Ijumaa, 18 Rabi' al-thani 1447 | 2025/10/10
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Afisi ya Habari
Wilayah Sudan

H.  14 Rabi' II 1447 Na: HTS 1447 / 41
M.  Jumatatu, 06 Oktoba 2025

Taarifa kwa Vyombo vya Habari

Hizb ut Tahrir / Wilayah Sudan
Yatoa Hotuba ya Hadhara eneo la Nile Mashariki, Khartoum
(Imetafsiriwa)

Kama sehemu ya kampeni yake ya kutibua mpango wa kuigawanya Sudan kwa kutenganisha Darfur, Hizb ut Tahrir/Wilayah Sudan ilitoa hotuba ya hadhara mnamo Jumamosi, tarehe 4 Oktoba 2025, katika Soko la 6 la Al-Wahda katika mtaa wa Nile Mashariki, Khartoum. Ustadh Omar Hassan, mwanachama wa Hizb ut Tahrir, alizungumzia kuhusu umoja wa Ummah kama suala nyeti. Alianza hotuba yake kwa maneno ya Mwenyezi Mungu (swt):

[وَاعْتَصِمُوا بِحَبْلِ اللهِ جَمِيعاً وَلَا تَفَرَّقُوا]

“Na shikamaneni kwa Kamba ya Mwenyezi Mungu nyote pamoja, wala msifarikiane.” [Aal-i-Imran:103].

Akaeleza maana ya aya hiyo, kisha akasema kwamba Umma wa Kiislamu ulishikamana na kamba ya Mwenyezi Mungu (swt) mpaka akaja mkoloni kafiri, akaivunja Khilafah, akazichana ardhi za Waislamu katika vidola vidogo, anaendelea kupanga njama dhidi ya Ummah na kugawanya kile kilichogawanyika na kutenganisha Sudan Kusini na kutayarisha dola zilizobaki kwa ajili ya kujitenga. Sasa, Amerika inatafuta kutenganisha eneo la Darfur. Alieleza kuwa Muungano wa Uasisi wa Sudan ni hatua moja tu katika njia ya kuisambaratisha nchi kwa kutenganisha Darfur.

Kisha akatoa wito kwa Ummah kubeba jukumu lake, kutimiza wajibu wake, na kujitahidi kwa dhati kuzuia kujitenga kwa Darfur, kama ilivyokuwa kwa Sudan Kusini. Hadhira iliitikia kwa shauku hotuba hiyo.

Ibrahim Othman (Abu Khalil)
Msemaji Rasmi wa Hizb ut Tahrir
katika Wilayah Sudan

Hizb-ut Tahrir: Afisi ya Habari
Wilayah Sudan
Address & Website
Tel: 0912240143- 0912377707
http://www.hizb-sudan.org/
E-Mail: Spokman_sd@dbzmail.com

Andika maoni

Hakikisha umejaza (*) habari zinazohitajika palipoashiriwa. Kodi za HTML haziruhusiwi.

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu