Jarida la Al-Waie: Vichwa Vikuu vya Habari vya Toleo (470)
- Imepeperushwa katika Jarida la Al-Waie
- Kuwa wa kwanza kutoa maoni!
Mwenyezi Mungu (swt) hakumuumba mwanadamu bila ya kuweka mbele yake mitihani kulingana na ukubwa wa Imani yake na kujitolea kwake katika Dini, ili Mwenyezi Mungu (swt) apate kujua ni nani atakayekuwa na subira mbele ya mitihani hiyo na kuweka tegemeo lake (tawakkul) kwa Mwenyezi Mungu (swt) . Haya ni ili Mwenyezi Mungu (swt) amuepushe na fitna. Ama wale ambao watafeli ndani ya mitihani hiyo, watafeli tu kwa sababu ya hukumu yao mbaya, kughafilika kwao na Amri za Mwenyezi Mungu (swt), na Imani yao dhaifu.
Katika kundi la majina yenye kung'aa ya maswahaba watukufu, jina la Mus’ab bin Umair (ra) linajitokeza kama ishara ya muhanga na uthabiti. Mus’ab alikuwa mshika mwenge wa Da’wah katika hatua zake zote, kwani alikuwa ni kijana miongoni mwa vijana bora wa Makka, aliyejulikana kwa uzuri wake, harufu ya kupendeza, na maisha ya anasa, kiasi kwamba Maswahaba, Mwenyezi Mungu (swt) awawie radhi wote, wakasema juu yake, ما رأينا بمكة أحدا انعم عيشا من مصعب بن عمير “Hatujamuona mtu yeyote mjini Makka ambaye aliishi kwa neema kuliko Mus’ab bin Umair.”
Maelezo yanayohusiana na ramani hayaishii tu katika kujua eneo la nchi ambayo tukio mahususi linalochunguzwa linahusiana. Badala yake, inapanuka hadi kuelewa eneo la nchi kwenye ramani, asili ya jiografia inayohusiana na nchi, asili ya mipaka yake, mafungamano yake na bahari, mafungamano yake na vipengee muhimu vya kijiografia, na kufahamu hali ya ya watu kulingana na idadi ya watu, msongamano wa watu, asili na sifa za idadi ya watu, na umiliki wake wa nishati na teknolojia.
Abu Ubaidah Aamir bin Abdullah bin Al-Jarrah Al-Fihri Al-Qurashi (40 Kabla ya Hijra/584 M hadi 18 Baada ya Hijrah/639 M) alikuwa Swahaba (ra) wa Mtume (saw), kamanda wa Kiislamu, na mmoja wa Maswahaba kumi (ra) waliopewa bishara njema ya Pepo. Alikuwa miongoni mwa watu wa kwanza kusilimu.