Jumatatu, 09 Rabi' al-awwal 1447 | 2025/09/01
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Ujumbe kutoka Hizb ut Tahrir / Wilayah Sudan Wanamtembelea Mkuu wa Chama cha Democratic Unionist mjini Al-Obeid

Ujumbe kutoka Hizb ut Tahrir / Wilayah ya Sudan, ukiongozwa na Ustadh Al-Nazir Muhammad Hussein - Mjumbe wa Baraza la Hizb ut Tahrir katika Wilayah ya Sudan - akifuatana na Ustadh Issam al-Din Abdul Qadir, walimtembelea Ustadh Khalid Hussein, Mkuu wa Chama cha Democratic Unionist, katika afisi yake katika mji wa Al-Obeid, mnamo Jumanne 3 Rabi’ al-Awwal sawia na tarehe 26 Agosti 2025 M, kama sehemu ya kampeni iliyoandaliwa na Hizb ili kutibua mpango wa kuitenganisha Darfur.

Soma zaidi...

Ujumbe kutoka Hizb ut Tahrir / Wilayah Sudan Waitembelea Idara ya Muongozo na Ushauri katika Jimbo la White Nile

Ujumbe kutoka Hizb ut Tahrir / Wilayah Sudan – Mji wa Rabak, White Nile, uliitembelea Idara ya Muongozo na Ushauri mnamo Jumapili, 1 Rabi' al-Awwal 1447 H sawia na tarehe 24 Agosti 2025. Ujumbe huo ulikutana na mkuu wa Sekretarieti katika Jimbo la White Nile, Sheikh Abdul Mubara Mahmoud Al-Mahmoud. Ujumbe huo uliongozwa na Dkt. Ahmed Muhammad Fadl Al-Sayyid, mwanachama wa Hizb ut Tahrir, na alifuatana na Ustadh Faisal Madani, mwanachama wa Hizb ut Tahrir.

Soma zaidi...

Usaliti Mpya: Mamlaka ya Lebanon Yamwachilia Huru Mmoja wa Wafungwa Wanaohusishwa na umbile la Kiyahudi!

Leo, Alhamisi, tarehe 21/8/2025, mamlaka ya Lebanon ilimwachia huru ghafla Saleh Abu Hussein, ambaye ni mmoja wa washirika wa umbile la Kiyahudi, bila kubadilishana na yeyote! Na wakamkabidhi kwa umbile hilo kililokuwa mstari wa mbele wa ukaliaji kimabavu wa Palestina mjini Naqoura!

Soma zaidi...

Migogoro Inayosababishwa na Utawala Fisadi Haiwezi Kutatuliwa Kupitia Nao

Tangu Marekani ilipoikalia kwa mabavu Iraq mwaka 2003, na kwa miaka 22 sasa, imekuwa ikikumbwa na mzozo wa kifedha na umaskini na uchochole ulioenea. Licha ya mapato ya mafuta yanayofikia mamia ya mabilioni kila mwaka, wanasiasa na wataalamu wake hujitokeza kila mwaka kutoa tahadhari kuhusu mgogoro wa kifedha unaoweza kusababisha serikali kukosa uwezo wa kulipa mishahara ya wafanyikazi.

Soma zaidi...

Je, Mubashir Ahmad Atakuwa Mwathirika Mwengine wa Utawala wa Uzbekistan?

Mnamo Agosti 19 mwaka huu, mashtaka yalianza katika kesi ya jinai dhidi ya Alisher Tursunov, anayejulikana kwa jina lake bandia Mubashir Ahmad. Anatuhumiwa kwa kuchapisha machapisho yanayopigia debe mawazo ya kidini yenye msimamo mkali na ushupavu kupitia vyombo vya habari. Hapo awali alishtakiwa kwa kuandaa, kuhifadhi, au kusambaza nyezo za kidini kinyume cha sheria, na Wizara ya Mambo ya Ndani ilimweka kwenye orodha ya watu wanaotafutwa kimataifa! Uturuki ilimregesha Mubashir Ahmad hadi Uzbekistan kwa ombi lake mwezi Mei mwaka huu.

Soma zaidi...

Mwaliko wa Kuhudhuria Kikao cha Kisiasa

Afisi ya Habari ya Hizb ut Tahrir katika Wilayah Sudan inafuraha kuwaalika ndugu katika vyombo vya habari, wanasiasa, na wale wote wanaopenda masuala ya umma, kuhudhuria na kushiriki katika kikao kipya cha Kisiasa, ambapo Ustadh Hatim Jaafar, mwanasheria - mjumbe wa Baraza la Hizb ut Tahrir katika Wilayah ya Sudan.

Soma zaidi...

Ufuatiliaji Mkubwa wa Mkoloni Amerika juu ya kile kinachoitwa “Mageuzi” sio Chengine ila ni Jaribio la kupanua Udhibiti wake nchini Bangladesh

Balozi Mdogo wa Marekani jijini Dhaka, Tracy Ann Jacobson, alifanya mkutano na Profesa Ali Riaz, Makamu Mwenyekiti wa Tume ya Kitaifa ya Maridhiano wiki iliyopita ili kuuliza kuhusu mipango ya mageuzi inayoendelea na maendeleo yake. Jacobson na manaibu wake wamekuwa wakifanya mfululizo wa mikutano na wawakilishi wa vyama vikuu vya kisiasa. Kama sehemu ya ushirikiano wa Marekani ‘kukuza demokrasia’ nchini Bangladesh, tunaona mikutano na taarifa za mara kwa mara kutoka kwa Ubalozi wa Marekani nchini Bangladesh na Wizara ya Mambo ya Nje ya Marekani zinazohimiza marekebisho katika utawala. Kusiwe na shaka kwamba msukumo wa Marekani wa kuleta mageuzi na kile kinachoitwa ‘uwajibikaji wa kidemokrasia’ haukusudiwi kheri ya watu wetu. Katika historia, mbeberu mamboleo Marekani imekuwa ikiunga mkono madikteta kwa maslahi yake huku ikitetea ‘demokrasia’ na ‘haki za binadamu’.

Soma zaidi...

Ni Wakati sasa wa Kugeuza Ukurasa wa Giza wa Oslo

Smotrich alitangaza kuangamia kwa mradi wa Dola ya Palestina kwa kuzinduliwa kwa mradi wa E1 au East One, ambao unachukuliwa kuwa utekelezaji wa kinachojulikana kama Mpango wa Jerusalem Kuu. Mpango huu unatenganisha Ukingo wa Magharibi wa Kaskazini kutoka Ukingo wa Magharibi wa Kusini, na, sambamba na hatua zilizochukuliwa na umbile la Kiyahudi uwanjani, unaunda viunga vilivyotengwa ndani yake ambavyo vinawazingira watu wa Ukingo wa Magharibi. Hili lilitanguliwa na kubomolewa kwa kambi kaskazini mwa Ukingo wa Magharibi na kuorodheshwa kwa UNRWA kama shirika lisilo halali, ili suala la wakimbizi libaki kuwa lisilo na umuhimu wowote.

Soma zaidi...

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu