Mwaka Mpya wa Hijri Sio Maadhimisho ya Kihistoria, Bali Mwanzo wa Kusimamishwa kwa Dola ya Kiislamu Na Khilafah Rashida ya Pili kwa Njia ya Utume Itarudi Tena
- Imepeperushwa katika Syria
- Kuwa wa kwanza kutoa maoni!
- |
Mwaka Mpya wa Hijri unatujia tarehe 1 Muharram 1448 H, sawia na 16/06/2026 M. Hii ndiyo tarehe iliyochaguliwa na Al-Faruq Umar ibn Al-Khattab na Maswahaba watukufu (ra) kama kalenda ya Waislamu. Alichagua tarehe hii kwa sababu iliashiria kuzaliwa kwa Dola ya kwanza ya Kiislamu iliyosimamishwa na Mtume wetu (saw) mjini Al-Madinah Al-Munawwarah.



