Ijumaa, 18 Rabi' al-thani 1447 | 2025/10/10
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Mpango wa Trump wa Gaza ni Mpango Muovu wa Usaliti Unaolenga Kuangamiza Kadhia ya Palestina

Rais wa Marekani Donald Trump alitangaza kuwa Waziri Mkuu wa “Israel” Benjamin Netanyahu amekubali mpango wenye vipengee 20 ambao ungemaliza vita katika Ukanda wa Gaza. Trump na Netanyahu walifanya mkutano wa pamoja na waandishi wa habari baada ya mkutano wao jijini Washington. Trump alisema kuwa amani ya Gaza ilikuwa karibu sana kupatikana na kumshukuru Netanyahu kwa kuidhinisha mpango huo (DW Turkish 29.09.2025).

Soma zaidi...

Kuunganisha Fikra na Wabebaji Wake Ndio Njia ya Mabadiliko ya Kweli

Ni wazi, kwa wale wanaofanya kazi kwa ikhlasi kwa ajili ya kuhuisha Umma wa Kiislamu kupitia Uislamu, kile ambacho hali ya Ummah imefikia, kushambuliwa na mataifa mengine kama mwindaji anapolenga kwenye mawindo yake. Vile vile, ni dhahiri kwa wachunguzi jinsi Ummah unavyoelewa kwa uwazi uhalisia wake na kutambua sababu za mateso na maumivu yake. Kinachojulikana kwa Ummah kwa kiasi kikubwa kimefungika kwa makafiri wakoloni, watawala vibaraka, na tawala zilizowekwa na dola hizi za kikoloni juu ya shingo za Ummah ili kuukandamiza, kupora rasilimali zake, na kuuzuia kujikomboa kutoka kwa mshiko wa wakoloni kwa kusimamisha Khilafah kwa njia ya Utume.

Soma zaidi...

Misri Imenaswa Kati ya Kiu na Mafuriko! Gharama ya Miongo Kadhaa ya Uzembe na Mapuuza

Mgogoro wa mafuriko ambayo yalisomba baadhi ya vijiji vya Misri, na kuzamisha nyumba za makumi ya familia, ni sehemu moja tu ya mgogoro mkubwa na hatari zaidi. Mgogoro huu ni uzembe wa serikali juu wa haki za maji za Misri na kupuuza kwake kwa muda mrefu masuala ya wananchi na usimamizi wa rasilimali za nchi kwa ajili ya kulinda usalama wake na maslahi ya wananchi wake. Mgogoro huu haukutokea ghafla. Badala yake, ni matokeo ya mrundikano mtawalia wa sera zilizofeli ambazo zimekausha serikali zana zake za ulinzi wa maji na kufungua mlango kwa Ethiopia kudhibiti njia ya uhai wa Misri na Sudan kupitia Bwawa Kuu la An-Nahdha la Ethiopia.

Soma zaidi...

Kauli za Uhalalishaji Mahusiano ni Tangazo la Wazi la Kuoanishwa na Adui na Kujitenga na Ummah

Siku za hivi karibuni zimeshuhudia msururu wa kauli zilizotolewa na Waziri wa Mambo ya Nje wa Misri Badr Abdelatty wakati wa ushiriki wake katika makongamano ya kimataifa. Maarufu zaidi kati ya kauli hizi ni msisitizo wake juu ya “umuhimu wa 'Israel' kuishi kwa amani na kuoanishwa ndani ya eneo hili,” na “utayari kamili wa kuhalalisha mahusiano na ‘Israel’" pamoja na Saudi Arabia na nchi zengine, na kauli yake kwamba “suluhisho pekee kwa mustakbali ni kuanzishwa kwa dola ya Palestina isiyo na kijeshi inayoishi kwa amani na ‘Israel’.” Kauli hizi waziwazi zinaakisi mwelekeo unaofuatwa na tawala zilizoko katika nchi za Kiislamu: njia iliyojaa uhalalishaji mahusiano na umbile nyakuzi, na hata juhudi za kulilinda na kulioanisha ndani ya eneo hili, kuhudumia mradi wa kikoloni wa Magharibi.

Soma zaidi...

Uacheni Umma Ufanye Uamuzi Wake, Enyi Watawala Waoga!

Hatukushangazwa, wala Umma wa Kiislamu haukushangazwa na ukaribishaji wa watawala wasaliti wa Waislamu wa mpango wa rais wa Marekani Donald Trump wa kuipoteza Gaza, kwani wao wametuzoezesha sisi kuwa waoga, badala ya kula njama na wakoloni makafiri dhidi ya masuala yetu. Trump alikuwa amekutana na baadhi yao jijini New York kando ya mikutano ya Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa, mnamo Jumanne tarehe 23/9/2025, na wakamsifu na kutangaza kumtegemea yeye kumaliza vita dhidi ya Gaza. Mara tu Trump alipotangaza mpango wake wa ukoloni, waliharakisha kuukaribisha. Wasingewezaje kuukaribisha, wakati hakuna hata mmoja wao aliyesubutu kufanya vyenginevyo, kwa kuwa wamepoteza ari na ushujaa wa wanaume.

Soma zaidi...
Jiunge kwa hii RSS feed

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu