Moto Mijini: Jinsi Ubepari Unavyowasha Moto katika Miji ya Waislamu yenye Wakaazi Wengi
- Imepeperushwa katika Kitengo cha Wanawake Afisi Kuu ya Habari
- Kuwa wa kwanza kutoa maoni!
- |
Mnamo Jumatatu, tarehe 1 Juni 2026, vyombo vya habari viliripoti kuhusu moto mkubwa ulioharibu eneo la makaazi lenye watu wengi huko Kebon Kosong, Kemayoran, Jakarta ya Kati, Indonesia. Takwimu rasmi kutoka kwa Wakala wa Kupunguza Maafa wa DKI Jakarta (BPBD) na uthibitishaji wa uwanjani zinaonyesha takriban familia 354—takriban watu 620—waliachwa bila makao. Takriban watoto 160 wenye umri wa kwenda shule waliathiriwa moja kwa moja.



