Jumapili, 22 Rajab 1447 | 2026/01/11
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Lazima Tuitupilie Mbali Miungu ya Uongo na Miovu ya Utaifa na Ukabila Kwenye Jaa la Historia!

Kutokana na utaifa, ukabila na kuanzishwa kwa dola za kitaifa na mipaka yake katika ardhi za Waislamu, kitambulisho cha Waislamu kimeharibika na kutengana, ambapo Ummah wa Kiislamu hapo awali uliunganishwa katika udugu mmoja na ndani ya Dola moja ya Kiislamu, badala yake ukagawanyika katika dola za kitaifa zaidi ya 50 na vitambulisho vya kitaifa kufuatia kuvunjwa kwa Khilafah mnamo tarehe 28 Rajab, 1342, mikononi mwa Mustafa Kamal, “baba wa udhalifu”.

Soma zaidi...

Dori ya Magharibi Kafiri katika Kuuchana Umma wetu na katika Kuivunja Khilafah yetu, Nembo ya Nguvu Yetu

Tulipokuwa Umma mmoja tofauti na mwingine wowote, dola yetu iliweka Rayah (bendera) yake juu ya maeneo yote; ilikuwa mlinzi, kimbilio, na kizuizi dhidi ya yeyote ambaye angeweza hata kufikiria kumshambulia Muislamu mmoja. Waislamu walikuwa mwili mmoja, wakisaidiana kwa ushindi, msaada, na kuimarishana. Iwapo kiungo kimoja kingelalamika, mwili uliobaki ungejibu kwa kukesha na homa. Kisha maadui walielewa kwamba umoja huu na dola hii ndio sababu ya nguvu ya Umma wa Kiislamu na ngao yake ya kinga. Kwa hivyo walianza kulenga ngao hiyo, wakijaribu kuivua, wakifanya juhudi kubwa kwa miaka mingi mirefu hadi walipofikia lengo lao, kwa masikitiko, na kuivunja Dola ya Khilafah mnamo 1924, wakiuchana Ummah wa Uislamu vipande vipande ili kuizuia kurudi katika hali yake ya zamani.

Soma zaidi...

Rajab na Suala la Umoja wa Waislamu

Kwa Waislamu wengi leo, neno “Khilafah” huhisika kama jambo la mbali. Baadhi hulihusisha na vitabu vya historia, wengine huliona kama jambo la kindoto au lisilo la kawaida. Hili linaeleweka, hasa kwa kizazi ambacho kimewahi kuishi ndani ya mfumo wa kisasa wa dola ya kitaifa. Lakini kila mwaka, mwezi wa Rajab hutukumbusha kimya kimya mabadiliko makubwa katika historia ya Waislamu. Katika Rajab 1924, Khilafah ilifutwa. Huu haukuwa tu mwisho wa serikali, bali kupotea kwa muundo uliopangilia umoja wa Ummah wa Kiislamu kwa zaidi ya karne kumi na tatu.

Soma zaidi...

Tafsiri Al-Baqarah [Muhkam na Mutashabiha]

Jambo muhimu katika sayansi ya Quran linalohusiana na tafsiri ya aya za Mwenyezi Mungu, mbali na maana halisi na ya kimajazi, ni kuwepo kwa yaliyo wazi na yaliyo na utata katika Kitabu. Mwenyezi Mungu (saw) amesema, “Yeye ndiye aliye kuteremshia Kitabu hichi. Ndani yake zimo Aya muhkam, zenye maana wazi. Hizo ndizo msingi wa Kitabu hichi. Na ziko nyengine za mifano. Ama wale ambao nyoyoni mwao umo upotovu wanafuata zile za mifano kwa kutafuta fitna, na kutafuta maana yake; na wala hapana ajuaye maana yake ila Mwenyezi Mungu. Na wale wenye msingi madhubuti katika ilimu husema: Sisi tumeziamini, zote zimetoka kwa Mola wetu Mlezi. Lakini hawakumbuki hayo isipo kuwa wenye akili.” 

Soma zaidi...

Kipindi cha “Nampenda Muhammad” nchini India Chafichua Udhalilifu wa BJP Uliofinikwa na Imani ya Wengi

Kipindi cha “Nampenda Muhammad” kilichozuka kote Uttar Pradesh Septemba hii kimefichua tena utata wa kisaikolojia na kisiasa unaoendesha Chama tawala cha Bharatiya Janata (BJP) cha India. Kile kilichoonekana, juujuu, kuwa mzozo wa sheria na utaratibu kuhusu mabango ya kidini na machapisho ya mitandao ya kijamii, kwa kweli, kinaakisi wasiwasi mkubwa zaidi – udhalilifu unaojificha nyuma ya onyesho la imani ya wengi.

Soma zaidi...

Kuwahamasisha Watu Wenye Azma ya Kutimiza Faradhi Yao ya Shariah

Enyi ndugu na dada: tuna jukumu kubwa. Ni amana ya kueneza ujumbe wa Risaalah, kubeba Uislamu, na kusimamisha Uislamu kama mfumo kamili wa maisha kivitendo. Hili ni jukumu la Mitume (as) na urithi wa Mtume wetu mpendwa Muhammad (saw). Mwenyezi Mungu (swt) atatuuliza kuhusu kile tulichokabidhiwa, kwa hivyo tufanye kazi kwa ajili ya siku ambayo utajiri wala watoto hawatakuwa na faida yoyote, isipokuwa wale wanaomjia Mwenyezi Mungu (swt) kwa moyo safi.

Soma zaidi...

Uzbekistan iko katika Hali Tete!

Uchumi wa Uzbekistan uliporomoka baada ya kuvunjika kwa Muungano wa Kisovieti na uhuru wake. Mamilioni ya Wauzbeki waliondoka nchini mwao kutafuta kazi, hasa Urusi, ambapo wakawa wafanyikazi wahamiaji, na wakabaki kwa miaka mingi. Dola hii ilishindwa kuwapa fursa za kazi, au kurekebisha uchumi. Ilishindwa kujenga viwanda na mitambo mipya, na badala yake ikabomoa vile vilivyokuwepo tangu enzi ya Usovieti.

Soma zaidi...

Mambo Muhimu Kuhusu Ziara ya Rais wa Syria, Ahmad al-Shara, jijini Moscow

Rais wa mpito wa Syria, Ahmad al-Sharaa, akifuatana na ujumbe rasmi uliojumuisha waziri wake wa mambo ya nje, Asaad Al-Shaibani, walizuru mji mkuu wa Urusi, Moscow, mnamo 15 Oktoba 2025. Walikutana na Rais wa Urusi Putin katika ziara yao ya kwanza rasmi tangu kuanguka kwa utawala wa Assad, mwishoni mwa mwaka jana.

Soma zaidi...

Ummah Kati ya Uwepo Tu na Kazi Halisi, Kutokuwepo au Kutoweka? Sababu na Mbinu za Uchangamshaji

Ni muhimu kutofautisha kati ya uwepo wa awali wa jambo na maelezo ya hali yake. Kwa mfano, uwepo wa kimwili wa gari ni wa kudumu, lakini kuharibika au kutotembea kwake kunaelezea hali yake. Vile vile, uwepo wa Ummah wa Kiislamu ni wa kweli na imara, wenye kumiliki vipengee vyake muhimu: Aqidah (itikadi) inayounganisha na mifumo ya maisha inayotokana na aqidah hiyo.

Soma zaidi...

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu