Jumanne, 09 Ramadan 1445 | 2024/03/19
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Mateso ya Wanawake wa Gaza Waliodhulumiwa, je wana Mlipizaji Kisasi? na je Umma wa Kiislamu Umepoteza Mu’tasem wake?!

Ripoti ya Umoja wa Mataifa ilifichua mnamo Jumatatu kwamba idadi kadhaa ya wanawake na wasichana katika Ukanda wa Gaza wamebakwa na jeshi la Kiyahudi linalokalia kwa mabavu. Kamishna Mkuu wa Haki za Binadamu wa Umoja wa Mataifa amesema leo kuwa wataalamu wake wana wasiwasi kuhusu ripoti zinazoonyesha kuwa wanawake na wasichana wa Kipalestina wanaoshikiliwa mateka wamekuwa wakifanyiwa vitendo mbalimbali vya unyanyasaji wa kingono.

Soma zaidi...

“Je, Palestina Tutaikomboa Vipi?” Kongamano la Kimataifa la Wanawake Mtandaoni juu ya Palestina Lililoandaliwa na Kitengo cha Wanawake katika Afisi Kuu ya Habari ya Hizb ut Tahrir kwa Ushirikiano na Wanawake wa Hizb ut Tahrir Ulimwenguni

Huku mauaji ya halaiki na mzingiro wa kikatili juu ya Gaza yakiendelea, na ugaidi, kukamatwa kwa watu wengi na mauaji ya Wapalestina katika Ukingo wa Magharibi yakipamba moto mikononi mwa umbile katili uaji la Kizayuni, miito imepazwa kote ulimwenguni, kutoka kwa Waislamu na vilevile wasiokuwa Waislamu, ya ‘Ukombozi wa Palestina’.

Soma zaidi...

Kampeni ya Kimataifa na Siku ya Kimataifa ya Wanawake Kuchukua Hatua kwa ajili ya Palestina Kuyaita Majeshi ya Waislamu Kuwaokoa Wanawake na Watoto wa Gaza na Kuikomboa Ardhi Yote ya Al Aqsa

Huku ulipuaji mabomu wa kikatili wa Gaza ukiendelea na umbile uaji la 'Kizayuni', ni wanawake na watoto ndio wanaohimili makali ya mauaji haya ya halaiki, wakijumuisha 70% ya wale waliouawa. Mvua ya mabomu kwenye majengo ya makaazi, maeneo ya hifadhi, shule, hospitali na vitongoji yamesababisha Gaza kuwa makaburi kwa wanawake na watoto, huku watoto zaidi ya 4500 na wanawake 3000 wakiuawa tangu Oktoba 7.

Soma zaidi...

Watu wetu mjini Gaza Wanaangamizwa Huku Watawala Wasaliti Wanatazama Hivi Wako Wapi Watu wenye Ikhlasi katika Ummah wa Uislamu?

Mnamo siku ya 35 ya vita vyake dhidi ya Ukanda wa Gaza, umbile la Kiyahudi lilivisukuma vikosi vyake pamoja na vifaru vyake karibu na eneo la Uwanja wa Hospitali katikati mwa mji wa Gaza, ambalo linajumuisha hospitali 4, Al-Rantisi, Al-Nasr, Al-Ayoun, na hospitali ya afya ya akili. Vikosi vyake vilizingira maeneo yake huku kukiwa na mzoroto mkubwa katika sekta ya afya, haswa kufuatia mzingiro mkali uliuweka kwenye Ukanda wote wa Gaza tangu Oktoba 7.

Soma zaidi...

Sudan Inavuja Damu na Inalilia Msaada... Je, Kuna Mwokozi kwa Watoto na Wanawake?

Mnamo tarehe 15/4/2023, mapigano yalizuka jijini Khartoum kati ya jeshi na Vikosi vya Msaada wa Haraka. RT mtandaoni ilinukuu yafuatayo kutoka kwa AFP: "Mapigano yanaendelea kati ya jeshi na Vikosi vya Msaada wa Haraka huko Khartoum, wakati ambapo shirika moja la misaada lilionya juu ya mlipuko wa ukambi na utapiamlo miongoni mwa watoto katika kambi za waliohamishwa, na unyanyasaji wa kijinsia kwa wanawake.''

Soma zaidi...

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu