Jumanne, 19 Jumada al-thani 1447 | 2025/12/09
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Afisi ya Habari
Wilayah Sudan

H.  10 Jumada II 1447 Na: HTS 1447 / 61
M.  Jumatatu, 01 Disemba 2025

Taarifa kwa Vyombo vya Habari

Ujumbe kutoka Hizb ut Tahrir / Wilayah Sudan
Wakutana na Mkuu wa Chama cha Wanasheria katika Jimbo la Bahari Nyekundu
(Imetafsiriwa)

Mnamo Jumatatu, 1 Disemba 2025, ujumbe kutoka Hizb ut Tahrir / Wilayah Sudan, ukiongozwa na Ustadh Nasser Ridha, Mwenyekiti wa Kamati Kuu ya Mawasiliano ya Hizb ut Tahrir katika Wilayah Sudan, akifuatana na Ustadh Abdullah Ismail, Mjumbe wa Kamati Kuu ya Mawasiliano ya Hizb ut Tahrir katika Wilayah Sudan, walimtembelea Dkt. Imad al-Din Muhammad Hamdallah, mkuu wa Chama cha Wanasheria katika Jimbo la Bahari Nyekundu, afisini kwake Port Sudan.

Baada ya kutambulishana, mkuu wa ujumbe alielezea kuhusu Hizb ut Tahrir na malengo yake: “Kuregesha maisha kamili ya Kiislamu kupitia kusimamishwa kwa Khilafah Rashida kwa njia ya Utume, ikiliona kama jambo la hatima na faradhi kwa kila Muislamu kufanya kazi kuelekea hilo.” Mwenyekiti alijibu, “Tunawaunga mkono wale wote wanaofanya kazi kwa ajili ya Uislamu,” na akaomba baadhi ya machapisho ya hizb. Ujumbe huo uliahidi kuyatoa na kisha ukampa machapisho yanayohusiana na kampeni ya Hizb ut Tahrir nchini Sudan ya kutibua mpango wa Amerika wa kutenganisha Darfur.

Ujumbe ulimshukuru nahodha kwa mapokezi ya dhati.

Ibrahim Othman (Abu Khalil)
Msemaji Rasmi wa Hizb Ut Tahrir
katika Wilayah Sudan

Hizb-ut Tahrir: Afisi ya Habari
Wilayah Sudan
Address & Website
Tel: 0912240143- 0912377707
http://www.hizb-sudan.org/
E-Mail: Spokman_sd@dbzmail.com

Andika maoni

Hakikisha umejaza (*) habari zinazohitajika palipoashiriwa. Kodi za HTML haziruhusiwi.

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu