Sera ya Elimu Baina ya Kufeli kwa Dola ya Kisasa na Ruwaza ya Khilafah Rashida
- Imepeperushwa katika Tunisia
- Kuwa wa kwanza kutoa maoni!
- |
Sera ya elimu nchini Tunisia, kama moja ya nguzo za dola ya kisasa, imefeli, na mageuzi yanayorudiwa rudiwa hayajafanikiwa. Watoto wetu wamekuwa chini kabisa katika orodha ya kimataifa, na shule na vyuo vikuu vyetu viko nje ya uainishwaji, huku makumi ya maelfu ya wanafunzi wakiacha shule kila mwaka na kutupwa mitaani, ili kumezwa na ukosefu wa ajira, dawa za kulevya, mashua za vifo, na vikundi vya uhalifu, hadi kila mtu atakaposhuhudia ufisadi wa mtaala wa elimu na kufeli kwa matokeo yake, bila kusahau kutengwa kwa walimu na kuwaacha chini kabisa katika ngazi ya mshahara.



