2025 katika mazingira mazuri ya tafakari ya dhati na wasiwasi wa kweli kuhusu hali ya wanadamu na mwelekeo wake wa baadaye. Kongamano hilo lilijaa hotuba zenye hisia kali na hadhira iliyotiwa moyo na lilijumuisha ujumbe wa video unaotetemesha moyo kutoka katikati mwa Gaza iliyoharibiwa.

Soma zaidi...

Tishio la Kupiga Marufuku Hizb ut Tahrir nchini Australia

Kabla ya waathiriwa wa janga la Bondi hata kuzikwa, watetezi wanaounga mkono Uzayuni katika nchi hii walikuwa tayari wamekubaliana kuhusu simulizi yao na kuchochea orodha yao ya madai ya umma. Uchunguzi ndio umeanza tu, lakini watetezi wanaounga mkono Uzayuni katika nchi hii, wakichukua maelekezo kutoka kwa mhalifu wa kivita Netanyahu, wanasisitiza kwamba kipindi hiki chote kinaweza kuelezewa pekee kupitia jicho la chuki dhidi ya Mayahudi.

Soma zaidi...

Dola ya Kitaifa ndiyo Kikwazo Kikubwa Zaidi katika Kulinda Heshima na Maisha ya Waislamu Iwe nchini India au Gaza

Waziri wa Mambo ya Nje na Naibu Waziri Mkuu Ishaq Dar alilaani vikali tukio ambapo Waziri Mkuu wa Bihar Nitish Kumar alivua hijabu ya mwanamke wa Kiislamu Nusrat Parveen katika hafla ya serikali, akilitaja kuwa ‘la kuchukiza sana’. Dar alielezea tukio hilo kama la aibu, akisema lilionyesha haja ya haraka ya kulinda haki za wachache na kupunguza wimbi linaloongezeka la chuki dhidi ya Uislamu.

Soma zaidi...

Ukandamizaji Unaoongezeka wa Marekani dhidi ya Mashirika ya Kiislamu - Toleo la Texas

Katika hatua ya kushangaza wiki hii, Gavana wa Texas Greg Abbott alitangaza Baraza la Mahusiano ya Kiislamu na Kiamerika (CAIR) na Ikhwan al-Muslimin kama “mashirika ya kigaidi ya kigeni.” Tangazo lake linaharamisha makundi haya kumiliki mali huko Texas na kuidhinisha hatua za kisheria za serikali dhidi ya vyama vinavyohusiana nayo. Ingawa Abbott aliweka uamuzi huo kama msimamo dhidi ya “misimamo mikali,” hatua hiyo inawakilisha ongezeko kubwa la ulengaji unaoendelea wa mashirika ya Kiislamu na inaangazia mgogoro mkubwa wa uhuru wa kuzungumza, ukandamizaji wa serikali, na unafiki katika jinsi Amerika inavyowatendea raia wake Waislamu.

Soma zaidi...

Kifo cha Imam Fouad Saeed Abdulkadir: Pindi Hifadhi Inapogeuka Kuwa Mkasa

Idara ya Uhamiaji na Forodha ya Marekani (ICE) imethibitisha kifo cha Fouad Saeed Abdulkadir, raia wa Eritrea mwenye umri wa miaka 46, ambaye alifariki tarehe 14 Disemba akiwa kizuizini mwa ICE katika Kituo cha Ushughulikiaji cha Moshannon Valley huko Pennsylvania. Kulingana na ICE, Imam Abdulkadir anaripotiwa kupata maumivu ya kifua na kupokea uangalizi kutoka kwa wafanyikazi wa matibabu na huduma za matibabu za dharura. Kifo chake, mojawapo ya vifo kadhaa vilivyoripotiwa katika vituo vya ICE, bado kinachunguzwa na kimeongeza uchunguzi wa hali za uzuizi na upatikanaji wa huduma za afya za kutosha kwa wafungwa.

Soma zaidi...

Kipindi cha Tarique Rahman: Purukushani ya Kisiasa Kutoka kwa Mfumo wa Kisekula Uliovunjika

Huku Bangladesh ikiingia katika awamu muhimu ya kabla ya uchaguzi, kutangazwa kwa kurudi kwa Tarique Rahman, mwana wa Waziri Mkuu wa zamani wa Bangladesh Khaleda Zia na kaimu Mwenyekiti wa Chama cha Kizalendo cha Bangladesh (BNP), kumesababisha wimbi linalotabirika la umaarufu inaozingatia shakhsiya ya mtu. Simulizi hii, iliyokuzwa kwa ukali na chama chake, inamwakilisha kama suluhisho la pekee kwa changamoto za taifa. Lazima tuone hili kwa jinsi lilivyo: udanganyifu mkubwa wa kisiasa ambao unaficha kwa hatari uhalisia msingi wa mamlaka na mfumo wa leo.

Soma zaidi...
Jiunge kwa hii RSS feed

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu