Jumatano, 14 Muharram 1447 | 2025/07/09
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Hizb ut Tahrir / Wilayah Bangladesh Iliandaa Maandamano na Matembezi ya kupinga Uhamishaji wa India wa Waislamu hadi Bangladesh kwa Mtutu wa Bunduki

Hizb ut Tahrir / Wilayah Bangladesh, iliandaa maandamano na matembezi leo (Ijumaa, 4 Julai 2025) baada ya swala ya Ijumaa katika misikiti mbalimbali ya Dhaka na Chittagong kupinga uhamishaji unaoendelea wa India wa Waislamu hadi Bangladesh kwa mtutu wa bunduki. Wanachama mbalimbali wa Hizb ut Tahrir walitoa hotuba katika maandamano hayo ambayo yalimalizika sambamba na matembezi.

Soma zaidi...

Uhamishaji wa Dola ya Hindutva ya India wa Waislamu hadi Bangladesh kwa Mtutu wa Bunduki ni Uadui wa Wazi kwa Waislamu kama ule wa Umbile Haramu la Kiyahudi

Serikali ya Hindutva ya Modi inaendelea kuongeza kiwango cha ukandamizaji na mateso, ikiwa ni pamoja na kubomoa nyumba za Waislamu wa India na kuwapeleka uhamisho kwa nguvu usio wa haki. Kupitia hili kimsingi wanafuata nyayo za dola haramu ya Kiyahudi ‘Israel’. Hivi karibuni, hata wanawatendea Waislamu wa India kama wanyama kwa kuwaita wahamiaji haramu na kuwarudisha mamia yao nchini Bangladesh kwa mtutu wa bunduki, wakipuuza kile kinachoitwa michakato yao ya kisheria ya kitaifa na kimataifa. "Walitutendea kama wanyama," alisema mwanamke mmoja anayeitwa Rahima Khatun. "Tulipinga kwamba sisi ni Wahindi, kwa nini tuingie Bangladesh? Lakini walituelekezea bunduki na kutishia, 'Ikiwa hamtakwenda kwa huko, tutakupigeni risasi.' Baada ya kusikia milio minne ya risasi kutoka upande wa India, tuliogopa sana na haraka tukavuka mpaka kwa miguu". [Ripoti ya FP].

Soma zaidi...

Ni kutokana na Usaliti wa Watawala Vibaraka wa Ulimwengu wa Kiislamu ambapo Wakatili Wawili wa Amerika - Umbile la Kiyahudi katika Ardhi za Kiarabu na India ya Hindutva huko Asia Kusini - wanaonyesha Kusubutu kwao Kukiuka Ubwana wa Ardhi za Kiislamu

Hizb ut Tahrir / Wilayah Bangladesh, leo (Juni 20, 2025) Ijumaa baada ya swala ya Ijumaa, iliandaa maandamano katika misikiti mbalimbali ya Dhaka na Chittagong kupinga kuendelea kwa mauaji ya halaiki huko Gaza ikiwa ni pamoja na kuzuiliwa kwa chakula na shambulizi dhidi ya Iran na umbile nyakuzi la kiyahudi.

Soma zaidi...

Mkataba wa Yunus-Tarique wa London ni Jaribio la Kudumisha Utawala wa Marekani na Mfumo wao Kandamizi wa Kisekula wa Kibepari

Mnmo tarehe 13 Juni 2025, mkuu wa serikali ya mpito Dkt. Yunus, akiwa amkeketi jijini London, amewakatisha tamaa wananchi kwa kufanya maridhiano ya kisiasa na Tarique Rahman, kaimu mwenyekiti wa BNP (Bangladesh Nationalist Party) kwa sababu watu wa nchi hii hawajasahau historia ya utawala mbaya na ufisadi wa matabaka tawala ya BNP. Kwa hakika, maridhiano haya ya kisiasa ya Yunus-Tarique na kugawanya madaraka ni sehemu ya mpango wa Marekani, ambao kupitia kwao wataweza kutekeleza miradi ya kikoloni. Mumeshuhudia kwamba waliokuwa mabalozi wa Marekani Dan Mozena, Bernicat na Peter Hass, wote wamekaribisha maridhiano haya na kuonesha kuridhika, na kwa mujibu wa taarifa za habari, BNP pia imependekeza kumfanya Dkt. Yunus kuwa rais. Kupitia kuanguka kwa dhalimu Hasina, watu wa nchi hii walionyesha nia yao ya kutaka kuwa huru kutokana na mfumo dhalimu wa kibepari na kutawaliwa na Wakoloni makafiri wa Magharibi. Aina hii ya maridhiano si lolote bali ni usaliti kwa watu wa nchi hii.

Soma zaidi...

Serikali ya Muda Inatengwa na Wananchi kwa sababu ya Utiifu wao kwa Amerika; kwa upande mwingine, Msimamo wa Jeshi letu katika Kupendelea Ubwana wa Nchi kwenye Masuala ya 'Mkondo' na 'Bandari' ni Dhihirisho la Matarajio ya Watu

Huku serikali ya mpito, ikiwapuuza Waislamu wa Rohingya na ubwana wa nchi hiyo, inatamani sana kupeana 'mkondo' kwa maslahi ya kisiasa ya kijiografia ya Amerika na kukabidhi shughuli za 'New Mooring Container Terminal' kwa kampuni yenye ushawishi wa Marekani "DP World", msimamo mkali wa jeshi letu kuunga mkono ubwana wa nchi umesifiwa na watu wengi.

Soma zaidi...

Maandamano ya Kulaani yaliyoandaliwa na Hizb ut Tahrir, Wilayah Bangladesh: “Palestina, Kashmir, Arakan – Khilafah pekee ndiyo Suluhisho”

Hizb ut Tahrir / Wilayah Bangladesh, leo (23/05/2025) baada ya swala ya Ijumua, iliandaa maandamano ya kulaani katika misikiti mbalimbali ya Dhaka na Chittagong dhidi ya wimbi jipya la mashambulizi ya umbile lililolaaniwa la Kiyahudi kuchukua udhibiti wa Ukanda wote wa Gaza.

Soma zaidi...

Mwisho wa Enzi ya Awami League, Chama Kinara cha Siasa za Kisekula - ni Onyo la Kihistoria kwa Vyama Vilivyopo vya Kisiasa na Nyuso Mpya za Kisiasa

Kwa kuanguka kwa dhalimu Hasina na tangazo rasmi la kupigwa marufuku kwa shughuli zote za chama kiovu cha Awami League, enzi ya giza ya siasa za chama kikuu cha kisekula -Awami League imekamilika. Kuangamia huku kwa Awami League, mrithi wa 'All India Muslim League' iliyoanzishwa mwaka wa 1906, hakutokani na mlingano wa kisiasa wa mamlaka ya kundi lolote la kisiasa, bali ni ukweli wa kihistoria na usioepukika. Hamu ya Waislamu wa India ni kuishi chini ya utawala wa Kiislamu-Khilafah.

Soma zaidi...

Kukabidhi Uendeshaji wa Operesheni za "Bohari la Kontena la New Mooring " kwa Kampuni ya Wakoloni yenye Ushawishi wa Marekani "DP World" kutatishia Ubwana wa Nchi

Bila kujali ubwana wa nchi, serikali ya mpito inaendelea na mchakato wa kukabidhi huduma na mabohari mbalimbali ya Bandari ya Chittagong muhimu kimkakati na kiuchumi kwa wageni kwa jina la kuongeza uwezo wa bandari kwa kisingizio cha uwekezaji wa moja kwa moja wa kigeni (FDI). Kama sehemu ya hili, mchakato wa kukabidhi Bohari Kuu la Kontena la New Mooring (NCT) la Bandari ya Chittagong linalojitosheleza na la juu zaidi la kuzalisha mapato kwa kampuni ya DP World uko katika hatua zake za mwisho (Daily Jugantor, Mei 6, 2025).

Soma zaidi...

Wakati wa Ziara yake nchini India, Tulsi Gabbard katika Taarifa yake Alieleza Kujitolea kwa Ushirikiano wa Marekani na India na Mapambano dhidi ya Uislamu na Waislamu

Ingawa maoni ya chuki yaliyotolewa na Mkuu wa Ujasusi wa Kitaifa wa Kruseda Amerika, Tulsi Gabbard wakati wa ziara yake nchini India juu ya mateso ya watu walio wachache nchini Bangladesh na 'Khilafah ya Kiislamu' hayakuwashtua watu wanaozingatia siasa na wapenda Uislamu wa nchi hii, yaliondoa aibu ya mwisho ya vibaraka wa Amerika nchini Bangladesh. Kwa sababu vibaraka hawa walikuuza kukubalika kusiko epukika kwa Amerika kama rafiki wa Bangladesh ili kukabiliana na India na kuwahakikishia watu wapenda Uislamu wa nchi hii kwamba Amerika ilikuwa imeacha sera ya "vita dhidi ya Uislamu". Ingawa ukweli ni kwamba, hata kama uongozi wa Amerika utabadilika, 'sera yao ya kigeni' haibadilika. Badala yake, Trump shupavu au utawala wake hupenda kuwatusi vibaraka wake na kufichua nia za ‘sera zao za kigeni’. Kwa hili ametaka uwajibikaji wa dolari milioni 29 ambazo zililipwa kwa vibaraka ili kubadilisha mazingira ya kisiasa ya Bangladesh, huku kutumia pesa kama hizo kudhibiti siasa za nchi huru ni uhalifu mkubwa na ni sawa na kuingilia masuala ya ndani ya nchi nyingine.

Soma zaidi...

Doria ya Pamoja ya 'CORPAT' na Adui India na Zoezi la Pande Mbili 'Bangosagar' Inathibitisha kuwa Vibaraka wa Marekani-India Wanacheza na Ubwana wa Nchi kwa Maslahi ya Mabwana zao Wakoloni

Moja ya sababu zilizomfanya msaliti Hasina kupinduliwa na watu ni kwamba alitekeleza njama ya India kule Pilkhana na mara kwa mara alifanya majaribio mabaya yote ya kuweka udhibiti wa India juu ya jeshi la nchi hiyo. Wakati ambapo wananchi wanapaza sauti kudai haki kwa mkasa wa Pilkhana, doria ya pamoja 'CORPAT' na zoezi la pande mbili 'Bangosagar' lililofanyika katika Ghuba ya Bengal kwa kushirikisha jeshi la wanamaji la Bangladesh na India imewashtua watu. Kwa kweli, vibaraka wa Marekani-India wamedhamiria kulinda maslahi ya kijiografia ya wakoloni wao hata kwa gharama ya ubwana wa nchi. Inafaa kutaja kwamba wakati matabaka ya kisiasa ya kisekula ya nchi hayakupaza sauti yake dhidi ya njama hiyo ya Pilkhana, ni Hizb ut Tahrir pekee ndiyo iliyofichua njama hiyo mbele ya taifa hilo kwa ushujaa na kupinga njama hiyo dhidi ya ubwana wa nchi hii.

Soma zaidi...

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu