Jumanne, 14 Dhu al-Hijjah 1446 | 2025/06/10
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Hizb ut Tahrir / Wilayah Sudan Yahuisha Ibada ya Takbira Katika Mwezi wa Dhul-Hijjah kwa Matembezi ya Kishindo katika Soko Kuu la Port Sudan

Baada ya swala ya Alasiri mnamo siku ya Jumatatu, tarehe 6 Dhul-Hijjah 1446 H, sawia na tarehe 2 Juni 2025 M, Mashababu wa Hizb ut Tahrir / Wilayah Sudan walihuisha ibada ya takbira katika mwezi wa Dhul-Hijjah. Ustadh Muhammad Jami’ (Abu Ayman), Msaidizi wa Msemaji wa Hizb ut Tahrir katika Wilayah ya Sudan, alihutubia waumini katika Msikiti wa Ibn Mas’ud katika soko kuu la Port Sudan baada ya Swalah ya Alasiri, akiwakumbusha juu ya ubora wa siku hizi zilizobarikiwa za Dhul-Hijjah, na jinsi Maswahaba – Mwenyezi Mungu awe radhi nao – walivyozitukuza siku hizi kwa takbira na tahleel. Kisha akaanza kupiga takbira, ikifuatiwa na dua. Baadaye wote wakatoka kwa matembezi ya kishindo wakiwa wamebeba Rayah (bendera) ya Mtume wa Mwenyezi Mungu (saw), na alama kubwa isemayo: "Kuhuisha Ibada ya Takbira katika Mwezi wa Dhul-Hijjah."

Soma zaidi...

Hotuba Inayohusu Bendera za Rayah na Liwaa za Mtume (saw) Ilipambwa kwa Takbira na Machozi katika Soko Kuu la Port Sudan

Hizb ut Tahrir / Wilayah Sudan ilitoa hotuba yake ya kisiasa ya kila wiki, iliyokuwa na kichwa: “Je, Mtume (saw) alikuwa na bendera na Rayah?”, mnamo Jumatatu tarehe 28 Jumada al-Akhirah 1446 H sawia na 30/12/2024 M. Ustadh Muhammad Jami’ (Abu Ayman), Msaidizi wa Msemaji Rasmi wa Hizb ut Tahrir katika Wilayah ya Sudan, alizungumza akisisitiza kuwa bendera ya Liwaa na Rayah katika Uislamu ni suala la dini, itikadi, mfumo na nembo ya Uislamu. Mtume (saw), ana benera (Liwaa) nyeupe kama bendera ya amiri jeshi, na bendera (Rayah) nyeusi kwa makamanda wa majeshi na vikosi, na inaitwa Uqab, zimeandikwa juu yazo “La Ilaha illa Allah Muhammad Rasulullah”.

Soma zaidi...

Mkutano wa Waandishi Habari juu ya Sarafu na Mshtuko wa Nixon

Kabla ya kuanzishwa kwa sarafu, watu walitumia ubadilishanaji wa bidhaa kwa huduma. Kwa kuwa dhahabu na fedha zimezingatiwa kuwa madini ya thamani yenye kima cha asili kwa binadamu tangu nyakati za zamani, zilitabanniwa kama pesa, huku sarafu zikichongwa kwazo ili kurahisisha ubadilishanaji. Dhahabu, hasa, inajulikana kwa kuhimili kwake kuharibika kwa muda mrefu.

Soma zaidi...

Hotuba ya Kisiasa mjini Port Sudan Haki ya Kisheria ya Waislamu katika Dhahabu, Petroli, na Rasilimali Nyenginezo

Hizb ut Tahrir / Wilayah Sudan ilitoa hotuba ya kisiasa mbele ya Klabu ya Al-Shabiba katika Soko Kuu la Port Sudan, mnamo siku ya Jumatatu tarehe 7 Jumada al-Akhirah 1446 H, sawia na 9/12/2024 M, yenye kichwa: “Haki ya Kisheia ya Waislamu katika dhahabu, petroli na rasilimali nyenginezo”, ambapo Ustadh Ahmed Abkar, wakili, mjumbe wa baraza la Hizb ut Tahrir / Wilayah Sudan alizungumza, ambapo ilifafanua mali ya umma kuwa ni vitu vilivyoainishwa na sheria kwa ajili ya jamii, vinavyoshirikiwa kati yao, na kukatazwa kumilikiwa na mtu binafsi peke yake.

Soma zaidi...

Hizb ut Tahrir / Wilayah Sudan Ripoti ya Jukwaa la Masuala ya Ummah la Kila Mwezi: Wingi wa Majeshi na Wanamgambo ni Ishara ya Kuangamia kwa Dola, kwa hivyo ni ipi Njia ya Kutokea?

Afisi ya Habari ya Hizb ut Tahrir/Wilayah ya Sudan ilifanya Jukwaa la Kila Mwezi la Masuala ya Ummah, mnamo siku ya Jumamosi, tarehe 5 Jumada Al-Akhir 1446 H sawia na tarehe 7 Disemba 2024 M lenye kichwa: “Wingi wa Majeshi na Wanamgambo ni Ishara ya Kuangamia kwa Dola, kwa hivyo ni ipi Njia ya Kutokea?”

Soma zaidi...

Waziri wa Masuala ya Kidini na Wakfu awa Mgeni wa Hizb ut Tahrir

Ujumbe kutoka Hizb ut Tahrir/Wilayah Sudan ukiongozwa na Ustadh Nasser Ridha (Abu Ridha), Mkuu wa Kamati Kuu ya Mawasiliano ya Hizb ut Tahrir katika Wilaya ya Sudan, na pamoja naye Ustadh Ibrahim Othman (Abu Khalil), Msemaji Rasmi wa Hizb utTahrir katika Wilayah ya Sudan, na msaidizi wake, Ustadh Muhammad Jameh (Abu Ayman) ulimpokea Ndugu Dkt. Omar Bakhit Muhammad Adam, Waziri wa Masuala ya Kidini na Wakfu wa Kifederali katika afisi ya Hizb mjini Port Sudan, jana, Jumamosi, 21 Jumada al-Awwal 1446 H sawia na 23/11/2024 M.

Soma zaidi...

Hizb ut Tahrir / Wilayah Sudan: Mkutano na Waandishi wa Habari “Makubaliano ya Entebbe, Bwawa la Al-Nahdha, na Kupuuza kwa Watawala Maslahi Muhimu ya Umma”

Hizb ut-Tahrir / Wilayah Sudan ilifanya mkutano na waandishi wa habari mnamo siku ya Jumamosi tarehe 23 Rabi’ al-Akhir 1446 H sawia na 10/26/2024 M katika afisi yake mjini Port Sudan, wenye kichwa: “Mkataba wa Entebbe, Bwawa la Al-Nahdha, na watawala kupuuza maslahi muhimu ya Umma”.

Soma zaidi...

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu