Mamlaka ya Palestina ilimuua Rami Zahran, Kisha Mzee Mmoja, Ikikamilisha Uhalifu wake Dhidi ya Watu wa Palestina
- Imepeperushwa katika Palestina
- Kuwa wa kwanza kutoa maoni!
- |
Mnamo siku ya Jumanne,13/5/2025, vikosi vya usalama vya Mamlaka ya Palestina vilimuua kijana Rami Zahran kutoka kambi ya wakimbizi ya Al-Far'a huko Tubas. Kisha wakafuatilisha hili kwa kumuua mzee mmoja (Abu Khalil al-Saba'neh) kutoka mji wa Jenin. Huu ni mwendelezo wa jinai zake dhidi ya watu wa Palestina, zikiwemo za mauaji, uchomaji moto, ukamataji, uvamizi wa misikiti, na unyang'anyaji mali ya Wapalestina kinyume cha sheria, kula mali zao kwa njia ya dhambi na fujo.