- |
- Kuwa wa kwanza kutoa maoni!
- ukubwa wa font punguza ukubwa wa font zidisha ukubwa wa font
بسم الله الرحمن الرحيم
Hizb ut Tahrir / Wilayah Jordan
[وإِنِ اسْتَنصَرُوكُمْ فِي الدِّينِ فَعَلَيْكُمُ النَّصْرُ]
“Lakini wakiomba msaada kwenu katika Dini, basi ni juu yenu kuwasaidia.” [Surah Al-Anfal: 72]
Kwa jina la Mwenyezi Mungu, Mwingi wa Rehema, Mwenye Kurehemu
[يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا لَا تَخُونُوا اللَّهَ وَالرَّسُولَ وَتَخُونُوا أَمَانَاتِكُمْ وَأَنتُمْ تَعْلَمُونَ]
“Enyi mlio amini! Msimfanyie khiana Mwenyezi Mungu na Mtume, wala msikhini amana zenu, nanyi mnajua.” [Surah Al-Anfal: 27]
Hii ni hotuba kutoka kwa Mwenyezi Mungu (swt) kwa Waislamu kuhusiana na faradhi ya Shariah ya kuwanusuru Waislamu walio chini ya mamlaka ya dola za kikafiri na makafiri ambao hawajahamia kwenye Nyumba ya Uislamu (Dar ul Islam), iwe kwa kuwazuia utekelezaji wa ibada zao za kidini au kwa kuwadhulumu.
Basi, vipi kuhusu hukmu ya Shariah kuhusu wale ambao wamechukuliwa mateka, na makafiri wanakalia kimabavu sehemu ya Ardhi ya Uislamu?
Faradhi ya Shariah ya kuwaokoa ni ya lazima na kali zaidi, kama vile faradhi ya Shariah ya kuwasaidia watu wa Palestina kwa kupeleka majeshi.
Iwapo itasemwa, kama wasemavyo wanazuoni waovu wa serikali, kwamba wameweka ahadi na mapatano baina yetu na wao, jibu kwao ni kwamba makubaliano haya ni batili katika Shariah, hayana thamani na uzito wa Shariah, kwa sababu mikataba ya hivi sasa na Mayahudi inatambua ukaliaji wao wa kimabavu ardhi ya Israa na Mi’raj.
Hili limeharamishwa na Shariah, na ni haramu kujifunga na mikataba hii. Hukmu ya Shariah inabakia kuwa wazi na isiyo na shaka, ambayo ni faradhi ya kuyakusanya majeshi.
Imetolewa na Afisi ya Habari ya Hizb ut Tahrir / Wilayah Jordan
Jumatatu, 03 Safar 1447 H - 28 Julai 2025 M