Jumatano, 17 Dhu al-Hijjah 1447 | 2026/06/03
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Salamu za Idd Idd ni Wakati Ambapo Furaha na Huzuni Zinaunganishwa!

Siku hizi Idd al-Adha inafika, ambapo furaha na huzuni zimechanganyika. Furaha katika mwitikio wa waumini kwa wito wa Mwenyezi Mungu wa Hijja, wakiitikia wito wake katika mkusanyiko unaowaunganisha kutoka pembe zote za dunia, pamoja na makabila na rangi zao mbalimbali, kwa kutii amri ya Mwenyezi Mungu na kupata radhi Zake. Na huzuni kubwa inawakumba nyoyo zao kwa masaibu yao tangu kupoteza nguvu yao na kuvunjwa kwa dola yao mikononi mwa mhalifu Mustafa Kemal. Ni Idd ya aina gani huku Gaza ikiendelea kutokwa na damu?! Idd ya aina gani huku kambi na meli za kivita za maadui wa Umma zikiwa katikati ya ardhi zake?! Idd ya aina gani huku wanawake huru wa Waislamu wakidhalilishwa huko Palestina, Turkestan Mashariki, Myanmar, na India?!

Soma zaidi...

Kama Hujui, Hilo Ni Janga; Lakini Kama Unajua, Basi Janga Ni Kubwa Zaidi!

Wakati wanasiasa wa Iraq na kambi zao wakigombea nyadhifa, matukio yanajitokeza ambayo yanathibitisha tena kwamba nchi hii si tu kwamba haina ubwana, bali pia kwamba maamuzi yake, ardhi, na anga zake vinakiukwa waziwazi na mtu yeyote na kila mtu. Amri za Marekani zinatolewa waziwazi na bila kuficha kuhusu uundaji wa serikali. Uingiliaji kati wa Iran kupitia kamanda wa Kikosi cha Quds cha Iran na ziara zake za mara kwa mara pia ni uko hadharani na haujafichika. Suala jengine lilikuwa ni ufichuzi wa ‘New York Times’ wa kuwepo kwa kambi mbili za kijeshi za umbile la Kiyahudi wakati wa vita vya Marekani dhidi ya Iran: moja katika Jangwa la Al-Nukhaib na nyingine katika jangwa la magharibi.

Soma zaidi...

Udhalimu wa Watawala Wakandamizaji Unaweza Kukomeshwa Tu Kupitia Mabadiliko Msingi

Tangu Jumamosi iliyopita, mkoa wa Erbil umekuwa ukishuhudia mvutano wa kiusalama kufuatia maandamano ya makabila ya Herki katika wilaya ya Khabat, yakikituhumu Chama cha Kidemokrasia kwa kukaidi ahadi zake za kuwapa viti vitatu bungeni kwa badali ya kabila hilo kuwapa kura zao katika uchaguzi. Maandamano hayo kisha yakageuka kuwa mapigano kati ya makabila ya Herki na vikosi vya usalama, na kusababisha vifo na majeraha. Katika tukio muhimu, kabila hilo lilitangaza uhamasishaji wa jumla huko Erbil, na waandamanaji wakachoma makao makuu ya Chama cha Kidemokrasia cha Kurdistan katika wilaya hiyo leo, Jumatatu.

Soma zaidi...

Masanduku ya Kura katika Mfumo Fisadi Ndio Udanganyifu Mkubwa Zaidi kwa Mabadiliko

Tangu Marekani ilipovamia mwaka wa 2003 hadi sasa, Iraq imekuwa ikizama katika matatizo, na hali yake inazidi kuwa mbaya. Yote hayo ni matokeo ya ramani ya kisiasa ambayo mvamizi Marekani aliiunda na kuilazimisha. Ndiyo iliyoweka misingi ya mfumo huo na kuchora ramani ya kisiasa ya nchi hii, ikiudanganya umma wa Iraq kuamini kwamba suluhisho la matatizo yanayozalishswa na mfumo huu ni masanduku ya kura.

Soma zaidi...

Ubwana Uliopotea na Vyama Vikipigania Nyadhifa Huku Uchungaji wa Ummah ukiwa Sio Miongoni mwa Hamu Zao

Katika wakati ambapo vyama tawala vinajiandaa kushindana katika uchaguzi na ngawira zake zilizopangwa kufanyika Novemba 11 mwaka huu, vikosi maalum, vifaru, na magari ya kivita, alfajiri ya Ijumaa, 22/08/2025, vilizingira Hoteli ya Lalezar katikati ya Sulaymaniyah na kuivamia, ili kutekeleza operesheni ya kumkamata mkuu wa Chama cha Jabhat Ash-Sha’ab, Lahur Sheikh Jangi. Baada ya mapigano makali ya silaha yaliyodumu kwa masaa mengi kati ya Vikosi vya Kupambana na Ugaidi na Vikosi Maalum (Commandos) na “Asayish,” vikosi vya usalama vilivyounganishwa na Muungano wa Uzalendo wa Kurdistan upande mmoja, na walinzi wa Sheikh Jangi upande mwengine, yalimalizika kwa kukamatwa kwa Lahur na kaka yake Pulad, na kusababisha vifo na majeraha.

Soma zaidi...

Migogoro Inayosababishwa na Utawala Fisadi Haiwezi Kutatuliwa Kupitia Nao

Tangu Marekani ilipoikalia kwa mabavu Iraq mwaka 2003, na kwa miaka 22 sasa, imekuwa ikikumbwa na mzozo wa kifedha na umaskini na uchochole ulioenea. Licha ya mapato ya mafuta yanayofikia mamia ya mabilioni kila mwaka, wanasiasa na wataalamu wake hujitokeza kila mwaka kutoa tahadhari kuhusu mgogoro wa kifedha unaoweza kusababisha serikali kukosa uwezo wa kulipa mishahara ya wafanyikazi.

Soma zaidi...

Majanga na Maafa ni Matokeo ya Kimaumbile ya Kukosekana Dola yenye Kujali

Katika msururu wa ajali za mara kwa mara na moto wa kutisha-hasa ule moto wa ukumbi wa harusi wa mwaka 2023 huko Ninawi, ambao uligharimu maisha ya zaidi ya watu 120 na kujeruhi 200; moto wa mwaka 2021 katika Hospitali ya Al-Hussein huko Dhi Qar, ambao uliua zaidi ya watu 92; na moto wa mwaka 2021 wa kituo cha utengaji wagonjwa wa COVID-19 katika Hospitali ya Ibn Al-Khatib jijini Baghdad, ambao ulisababisha vifo vya watu 82-unakuja msiba mwengine tena wa kutisha. Moto mkubwa ulizuka katika soko kuu la Kut jioni ya Jumatano, 16 Julai 2025. Wizara ya Mambo ya Ndani ya Iraq ilithibitisha kuwa moto huo, ambao ulizuka ndani ya jengo la biashara la ghorofa tano katikati mwa mji wa Kut, uliwaua watu 61, ikiwa ni pamoja na miili 14 iliyoungua ambayo bado haijatambuliwa. Waathiriwa wengi walikufa kutokana na kuvuta moshi. Wizara hiyo iliongeza kuwa jengo hilo ambalo lilikuwa na mkahawa na kituo cha biashara, lilikuwa limefunguliwa kwa siku saba pekee.

Soma zaidi...

Mfuko wa Fedha wa Kimataifa: Chombo Mikononi mwa Makafari cha Kudhibiti Sera ya Ndani ya Nchi Inayokopa

Mnamo Jumatano, 9/7/2025, Mfuko wa Fedha wa Kimataifa (IMF) ulionya kwamba uchumi wa Iraq unakabiliwa na changamoto kubwa. Bodi ya IMF, katika taarifa yake ya kuhitimisha mashauriano ya Kifungu cha IV na Iraq, ilisema kuna nafasi ya kuimarisha mapato yasiyo ya mafuta kupitia ongezeko la kodi na ushuru wa forodha.

Soma zaidi...

Umbile la Kiyahudi ni Panya Anayejifanya Kumiliki Nguvu ya Simba, Ubabe na Ujasiri wake unatokana na Watawala Wasaliti wa Waislamu

Alfajiri ya Ijumaa, 13/6/2025, umbile la Kiyahudi lilifanya mashambulizi ya kushtukiza dhidi ya Iran, yakilenga maeneo ya nyuklia na makao makuu ya kijeshi, na kusababisha vifo vya viongozi kadhaa wa kijeshi na usalama, pamoja na wanasayansi wa nyuklia.

Soma zaidi...

Pongeza kutoka kwa Hizb ut Tahrir / Wilayah Iraq kwa Sikukuu ya Idd al-Adha 1446 H

Afisi ya Habari ya Hizb ut Tahrir / Wilayah Iraq inatoa pongezi na baraka zake nyingi kwa Umma wa Kiislamu kwa mnasaba wa Idd al-Adha iliyobarikiwa. Hasa tunatoa salamu hizi kwa wabebaji da’wah, na kwa mwanachuoni mkubwa, Amiri wa Hizb utTahrir, Ata Bin Khalil Abu Al-Rashtah Mwenyezi Mungu amlinde na amhifadhi na ampe ushindi na tamkini kupitia mikono yake.

Soma zaidi...

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu