Trump na Putin: Kutoka Mapenzi hadi Chuki ni Hatua Moja tu
- Imepeperushwa katika Habari na Maoni
- Kuwa wa kwanza kutoa maoni!
- |
Putin amemtishia Trump kwa “kuvunja mahusiano” endapo Ukraine itapokea makombora ya Tomahawk kutoka Marekani. (nv.ua)
Putin amemtishia Trump kwa “kuvunja mahusiano” endapo Ukraine itapokea makombora ya Tomahawk kutoka Marekani. (nv.ua)
Rais wa Marekani Donald Trump alitangaza kuwa Waziri Mkuu wa “Israel” Benjamin Netanyahu amekubali mpango wenye vipengee 20 ambao ungemaliza vita katika Ukanda wa Gaza. Trump na Netanyahu walifanya mkutano wa pamoja na waandishi wa habari baada ya mkutano wao jijini Washington. Trump alisema kuwa amani ya Gaza ilikuwa karibu sana kupatikana na kumshukuru Netanyahu kwa kuidhinisha mpango huo (DW Turkish 29.09.2025).
Rais Recep Tayyip Erdoğan, katika hotuba yake kwa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa, alielezea kile kinachotokea Gaza kama “mauaji ya halaiki,” alisisitiza kuwa Israel inaua watoto kila siku, na kutoa wito kwa jumuiya ya kimataifa kuchukua hatua. Akisambaza picha kutoka Gaza, Rais Erdoğan alisema: “Hakuna vita mjini Gaza ... Huu ni uvamizi, uhamishaji, ufukuzaji, mauaji ya halaiki na uharibifu wa maisha.”
Katika Mkutano wa Kilele wa Jumuiya ya Ushirikiano wa Kiislamu (OIC) na Ligi ya Nchi za Kiarabu uliofanyika jijini Doha, mji mkuu wa Qatar, Rais Erdoğan alisema: “Tunafahamu kuwa Israel haitasimama katika muda mfupi isipokuwa itakabiliwa na hisia kali na vikwazo. Tunafahamu kwamba tunazo mbinu za kuzuia hili.” (Agencies 15.09.2025)
Kufuatia shambulizi la kombora la umbile la Kizayuni dhidi ya wanachama wa Hamas nchini Qatar, taarifa ya mwisho ya mkutano wa dharura wa kilele wa Waarabu-Waislamu (OIC na Ligi ya Waarabu) uliofanyika jijini Doha mnamo 15 Septemba 2025, “unashutumu vikali uvamizi wa Israel dhidi ya Qatar, na kuutaja kuwa ni kama pigo kwa matarajio yoyote ya amani katika eneo hilo. Tangazo hilo zilizisihi nchi wanachama kuzingatia upya mafungamano yao ya kidiplomasia na kiuchumi na Israel na kufuata hatua za kisheria dhidi yake.”
Takriban watu 24, wakiwemo watoto, wameuawa katika milipuko katika eneo la kijijini la Khyber Pakhtunkhwa kaskazini magharibi mwa Pakistan, na kusababisha wito wa uchunguzi wa tukio hilo. Hakuna taarifa rasmi iliyotolewa kuhusu mauaji ya raia hao wakiwemo wanawake na watoto. (aljazeera.com)
Kwa mara nyengine tena, Amerika inafichua kiburi chake mbele ya ulimwengu. Onyo la Donald Trump kwamba “mambo mabaya yatatokea” isipokuwa Afghanistan ikabidhi Kambi ya Anga ya Bagram inaakisi sauti ile ile ya kibeberu ambayo kwa muda mrefu imekuwa ikifafanua sera ya Marekani kwa ardhi za Waislamu. Maneno kama haya sio lugha ya dola huru zinazoamiliana kwa usawa, bali ni maagizo ya mkoloni ambaye anaziona ardhi za Waislamu kama kituo cha kijeshi kwa ajili ya matamanio yake. Hii ndiyo hali halisi ya siasa za Magharibi: ushurutishaji, vitisho, na kudharau ubwana wa nchi zetu.
Mnamo Septemba 2025, “Israel” ilishambulia Doha, na kuua viongozi wa Hamas na mlinzi wa Qatar. Gazeti la ‘The Independent’ liliripoti kuwa Trump alikasirika kwa sababu Netanyahu alimfahamisha katika dakika za mwisho tu – “He's f***ing me” – huku vyanzo vya “Israel” badala yake vilizungumza kuhusu “idhini” ya Trump.
Pakistan na Saudi Arabia zimeingia katika makubaliano ya kihistoria ya ulinzi wa pande zote, ambapo uvamizi wowote dhidi ya dola moja utachukuliwa kuwa shambulizi kwa pande zote mbili. ‘Mkataba wa Kimkakati wa Ulinzi wa Pamoja’ ulitiwa saini na Waziri Mkuu wa Pakistan Shehbaz Sharif na Mfalme Mtarajiwa wa Saudia Mohammad Bin Salman katika Kasri la Al-Yamamah jijini Riyadh mnamo Jumatano, 17 Septemba 2025.
Indonesia inafikiria kujadili upya deni la mradi wa reli ya mwendo kasi wa Jakarta–Bandung, unaojulikana kama Whoosh, kutokana na mzigo mzito wa kifedha unaouweka kwa mwendeshaji wa reli ya serikali Kereta Api Indonesia (KAI). Waziri wa Biashara Zinazomilikiwa na Serikali Erick Thohir alisema mpango huo utaruhusu KAI kusimamia treni huku serikali ikisimamia miundombinu. Mradi huo wenye thamani ya dolari bilioni 7.3 ulifadhiliwa hasa kupitia mikopo kutoka Benki ya Maendeleo ya China, awali kwa riba ya asilimia 2. Hata hivyo, kukatizwa na maambukizi na masuala ya ardhi yalisukuma gharama zaidi, na kuhitaji ufadhili wa ziada kwa riba ya asilimia 3.4.