Jumatano, 07 Muharram 1447 | 2025/07/02
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Tanzia ya Mbebaji Ulinganizi: Ustadh Yusuf Dhiab Al-Shalabi (Abu Diya')

Kwa imani kamili juu ya qadhaa ya Mwenyezi Mungu na kutaka malipo kutoka Kwake, Afisi ya Habari ya Hizb ut Tahrir / Wilayah ya Jordan inaomboleza kwa kuondokewa na mmoja wa wabebaji wake wa Da’wah: Ustadh Yusuf Dhiab Al-Shalabi (Abu Diya'), ambaye alifariki dunia kwenda kwenye rehema za Mwenyezi Mungu Mtukufu mnamo Alhamisi, tarehe 1 Muharram 1447 H sawia na 26 Juni 2025 M, akiwa na umri wa miaka 89, baada ya kuugua kwa muda mrefu ambapo alikuwa na subira na kwa kutarajia malipo ya Mwenyezi Mungu.

Soma zaidi...

Jinsi Dola Kubwa Zinavyozaliwa Utotoni mwao

Ni kweli kwamba dola kubwa hazizaliwi ghafla mara moja, lakini hakuna shaka kwamba zinajengwa juu ya itikadi ambayo kwayo mfumo huchipuka. Wakati wa kuzaliwa kwake, fikra yake ilijumuishwa katika kundi ambalo lilijitolea mhanga mali zake za thamani zaidi na kuiunga mkono kivitendo ndani yake. Hili lilizaa dola yake, ambayo ilijizatiti kujitengenezea njia kuelekea uongozi wa kimataifa kwa msingi wa itikadi yake, kufikia haki na rehema kulingana na viwango vya asili ya kimungu katika miongo michache tu. Ni lazima kwa Ummah ambao kwa hakika unataka kurudisha nafasi yake ya hadhi miongoni mwa mataifa, si tu duniani kote, kuregea kubeba ujumbe wake kwa ulimwengu na kulazimisha uongozi wake wa kifikra na utawala wake juu ya fikra za dhulma, ubabe, na utumwa, na kufikia ukombozi wa kifikra na wa kimada. Umma huu lazima uvuke hisia, mambo ya kijuujuu, na lugha ya maneno hadi vitendo.

Soma zaidi...

Serikali ya Hindutva ya India Inaendelea Kutumia Shirika la Kitaifa la Uchunguzi kwa Kazi yake Chafu

Mnamo tarehe 14 Juni 2025, Shirika  la Kitaifa la Uchunguzi (NIA) lilifanya uvamizi ulioratibiwa katika maeneo matatu huko Bhopal, Madhya Pradesh, na miwili huko Jhalawar, Rajasthan, kuhusiana na kesi ya Hizb ut Tahrir (HuT). Operesheni hiyo ililenga kukusanya ushahidi zaidi dhidi ya HuT. NIA ilidai kuwa uvamizi huu ulisababisha kukamatwa kwa "vifaa vya kidijitali na nyenzo za hatia" (vitabu na vifaa vya kuandikia tunavyodhania). Kabla ya uvamizi huu, Jharkhand (jimbo) ATS ilikuwa imewaweka kizuizini watu wawili kuhusiana na kesi ya Hizb ut Tahrir. Serikali ya India ilipiga marufuku kinyume cha sheria Hizb ut Tahrir mnamo tarehe 10 Oktoba 2024, ikitaja juhudi zake za kusimamisha "Khilafah" ya kimataifa kupitia ugaidi na itikadi kali.

Soma zaidi...

Na Mwenyezi Mungu si mwenye Kughafilika na Wanayoyafanya Madhalimu

Tunaona kwamba vyombo vya usalama vya dola nchini Kyrgyzstan vinawakamata wahalifu ambao wamefanya uhalifu mbalimbali, na baadhi yao walishtakiwa kuwa katika genge la wahalifu, huku wengine wakishtakiwa kwa hongo, mauaji, na mashtaka mfano wa hayo. Ikiwa kweli wanahusika katika uhalifu huo, basi wanachukuliwa pia kuwa wahalifu kwa mujibu wa Shariah ya Kiislamu. Lakini wakati huo huo, tunashuhudia kwamba kuna wafungwa ambao hawakufanya kitendo chochote cha jinai, bali walikamatwa kwa sababu tu ya kulingania dini ya Mwenyezi Mungu na kwa kusema: “Mola wetu ni Mwenyezi Mungu”! Na pia wanakamatwa kikatili mithili ya wahalifu wa kweli na kutupwa magerezani ambako hupigwa sana na mbinu nyingine za "kisasa" za mateso. Hawa ni wanachama wa Hizb ut Tahrir, na madhalimu ni maafisa wa serikali na vyombo vyao vya usalama.

Soma zaidi...

Wilayah Tunisia Tanzia ya Mbebaji Ulinganizi: Ndugu Basheer Qassila

Hizb ut Tahrir katika Wilayah ya Tunisia inaomboleza mmoja wa watu wake waliojitolea na wabebaji wa da'wah: mzee na kaka, simba wa da'wah, Basheer Qassila, ambaye alifariki mnamo Jumapili, tarehe 26 Dhul-Hijjah 1446 H, sawia na 22 Juni 2025 M, baada ya kupambana na maradhi yaliyomdhoofisha mwili wake lakini katu hayakuzima moto wa ujumbe wake wala azma yake ya kufanya kazi pamoja na safu akijitahidi kurudisha mfumo kamili wa maisha wa Kiislamu kwa kusimamisha Khilafah Rashida kwa njia ya Utume.

Soma zaidi...

Ni kutokana na Usaliti wa Watawala Vibaraka wa Ulimwengu wa Kiislamu ambapo Wakatili Wawili wa Amerika - Umbile la Kiyahudi katika Ardhi za Kiarabu na India ya Hindutva huko Asia Kusini - wanaonyesha Kusubutu kwao Kukiuka Ubwana wa Ardhi za Kiislamu

Hizb ut Tahrir / Wilayah Bangladesh, leo (Juni 20, 2025) Ijumaa baada ya swala ya Ijumaa, iliandaa maandamano katika misikiti mbalimbali ya Dhaka na Chittagong kupinga kuendelea kwa mauaji ya halaiki huko Gaza ikiwa ni pamoja na kuzuiliwa kwa chakula na shambulizi dhidi ya Iran na umbile nyakuzi la kiyahudi.

Soma zaidi...

“Baada ya Kuibuka kwa (Israel) Tulikabiliana na Ulimwengu wa Kiarabu Ulioungana, na Polepole Tukaugawanya”

Kwa maneno haya, Netanyahu anahutubia watu wake na ulimwengu, akijigamba kana kwamba amefanya hivyo. Kama ilivyo desturi ya watu wake, ni wachongezi, waongo na kudai wasichokuwa nacho! Kabla ya kuwepo kwa umbile la wale ambao Mwenyezi Mungu amewalaani na kabla ya kuvunjwa kwa Khilafah, “Ulimwengu wa Kiarabu” haukuunganishwa tu. Badala yake, ulikuwa ni umma mmoja chini ya dola moja. Umma huu haukugawanywa na nyinyi, bali mabwana zenu waliokubuni kwa uovu na hila. Mabwana wenu waliopigana na umma huu kwa karne nyingi, wakionja nguvu zake na kushuhudia kuanguka kwa miji yao mikuu mmoja baada ya mwingine. Konstantinopoli ilitekwa na dada yake (Roma) karibu kuanguka, lakini Mwenyezi Mungu akataka ibaki kuwa hifadhi kwa ushindi mpya ujao, Inshallah.

Soma zaidi...

Umbile la Kiyahudi ni Panya Anayejifanya Kumiliki Nguvu ya Simba, Ubabe na Ujasiri wake unatokana na Watawala Wasaliti wa Waislamu

Alfajiri ya Ijumaa, 13/6/2025, umbile la Kiyahudi lilifanya mashambulizi ya kushtukiza dhidi ya Iran, yakilenga maeneo ya nyuklia na makao makuu ya kijeshi, na kusababisha vifo vya viongozi kadhaa wa kijeshi na usalama, pamoja na wanasayansi wa nyuklia.

Soma zaidi...

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu