Jumanne, 14 Dhu al-Hijjah 1446 | 2025/06/10
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Pongezi kwa Idd Al-Adha Iliyobarikiwa 1446 H

Hizb ut Tahrir inatoa pongezi na baraka nyingi zaidi kwa Umma wetu mpendwa wa Kiislamu, wenye subira na wenye kukubali malipo licha ya maafa na majanga yote unaopitia, maafa na majanga ambayo ni mzigo mzito hata kwa kundi lililo imara zaidi la wanadamu, hususan watu wetu wenye subira mjini Gaza na katika Ardhi Iliyobarikiwa ya Palestina, katika Sikukuu ya Idd ul-Adha. Tunamuomba Mwenyezi Mungu azijaalie siku za Idd hii kuwa ni utulivu katika nyoyo zao na wanyanyuliwe daraja mbele ya Mola wa walimwengu wote.

Soma zaidi...

Jibu la Swali: Mashambulizi ya Droni na Yanayojiri katika Vita nchini Sudan

Siku za hivi karibuni zimeshuhudia maendeleo ya ajabu katika vita. Droni zilishambulia Port Sudan, mji mkuu wa utawala, kwa siku sita mfululizo, na kushambulia uwanja wa ndege wa kiraia, kambi ya anga, na maghala ya mafuta, na kusababisha mgogoro wa mafuta kote nchini. Droni pia zilishambulia mji wa Kassala kwenye mpaka wa Eritrea upande wa mashariki, pamoja na miji mingine. Haya yote yalisababisha vikosi vya jeshi kuondoka kuelekea upande wa El Fasher na kuzingatia kulinda Sudan mashariki, kama BBC ilivyoripoti mnamo tarehe 10/5/2025. Je, hii ina maana kwamba shambulizi la mashariki mwa Sudan linalenga kuliondoa jeshi kutoka Darfur, na kuiacha ikiwa chini ya udhibiti wa Vikosi vya Msaada wa Haraka (RSF) pekee? Je, matukio haya ni utangulizi wa Jukwaa la Jeddah (kongamano la mazungumzo)? Au kuna malengo mengine?

Soma zaidi...

Hatimaye, Dhalimu Trump Anahitimisha Ziara yake katika Kanda hii

Trump alianza ziara yake nchini Saudi Arabia mnamo Mei 13, 2025, ikifuatiwa na Qatar mnamo Mei 14, 2025, akihitimisha safari yake nchini Imarati mnamo Mei 15, 2025, na kuhitimisha ziara yake mnamo Mei 16, 2025. Kisha aliandamanisha ziara hii kwa udanganyifu wake kwamba hatazuru umbile la Kiyahudi, kuwakejeli wajinga wanaodai kuwa uungaji mkono wa Trump kwa umbile la Kiyahudi umetikiswa! Hii ni licha ya ukweli kwamba umbile la Kiyahudi lilipanua mashambulizi yake kwenye Ukanda wa Gaza baada ya Trump kuondoka katika nchi hizo tatu.

Soma zaidi...

Jibu la Swali: India, Pakistan, na Usitishaji Mapigano

Trump alitangaza kwa mshangao jana, Jumamosi, katika chapisho kwenye jukwaa lake la Ukweli wa Kijamii (Truth Social platform), kwamba "Baada ya usiku mrefu wa mazungumzo yaliyopatanishwa na Marekani, ninafurahi kutangaza kwamba India na Pakistan zimekubali kusitishwa kwa mapigano kamili na mara moja, "na kuzisifu nchi zote mbili kwa kutumia busara na akili kubwa." (Al Jazeera, 11/5/2025) ... ni upi ukweli katika uhasama na mzozo huu? Je, Mkataba wa Maji wa Indus ni nini haswa ambao India imeusitisha kwa muda? Je, Marekani inahusika katika kuanzisha shambulizi hilo na pia kulisitisha?

Soma zaidi...

Jibu la Swali: Dola ya Kina (Deep State)

Neno “dola ya kina” (deep state) limetumika sana miongoni mwa wanasiasa na katika vyombo vya habari. Hata hivyo, katika kuchunguza kauli hizi, inadhihirika kwamba ziko tofauti. Je, unaweza kufafanua zaidi uwezekano wa maana ya suala hili ili tuweze kuelewa uhalisia wa kisiasa kuhusiana na neno hili, na kutoa baadhi ya mifano kwa ufafanuzi zaidi?

Soma zaidi...

Jibu la Swali: Mazungumzo kati ya Marekani na Iran

Ufalme wa Oman, ambao unaendesha upatanishi katika mazungumzo ya Marekani na Iran, ulitangaza mnamo Alhamisi (kuakhirishwa kwa raundi ya nne ya mazungumzo ambayo yalipangwa kufanyika mnamo Jumamosi katika mji mkuu wa Italia, Roma, "kwa sababu za kiufundi," bila kutaja tarehe mpya. Al-Sharq, 1/5/2025). Mazungumzo ya awali yasiyo ya moja kwa moja kati ya Marekani na Iran yalianza mnamo tarehe 12 Aprili 2025 katika mji mkuu wa Oman, Muscat, kwa upatanishi wa Waziri wa Mambo ya Nje wa Oman, Badr Al-Busaidi.

Soma zaidi...

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu