Jumamosi, 11 Jumada al-awwal 1447 | 2025/11/01
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Kipindi cha “Nampenda Muhammad” nchini India Chafichua Udhalilifu wa BJP Uliofinikwa na Imani ya Wengi

Kipindi cha “Nampenda Muhammad” kilichozuka kote Uttar Pradesh Septemba hii kimefichua tena utata wa kisaikolojia na kisiasa unaoendesha Chama tawala cha Bharatiya Janata (BJP) cha India. Kile kilichoonekana, juujuu, kuwa mzozo wa sheria na utaratibu kuhusu mabango ya kidini na machapisho ya mitandao ya kijamii, kwa kweli, kinaakisi wasiwasi mkubwa zaidi – udhalilifu unaojificha nyuma ya onyesho la imani ya wengi.

Soma zaidi...

Uzbekistan iko katika Hali Tete!

Uchumi wa Uzbekistan uliporomoka baada ya kuvunjika kwa Muungano wa Kisovieti na uhuru wake. Mamilioni ya Wauzbeki waliondoka nchini mwao kutafuta kazi, hasa Urusi, ambapo wakawa wafanyikazi wahamiaji, na wakabaki kwa miaka mingi. Dola hii ilishindwa kuwapa fursa za kazi, au kurekebisha uchumi. Ilishindwa kujenga viwanda na mitambo mipya, na badala yake ikabomoa vile vilivyokuwepo tangu enzi ya Usovieti.

Soma zaidi...

Mambo Muhimu Kuhusu Ziara ya Rais wa Syria, Ahmad al-Shara, jijini Moscow

Rais wa mpito wa Syria, Ahmad al-Sharaa, akifuatana na ujumbe rasmi uliojumuisha waziri wake wa mambo ya nje, Asaad Al-Shaibani, walizuru mji mkuu wa Urusi, Moscow, mnamo 15 Oktoba 2025. Walikutana na Rais wa Urusi Putin katika ziara yao ya kwanza rasmi tangu kuanguka kwa utawala wa Assad, mwishoni mwa mwaka jana.

Soma zaidi...

Matukio ya Kisiasa ya Hivi Majuzi nchini Yemen Yanaonyesha Nini?

Mnamo Alhamisi, 28 Agosti, Waziri Mkuu wa Wizara ya Mabadiliko na Ujenzi, Ahmed Ghaleb Al-Rahwi, aliuawa, pamoja na mawaziri wengine tisa: Waziri wa Sheria na Haki za Binadamu Mujahid Ahmed Abdullah Ali; Waziri wa Uchumi, Viwanda na Uwekezaji Moeen Hashim Ahmed Al-Mahaqri; Waziri wa Kilimo, Uvuvi na Rasilimali za Maji Radwan Ali Ali Al-Rubai; Waziri wa Mambo ya Nje na Wageni Jamal Ahmed Ali Amer; Waziri wa Umeme, Nishati na Maji Ali Seif Mohammed Hassan; Waziri wa Utamaduni na Utalii Ali Qasim Hussein Al-Yafei; Waziri wa Masuala ya Jamii na Leba Samir Mohammed Ahmed Bajaala; Waziri wa Habari Hashim Ahmed Abdul Rahman Sharaf Al-Din; na Waziri wa Vijana na Michezo Mohammed Ali Ahmed Al-Mawlid. Mawaziri wengine kadhaa bado wako katika hali mbaya na ya wastani, akiwemo Jalal Al-Ruwaishan, Naibu Waziri Mkuu wa Masuala ya Ulinzi na Usalama. Umbile la Kiyahudi limeeleza kuwa lilifanya shambulizi hilo, likiwalenga Waziri wa Ulinzi Mohammed Al-Atifi na Mkuu wa Majeshi Mohammed Abdul Karim Al-Ghamari.

Soma zaidi...

Ghasia za Indonesia: Mabadiliko Ambayo (Bado) Yamefungwa?

Msiba wa Affan Kurniawan, dereva wa teksi ya pikipiki wa mtandaoni wa Indonesia aliyeuawa baada ya kugongwa na gari la polisi aina ya barracuda mnamo 28 Agosti 2025, uliishia katika msururu wa maandamano katika miji mingi kote Indonesia. Makala haya hayakusudii kujibu maswali, bali kuibua maswali kwa yeyote anayedai kuwa mwanaharakati wa Kiislamu.

Soma zaidi...

Wanachama wa Hizb ut Tahrir huko Abbasiya Watangaza: Tibueni Mpango wa Amerika wa Kutenganisha Darfur

Kama sehemu ya kampeni iliyoandaliwa na Hizb ut Tahrir/Wilayah Sudan kutibua mpango wa kuichana Sudan kwa kutenganisha eneo la Darfur, na kwa kuzingatia kwamba umoja wa Ummah ni suala nyeti, ambalo ni lazima hatua za uhai au kifo zichukuliwe, Mashababu (wanachama) wa Hizb ut Tahrir walifanya mkutano mnamo Ijumaa, 6 Rabi’ al-Awwal 1447 H, sawia 29 Agosti 2025 M, baada ya swala ya Ijumaa, katika Msikiti wa Sheikh Yahya wa Kuhifadhi Qur'an. Walitoa wito wa dhati kwa Waislamu wa makundi yote, wakiwemo wanasiasa, wanahabari, maulamaa, maafisa na wanajeshi, na wengineo, wakiwataka watimize wajibu wao wa Shariah wa kuzuia kujitenga kwa Darfur.

Soma zaidi...

Upenyaji wa Mayahudi wa Jeshi la Misri

Tangu serikali ya Misri itie saini Makubaliano ya Camp David mwaka 1979, jeshi la Misri limeingia katika njia ya utegemezi na upenywaji, likijitenga na kanuni yake ya awali ya kuulinda Ummah na kulinda mipaka yake dhidi ya maadui wake wa kweli, wa kwanza miongoni mwao ni Mayahudi walioinyakua Palestina. Hatua kwa hatua, taasisi hii imebadilika na kuwa chombo kilichozuiliwa, chini ya masharti ya adui, hata kushiriki katika kuilinda na kuiwezesha kupitia mikataba ya kijeshi, usalama, kiuchumi, na ushauri ambayo iliunda utaratibu kamili wa ushawishi wa Kiyahudi, ndani ya jeshi na dola.

Soma zaidi...

Tofauti Kubwa Kati ya Azimio la Istanbul na Fatwa Zilizotangulia!

Mwishoni mwa kongamano lao waliloliita “Gaza ni Jukumu la Kiislamu na la Kibinadamu” lililofanyika jijini Istanbul kwa siku sita la maulamaa, lililoandaliwa na Erdogan, walitoa tamko la mwisho. Walianza na aya za Qur’an kuhusu maandalizi na Jihad katika Njia ya Mwenyezi Mungu (swt), ili kwamba yeyote anayeisoma afikirie kwamba kitakachofuata kingekuwa ni programu ya kivitendo ya jinsi ya kujishughulisha mara moja na Jihad ambayo sio tu inaiondolea Gaza bali pia inaikomboa Palestina na al-Masjid al-Aqsa. Hata hivyo, uhalisia ulikuwa kinyume.

Soma zaidi...

Utegemezi wa Dola za Kikoloni za Kikafiri Humpora Mtu Utashi wa Kisiasa, Hupotosha Dira ya Mtu na Kupoteza Nguvu za Mtu

Kwa kuzingatia ukandamizaji unaoendelea Syria kwa matakwa ya Amerika na mfumo wa kimataifa, watu wanahisi wameporwa utashi wao, kukosa uwezo wa kufanya maamuzi yao wenyewe, na kuhofia mustakabali wao. Ili kuelewa ni nani anayeamua mambo nchini Syria na kwa nini tumepoteza uwezo wetu wa kufanya maamuzi, lazima tuhakiki mkondo wa mapinduzi ya Syria tangu mwanzo wake.

Soma zaidi...

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu