Jumanne, 29 1448 | 2026/06/16
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Mwaliko wa Kuhudhuria na Kushiriki katika Kikao cha Kadhia za Umma

Tunafuraha, kama Hizb ut Tahrir / Wilayah Sudan, kuwaalika wanahabari, wanasiasa, na wote walio na hamu na masuala ya umma kuhudhuria na kushiriki katika Kikao cha kila mwezi cha Kadhia za Umma, ambacho mwezi huu kitafanyika katika afisi ya Hizb jijini Khartoum baada ya kukatizwa kwa muda mrefu kwa zaidi ya miaka mitatu kutokana na vita.

Soma zaidi...

Jibu kwa Mwandishi wa Makala (Usekula na Ugumu wa Historia ya Uislamu Iliyoghushiwa)

Uislamu ni itikadi ya kiroho na kisiasa ambayo ilikuja kushughulikia matatizo ya wanadamu, kwa kutambua kwamba wanadamu wana silika (ghariza) na mahitaji ya kimwili ambayo yanahitaji kushibishwa. Uislamu umebainisha jinsi mahitaji haya yanavyopaswa kukidhiwa bila ya ziada au upungufu, kupitia hukmu kutoka kwa Mwenye hekima, Mjuzi wa yote. Yeye aliyewaumba wanadamu anajua kipi kuna manufaa na kipi kina madhara kwao! Ukosefu wa elimu wa mwandishi juu ya hukmu hizi haumwondolei jukumu; badala yake, unasisitiza kutoujua kwake Uislamu.

Soma zaidi...

Vikosi vya Msaada wa Haraka Vinafanya Mauaji Dhidi ya Watu Wasio na Silaha, na Serikali Haiwezi Kuwalinda!

Mnamo Alhamisi na Ijumaa, Mei 28 na 29, 2026, Vikosi vya Msaada wa Haraka (RSF) vilizindua mashambulizi kwenye vijiji vilivyo magharibi mwa mji wa Bara katika Jimbo la Kordofan Kaskazini, na kusababisha vifo vya raia kadhaa wasio na silaha. Mtandao wa Madaktari wa Sudan ulithibitisha katika taarifa mnamo Ijumaa, Mei 29, 2026, kwamba RSF ilifanya mauaji makubwa katika mji wa Al-Marra na vijiji vinavyozunguka, na kuwaua raia 27. Katika ripoti yake ya hivi karibuni mnamo Jumamosi, Mei 30, 2026, Al-Arabiya TV ilisema: “Idadi ya vifo kutokana na mauaji ya Vikosi vya Msaada wa Haraka katika eneo la Al-Marra huko Kordofan Kaskazini imeongezeka hadi 58.” Wakati Vikosi vya Msaada wa Haraka vinafanya mauaji haya katika vijiji vya Kordofan, serikali inalaani tu na kuhesabu waliokufa, bila kuchukua hatua zozote kali kuzuia mauaji haya kutokea.

Soma zaidi...

Salamu za Idd al-Adha Iliyobarikiwa

Tunafurahi, katika Hizb ut Tahrir / Wilayah ya Sudan, kuupongeza Ummah mzima wa Kiislamu, na haswa watu wa Sudan, kwa kuwasili kwa Idd al-Adha iliyobarikiwa, tukimwomba Mwenyezi Mungu, Mtukufu, Mwenye Nguvu Zote, kuirudisha tena huku Ummah ukiwa umeungana chini ya umbo lake linalounganisha; Khilafah Rashida kwa njia ya Utume, na umeachwa huru kutokana na minyororo ya utumwa kwa wakoloni makafiri wa Magharibi, ukiwa umebeba bendera ya mabadiliko, ili wanadamu waweze kujitolea katika ibada kwa Mola Mlezi wa walimwengu.

Soma zaidi...

Ujumbe kutoka Hizb ut Tahrir / Wilayah ya Sudan Ulikutana na Kiongozi (Amir) wa Makabila ya Hausa Mjini Port Sudan

Mnamo Alhamisi, 21/5/ 2026, ujumbe kutoka Hizb ut Tahrir/ Wilayah ya Sudan, ukiongozwa na Mkuu wa Kamati Kuu ya Mawasiliano ya Hizb ut Tahrir/ Wilayah ya Sudan, Ustadh Nasser Ridha, akifuatana na Ustadh Abdullah Ismail, Mratibu wa Kamati ya Mawasiliano, walikutana na Amiri wa makabila ya Hausa katika Wilayah ya Port Sudan, Ustadh Salih Abdul Rahman, nyumbani kwake.

Soma zaidi...

Mwaliko wa Kuhudhuria Kikao cha Kisiasa

Afisi ya Habari ya Hizb ut Tahrir katika Wilayah Sudan ina furaha kuwaalika wanahabari, wanasiasa, na wote walio nah amu na masuala ya umma kuhudhuria kikao kipya cha kisiasa, kinachomkaribisha Ustadh Ibrahim Mushrif, mwanachama wa Afisi ya Habari ya Hizb ut Tahrir katika Wilayah Sudan, chenye kichwa: “Dori Iliyopewa Nchi Jirani katika Vita vya Sudan”

Soma zaidi...

Mapendekezo ya Kongamano Lililofanywa na Hizb ut Tahrir / Wilayah ya Sudan Kukumbuka 105 Hijri Tangu Kuvunjwa kwa Khilafah

Mnamo Jumamosi, tarehe 28 Rajab 1447 H, sambamba na tarehe 17 Januari 2026 M, Hizb ut Tahrir / Wilayah ya Sudan ilifanya kongamano la kumbukumbu ya miaka 105 tangu kuvunjwa kwa dola ya Kiislamu ya Khilafah. Kongamano hilo lilihudhuriwa na watu mashuhuri, wakiwemo wanasiasa, watu mashuhuri wa vyombo vya habari, wasomi, na viongozi wa jamii. Kwa kuzingatia kwamba kumbukumbu hii chungu inakuja huku sisi nchini Sudan tukiteseka kutokana na vita vilivyowashwa na ubeberu wa Marekani, ikiwatumia vibaraka wake wa ndani kusambaratisha kile kilichobaki cha umoja wa nchi yetu chini ya sera yake inayoitwa “Mipaka ya Damu”. Hivyo, kichwa cha kongamano letu kilikuwa: “Sudan Kati ya Sera za Mipaka ya Damu na Kuunganisha Watu Kuwa Umma Mmoja.”

Soma zaidi...

Vyombo vya Usalama jijini Umdurman Vyalikamata Kundi la Wanachama wa Hizb ut Tahrir

Kufuatia utekelezaji wa mashababu wa Hizb ut Tahrir katika Wilayah Sudan wa visimamo vitatu katika maeneo tofauti tofauti katika jiji la Omdurman, asubuhi ya Jumatano iliyopita, 25 Rajab 1447 H, sambamba na 14/1/2026 M, ndani ya muundo wa kukumbusha tukio la kupita kwa miaka 105 tangu kuvunjwa kwa Dola ya Khilafah mwezi Rajab 1342 H, vyombo vya usalama viliendelea kuwakamata wanachama watano wa Hizb: Al-Radi Muhammad Ibrahim, Fadlallah Ali Suleiman, Omar Al-Bashir, Hassan Fadl, na Mujahid Adam. Kisha waliachiliwa baada ya Magharibi siku ya Jumatano baada ya nambari zao za simu kuchukuliwa na baada ya kunyakua mabango ambayo Mashababu hao wa Hizb ut Tahrir walikuwa wamebeba katika visimamo hivyo vitatu. Kisha waliitwa mnamo alasiri ya Alhamisi, 15/1/2026, na wangali wako kizuizini hadi wakati wa kuandika taarifa hii!!

Soma zaidi...

Hizb ut Tahrir / Wilayah Sudan Ilifanya Kisimamo na Hotuba ya Hadhara huko Nile Mashariki jijini Khartoum

Mashababu wa Hizb ut Tahrir / Wilayah Sudan huko Nile Mashariki jijini Khartoum walifanya, mnamo Jumamosi, 10/01/2026, kisimamo na hotuba ya hadhara ya kisiasa huko Souq Sitta. Hotuba hiyo ilitolewa na Ustadh Hammad Al-Dayi, mwanachama wa Hizb, ambapo alielezea ubora wa Ummah huu, ambao ulitimiza wajibu wake katika kuwaongoza wanadamu chini ya Dola ya Khilafah, hadi ilipovunjwa na mkoloni kafiri mnamo Rajab 1342 H. Aliukumbusha Ummah kuhusu tukio hili uchungu, na jinsi, kwa kuvunjwa Khilafah, ulivyompoteza Imam ambaye ni ngao, umoja wake na kuchanika vipande vipande, na mkoloni kafiri akapata udhibiti juu yake ili kugawanya ardhi zake.

Soma zaidi...

Mwaliko wa Kuhudhuria Kongamano kwa Mnasaba wa Kumbukumbu ya Kuvunjwa Khilafah katika Hoteli ya Al-Busayri Plaza

Kwa mnasaba wa tukio la kupita miaka 105 ya hijriya tangu kuvunjwa kwa Dola ya Waislamu, Khilafah mnamo 28 Rajab 1342 H, na kama mwendelezo wa kuwakumbusha Waislamu faradhi ya kufanya kazi ya kuiregesha kama Dola ya Khilafah Rashida kwa njia ya Utume, Hizb ut Tahrir / Wilayah Sudan yatoa heshima kukualikeni kuhudhuria kongamano lenye kichwa: “Sudan Kati ya Sera ya Mipaka ya Damu na Sera ya Kuwaunda Watu Kuwa Ummah Mmoja”

Soma zaidi...

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu