Na Mwenyezi Mungu si mwenye Kughafilika na Wanayoyafanya Madhalimu
- Imepeperushwa katika Kyrgyzstan
- Kuwa wa kwanza kutoa maoni!
- |
Tunaona kwamba vyombo vya usalama vya dola nchini Kyrgyzstan vinawakamata wahalifu ambao wamefanya uhalifu mbalimbali, na baadhi yao walishtakiwa kuwa katika genge la wahalifu, huku wengine wakishtakiwa kwa hongo, mauaji, na mashtaka mfano wa hayo. Ikiwa kweli wanahusika katika uhalifu huo, basi wanachukuliwa pia kuwa wahalifu kwa mujibu wa Shariah ya Kiislamu. Lakini wakati huo huo, tunashuhudia kwamba kuna wafungwa ambao hawakufanya kitendo chochote cha jinai, bali walikamatwa kwa sababu tu ya kulingania dini ya Mwenyezi Mungu na kwa kusema: “Mola wetu ni Mwenyezi Mungu”! Na pia wanakamatwa kikatili mithili ya wahalifu wa kweli na kutupwa magerezani ambako hupigwa sana na mbinu nyingine za "kisasa" za mateso. Hawa ni wanachama wa Hizb ut Tahrir, na madhalimu ni maafisa wa serikali na vyombo vyao vya usalama.