Ijumaa, 19 Ramadan 1445 | 2024/03/29
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Afisi ya Habari
Wilayah Pakistan

H.  25 Muharram 1443 Na: 1443 / 06
M.  Alhamisi, 02 Septemba 2021

 Taarifa kwa Vyombo vya Habari

Kufa Shahidi kwa Syed Ali Gilani Kunahitaji kwamba Takbir ya Ushindi na Bendera ya Kalima Zipazwe katika Kashmir Iliyokaliwa, baada ya Kukombolewa Kwake na Jeshi la Pakistan kwa Jihad Iliyobarikiwa.

(Imetafsiriwa)

Kwa nyoyo nzito, Waislamu nchini Pakistan na Kashmir Iliyokaliwa walisikia habari za kuuawa shahidi kwa Syed Ali Gilani, huko Srinagar, mnamo Jumatano tarehe 1 Septemba 2021, saa 10.30 jioni. Ni cha Mwenyezi Mungu (swt) alichotoa na cha Mwenyezi Mungu (swt) alichochukua, kwa hivyo tunasema tu yale yanayomridhisha Mola wetu Mlezi,

 [إِنَّا للهِ وَإِنَّا إِلَيْهِ رَاجِعُونَ]

“Hakika sisi ni wa Mwenyezi Mungu, na kwake Yeye hakika tutarejea.” [Surah Al-Baqarah 2: 156]. Akikataa kata kata kukaliwa kwa Ardhi ya Waislamu tangu miaka ya sitini ya karne iliyopita, Syed Ali Gilani aliwekwa chini ya kifungo cha nyumbani na vikosi vamizi vya India kwa miaka kumi na moja iliyopita, ambapo ilimwathiri sana afya yake, na kuishia kufa shahidi. Kauli mbiu maarufu 'Hum Pakistani Hain, Pakistan Hamara Ha,' "Sisi ni Wapakistani na Pakistan ni yetu," iliundwa na Syed Ali Gilani, ikitaka ukombozi wa Kashmir Iliyokaliwa na kuunganishwa kwake na Pakistan.

Enyi Waislamu wa Pakistan!

Mwenyezi Mungu (swt) asema,

[مِّنَ الْمُؤْمِنِينَ رِجَالٌ صَدَقُوا مَا عَاهَدُوا اللَّهَ عَلَيْهِ فَمِنْهُم مَّن قَضَى نَحْبَهُ وَمِنْهُم مَّن يَنتَظِرُ وَمَا بَدَّلُوا تَبْدِيلاً]

“Miongoni mwa Waumini wapo watu walio timiza waliyo ahidiana na Mwenyezi Mungu. Baadhi yao wamekwisha kufa, na baadhi wanangojea, wala hawakubadilisha (ahadi) hata kidogo.” [Surah Al-Ahzaab 33: 23]. Tunaomba kwamba Syed Ali Gilani afufuliwe pamoja na Manabii (as), mashahidi na wakweli (siddiqin), kwani hakuna hasara kwa muumini ambaye amekaa sawa juu ya Ukweli. Isitoshe, kufa shahidi kwa Syed Ali Gilani sio kwa ajili ya kuomboleza, na bendera kupeperushwa nusu mlingoti, lakini lazima ichangamshe Takbir za kutangaza Jihad na kunyanyua bendera ya Kalima, kwa vikosi vya wapiganaji vya majeshi yetu. Syed Ali Gilani alikuwa mkweli kwa kile alichomuahidi Mwenyezi Mungu (swt), akitimiza ahadi yake hadi kifo, huku nafasi hiyo nzuri ikiwasubiri wale maafisa katika vikosi vyetu vya jeshi, wanaotii amri ya Mwenyezi (swt) na Mtume wake (saw), kwa kupigana hadi uvamizi wa India umalizwe.

Enyi Waislamu wa Jeshi la Pakistan!

Hakika, kushindwa kwa Amerika na washirika wake wa Magharibi nchini Afghanistan kulikuwa mikononi mwa mujahidina walio na silaha duni, kwa Nasr (ushindi) wa Mwenyezi Mungu (swt), kwa hivyo hakuna kitu cha kukuzuieni msilishinde na kulivunja moyo Jeshi la India lililoparaganyika, kwa Nasr ile ile. Zaidi ya hayo, kiburi cha India ni kivuli tu cha uwepo wa kieneo wa Amerika, ambao umefifia na unaweza kufanywa kutoweka milele, chini ya uongozi mtiifu kwa Mwenyezi Mungu (swt) na Mtume wake (saw). Wang'oeni watawala wa sasa wa Pakistan, ambao kwa khiyana waliisalimisha Kashmir kwa Modi mnamo 5 Agosti 2019, na muipe Nussrah yenu Hizb ut Tahrir ili kusimamisha tena Khilafah kwa Njia ya Utume. Hapo ndipo uwepo wa kieneo wa Amerika utakapotoweshwa milele, kuanzia kwa kufungwa kwa njia zake za usambazaji za hewani na ardhini na vituo vyake vya ujasusi katika misheni zake za kidiplomasia kwenye ardhi yetu. Hapo ndipo mipaka ambayo mkoloni aliyochorwa kwenye ramani ili kutugawanya na kututawala itafutwa, kwani nchi za Waislamu kuunganishwa kitu kimoja, moja baada ya nyengine, chini ya Khalifah mmoja. Hapo ndipo Umma wa Kiislamu utakapounganishwa kama dola yenye nguvu zaidi duniani, na kulazimisha kurudi nyuma kwa wale wote waliotangaza vita vya uvamizi kwa muda mrefu sana, huku wakifungua nchi zao wenyewe kwa ajili ya nuru na rehma ya Uislamu.

#أفغانستان           #Afghanistan              #Afganistan        

Afisi ya Habari ya Hizb ut Tahrir katika Wilayah Pakistan

Hizb-ut Tahrir: Afisi ya Habari
Wilayah Pakistan
Address & Website
Tel: 
https://bit.ly/3hNz70q

Andika maoni

Hakikisha umejaza (*) habari zinazohitajika palipoashiriwa. Kodi za HTML haziruhusiwi.

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu