Kuunganisha Fikra na Wabebaji Wake Ndio Njia ya Mabadiliko ya Kweli
- Imepeperushwa katika Uchambuzi
- Kuwa wa kwanza kutoa maoni!
- |
Ni wazi, kwa wale wanaofanya kazi kwa ikhlasi kwa ajili ya kuhuisha Umma wa Kiislamu kupitia Uislamu, kile ambacho hali ya Ummah imefikia, kushambuliwa na mataifa mengine kama mwindaji anapolenga kwenye mawindo yake. Vile vile, ni dhahiri kwa wachunguzi jinsi Ummah unavyoelewa kwa uwazi uhalisia wake na kutambua sababu za mateso na maumivu yake. Kinachojulikana kwa Ummah kwa kiasi kikubwa kimefungika kwa makafiri wakoloni, watawala vibaraka, na tawala zilizowekwa na dola hizi za kikoloni juu ya shingo za Ummah ili kuukandamiza, kupora rasilimali zake, na kuuzuia kujikomboa kutoka kwa mshiko wa wakoloni kwa kusimamisha Khilafah kwa njia ya Utume.