Ijumaa, 08 Jumada al-thani 1447 | 2025/11/28
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Trump Awaongoza Wafuasi wake kutoka kwa Watawala katika Ardhi za Waislamu kwenye Mkataba wa Fedheha na Aibu, Wakiinamisha Vichwa Vyao Nyuma Yake kwa Kuiweka Gaza Hashem chini ya Usimamizi na Ukoloni!

“Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa lilipitisha alfajiri ya Jumanne mpango wa Rais wa Marekani Donald Trump kuhusu Ukanda wa Gaza baada ya kuidhinisha rasimu ya azimio lililowasilishwa na Marekani na kuunga mkono mpango wa amani wa Trump katika sekta hiyo, na Rais Trump aliisifu kura ya Baraza la Usalama kuhusu azimio la Gaza kama wakati wa kihistoria...” (BBC, 18/11/2025). Kuhusu Azimio Nambari 2803, lilichapishwa na vyombo vya habari na lilikuwa ni idhini ya mpango wa pointi 20 wa Rais Donald Trump wa kukomesha mzozo mjini Gaza, lililotolewa mnamo tarehe 29 Septemba 2025.

Soma zaidi...

Jibu la Swali: Ruwaza ya Marekani ya Kutatua Kadhia ya Cyprus

“Afisi ya rais wa Uturuki ilitangaza mnamo Jumatatu kwamba Rais wa Jamhuri ya Uturuki ya Cyprus Kaskazini, Tufan Erhürman, atatembelea Ankara Alhamisi ijayo, 13/11/2025... Burhanettin Duran, mkuu wa idara ya mawasiliano ya rais wa Uturuki, alisema kwamba ziara ya Erhürman Ankara inakuja kutokana na mwaliko wa Rais Erdoğan, na Duran aliongeza kwamba ziara hiyo itakuwa kituo cha kwanza cha kigeni cha Erhurman... Na mnamo tarehe 19 Oktoba Bodi Kuu ya Uchaguzi ya Uturuki ya Cyprus ilitangaza ushindi wa kiongozi wa Chama cha Republican cha Kituruki, Tufan Erhürman, katika uchaguzi wa rais.” (Shirika la Anadolu, 10/11/2025). Kwa hivyo ni nini kimesababisha maridhiano haya? Ikifahamika kwamba Erhurman, wakati wa kampeni yake ya uchaguzi, alikuwa akitoa wito wa kuunganisha kisiwa hicho, huku Erdogan akitoa wito wa dola mbili? Na je, Amerika iko nyuma ya maridhiano hayo? Na Mwenyezi Mungu akulipe kheri.

Soma zaidi...

Jibu la Swali: Sudan Baada ya Vikosi vya Msaada wa Haraka Kuchukua Udhibiti wa El Fasher

“Massad Boulos, mshauri mkuu wa Rais wa Marekani Donald Trump kuhusu masuala ya Mashariki ya Kati, alithibitisha kwamba jeshi la Sudan na Vikosi vya Msaada wa Haraka wamekubaliana kusitisha mapigano kwa miezi mitatu, kulingana na mpango wa Quartet, unaojumuisha Imarati, Marekani, Saudi Arabia, na Misri, uliotangazwa mnamo Septemba 12.” (Sky News Arabia, 3/11/2025).

Soma zaidi...

Hizb ut Tahrir / Indonesia: Matembezi Makubwa ya Kukumbusha Ulimwengu “Palestina ingali chini ya Uvamizi”

Maelfu ya Waislamu katika miji mbalimbali ya Indonesia walifanya matembezi yanayounga mkono Palestina mnamo Oktoba 18 na 19, 2025, chini ya kauli mbiu “Palestinaingali chini ya Uvamizi.” Huko Bandung, zaidi ya waandamanaji 15,000 walikusanyika mbele ya jengo la Gedung Sati, wakinyanyua bendera za Rayah zenye tamko la Tawhid na mabango yenye kauli mbiu kama vile “Tumeni majeshi ya Kiislamu, yakomboe Palestina!”, na “Suluhisho la mwisho kwa Palestina ni kupitia jihad na Khilafah,” na “Palestina itakombolewa kupitia Khilafah na Jihad.”

Soma zaidi...

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu