Umaskini Ulioenea na wa Kimuundo Nchini Afghanistan: Matokeo ya Kufeli Kutabikisha Mfumo wa Kiuchumi wa Uislamu—Na Uendelevu wa Fikra ya Kiuchumi ya Enzi ya Jamhuri
- Imepeperushwa katika Afghanistan
- Kuwa wa kwanza kutoa maoni!
- |
Ripoti za hivi karibuni—ikiwa ni pamoja na ripoti ya kushtua ya BBC kutoka mkoa wa Ghor, kujichoma moto kwa mhandisi jijini Kabul, na simulizi zinazorudiwa rudiwa za watu wanaouza figo—zimefichua janga la kibinadamu linaloumiza moyo wa kila Muislamu. Katika baadhi ya miji, foleni ndefu za watu wanaotafuta kazi, njaa, na umaskini zimekuwa uhalisia unaoonekana. Wengine, wakiwa wamekandamizwa na umaskini na madeni, wamelazimika kuwauza binti zao wadogo ili kuokoa maisha ya wanafamilia wengine. Ripoti za UNDP zinaonyesha kwamba watu watatu kati ya kila wanne nchini Afghanistan hawawezi kukidhi mahitaji yao ya msingi ya maisha, na zaidi ya asilimia kumi ya idadi ya watu wako ukingoni mwa njaa.



