Jumatano, 04 Rajab 1447 | 2025/12/24
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Kuvunjwa Moyo Kupya: Watu wa Gaza Wanakufa kwa Baridi Baada ya Kuachwa Kuteswa na Mauaji ya Halaiki kwa Miaka Miwili!

Maafa yanayoikumba Palestina inayokaliwa kwa mabavu yanaendelea bila kukoma. Tangu kuanguka kwa Khilafah, ambayo mtawala wake aliwahi kutamka, “Palestina ni ardhi iliyonyweshwa kwa damu ya mababu zangu, na iwapo Khilafah itaanguka, mtaichukua bila malipo,” uvamizi wa Waingereza (ulioitwa Mamlaka) uliibadilisha. Na hadi leo, umbile la Kiyahudi linaloikalia kwa mabavu, lililoundwa na Uingereza na kuungwa mkono na nchi za Magharibi kwa mali yake yote, vifaa, ujuzi na uwezo wake wote, linaendelea kuwaua watu wa ardhi iliyobarikiwa, likiwafanyia ukatili vijana na wazee, na kuwatishia wafungwa kuwaua na kuwanyonga, huku ulimwengu ukitazama. Limeizingira Gaza kwa miaka mingi, likiishambulia bila kuchoka kwa ukatili usiofikirika, na kusababisha mauaji ya zaidi ya watu elfu sabiini. Na ulimwengu wa Kiislamu, pamoja na majeshi yake na wanazuoni, hutazama na kuona kama vipofu wanavyofanya, na husikia vilio vya wanawake waliofiwa kama viziwi wanavyosikia!

Soma zaidi...

Kilio cha Haraka cha Msaada, Enyi Ummah wa Kiislamu!

Wanawake na watoto wa Gaza wanalilia msaada... wanawake na watoto wa Sudan wanalalamika... wanawake na watoto wa Uyghur huko Turkestan Mashariki wanateseka na kupiga kelele... Wanawake wa Kiislamu na watoto wao kila mahali wanapaza kilio baada ya kilio, wakiita: Je, kuna mtu yeyote wa kusaidia? Je, kuna mtu yeyote wa kuitikia wito? Je, kuna mtu yeyote wa kujibu?!

Soma zaidi...

Enyi Waislamu: Waokoeni watu wa Gaza Kabla Hawajaangamizwa Kabisa na Jihadharini Isije Akakushukieni Ghadhabu na Adhabu ya Mwenyezi Mungu

Umbile la Kiyahudi linaendelea na vita vyake vya mauaji ya halaiki katika Ukanda wa Gaza, likilenga maeneo mbalimbali ya Ukanda huo kwa mashambulizi ya anga na mizinga mikubwa, na kusababisha makumi ya vifo na majeruhi kila siku. Kwa wiki kadhaa, limezidisha mashambulizi yake katika mji wa Gaza, eneo lenye wakaazi wengi na watu waliokimbia makaazi yao kutoka sehemu ya kaskazini ya Ukanda huo, kwa ajili ya maandalizi ya kukaliwa tena kimabavu. Linalenga shule na makaazi, linatekeleza operesheni kubwa za ubomoaji inayolenga nyumba zote za makaazi, na kuvunja magorofa ya makaazi, likiambatanisha na maonyo kuhamia sehemu ya kusini ya Ukanda huo.

Soma zaidi...

Wahanga wa Vita Wanaoteseka Zaidi ni Watoto wa Gaza wenye Ulemavu

Vita vya maafa dhidi ya Gaza, vilivyoanza mnamo Oktoba 7, 2023, vimeathiri kila nyanja ya maisha huko: watu, miti, mawe, na rasilimali, hasa wanawake na watoto. Vifo na uharibifu vimeenea kila mahali. Kulingana na Wizara ya Afya mjini Gaza, vimesababisha vifo vya zaidi ya watu 63,000, kujeruhiwa kwa wengine 160,000, na mamia ya maelfu ya watu kuyahama makaazi yao, huku kukiwa na janga kubwa la kibinadamu linalojumuisha uhaba wa chakula, dawa, na maji safi ya kunywa.

Soma zaidi...

Kitengo cha Wanawake katika Afisi Kuu ya Habari ya Hizb ut Tahrir Chazindua Kampeni ya Kimataifa “Vita vya Sudan: Hadithi ya Ukoloni, Usaliti na Udanganyifu”

Mgogoro wa kikatili nchini Sudan kati ya Wanajeshi wa Sudan (SAF) wanaoongozwa na mtawala mkuu wa Sudan, Jenerali Abdel Fattah al-Burhan, na Kikosi cha Msaada wa Haraka (RSF) kinachoongozwa na Mohamed Hamdan Dagalo (Hemedti), ambaye hapo awali alikuwa naibu wa al-Burhan katika Baraza Kuu, sasa umeingia mwaka wake wa tatu, na kusababisha vifo vya maelfu ya raia. Baadhi ya makadirio yanaweka idadi ya waliofariki katika vita hivi vya kipumbavu kufikia 150,000, huku kukiwa na ukatili wa kutisha uliofanywa na pande zote mbili, ikiwa ni pamoja na mauaji ya kinyama, mateso, ubakaji mkubwa na uhalifu mwingine wa kingono dhidi ya wanawake na wasichana. Mauaji ya kikabila pia yameripotiwa, huku jamii nzima zikiteketezwa kwa moto na kuangamizwa, na mauaji ya halaiki katika miji mbalimbali, vijiji na kambi za watu waliokimbia makaazi yao.

Soma zaidi...

Watoto Wanakufa kwa Njaa... Huku Watawala Wakiendelea na Uzembe wao!

Mkurugenzi Mkuu wa Wizara ya Afya ya Palestina mjini Gaza, Dkt. Munir Al-Barsh, alifichua kuongezeka kwa idadi ya watoto wanaokufa kwa njaa, na kuthibitisha kwamba uvamizi "unafurahi kuwaua," huku kukiwa na mzingiro unaoendelea, kufungwa kwa vivuko, na kupuuza mfumo wa kimataifa. Katika mahojiano katika Chaneli ya Al Jazeera, Al-Barsh alisema kuwa idadi ya watoto waliouawa shahidi kutokana na utapiamlo uliokithiri imefikia 66 hadi sasa, kati yao wa hivi punde ni mtoto mchanga wa miezi mitatu Jouri Al-Masri, akibainisha kuwa makundi yaliyo hatarini zaidi, hasa miongoni mwao ni watoto, wamekuwa wahanga wakuu.

Soma zaidi...

Enyi Waislamu! Msidharau Matendo Yenu Wenyewe kwa Kuangalia Matendo ya Watu! Kwa sababu Nyinyi Ni “Mashahidi” Juu ya Wanadamu!

Meli ya misaada ya "kwenda Gaza" ya Madleen na matendo ya wanaharakati wake maarufu wasio Waislamu yamekuwa na athari kubwa kwenye vyombo vya habari vya kawaida na mitandao ya kijamii. Nchi nyingi, ikiwemo Uturuki, zilitoa "msaada wa ushauri" kwa raia wao wenyewe kwenye meli hiyo, ambayo ilikamatwa na umbile vamizi la kigaidi la kizayuni.

Soma zaidi...

Umbile la Kiyahudi Linatekeleza Mauaji ya Halaiki na Unyanyasaji wa Kijinsia mjini Gaza. Je, Kuna Njia ya Kuamsha Uzembe Huu?

Tangu kutekelezwa Operesheni ya Kimbunga cha Al-Aqsa mnamo 7 Oktoba 2023, umbile la Kiyahudi limewatenga watu walio na msimamo thabiti wa Gaza na kumwaga chuki yake juu yao. Limefanya mauaji ya mfululizo ambayo yamesababisha makumi ya maelfu kuuawa shahidi, huku Umma wa Kiislamu ukiwa bado umefungwa pingu na majeshi yake yamenyamaza kimya kama watu wa makaburini! Lilianza tena mauaji yake baada ya kukiuka usitishaji vita, kwa uungaji mkono wa wazi wa Magharibi na ushirikiano wa wazi na wa aibu wa tawala angamivu katika nchi za Waislamu.

Soma zaidi...

Leo Gaza na Yemen, na Kesho nchi zengine za Waislamu, Isipokuwa Majeshi yao Yatangaze Kusonga

Kamandi Kuu ya Ulinzi ya Marekani (CENTCOM) ilitangaza kwamba jioni ya Jumamosi, 15 Machi 2025, ilianzisha msururu wa mashambulizi ya anga dhidi ya maeneo lengwa ya Mahouthi nchini Yemen. Ilidai kuwa ilifanya mashambulizi sahihi dhidi ya maeneo lengwa ya kundi hilo kote Yemen, ikihalalisha mashambulizi hayo kama utetezi wa maslahi ya Marekani, kuzuia dhidi ya maadui, na kuregesha uhuru wa bahari, kulingana na taarifa yake. Kufikia Alhamisi jioni, Machi 20, makumi ya mashambulizi ya anga ya Marekani dhidi ya Yemen yalikuwa yameripotiwa, na kusababisha vifo vya watu 53 na wengine zaidi ya 100 kujeruhiwa, wengi wao wakiwa wanawake na watoto. Kuna matarajio kwamba operesheni zitaendelea kwa wiki kadhaa. Haya ni mashambulizi ya kwanza dhidi ya Yemen tangu makubaliano ya kusitisha mapigano kati ya umbile la Kiyahudi na Hamas mjini Gaza Januari iliyopita, kufuatia kiapo cha Trump cha "kuwamaliza kabisa."

Soma zaidi...

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu