Alhamisi, 18 Ramadan 1445 | 2024/03/28
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

بسم الله الرحمن الرحيم

Hizb ut Tahrir/ Wilayah Pakistan:

Kashmir

Uislamu katu hauruhusu majadiliano ya kukubaliana na makafiri kuhusu maswala ya Ardhi za Waislamu na haki na ulinzi wa Waislamu. Hivi leo majeshi ya India yamegawanyika katika uwanja wa vita kwa mapande mawili; Kaskazini katika mpaka na China na Magharibi katika mpaka na Pakistan. Katika hali ile ile ya kutaka kudhibiti sintofahamu baina ya Pakistan na India, idadi ya vikosi baina ya India na Pakistan kwa sasa ni sawa. Uhuishaji wa makubaliano ya kusitisha vita katika udhibiti huu kwa hali hii ilivyo ni suala linalo ipa India nafasi kidogo ya kupumua. Hivi leo Waislamu na vijana wa Kashmir wamekataa kutwaliwa na India na pia India kukwapua kimabavu eneo la Kashmir. Katu India haiwezi kudumisha ukaliaji wake wa Kashmir bila vitisho na majeshi. Hii ni fursa adhimu kwa Pakistan kuikomboa Kashmir yote kwa kutumia majeshi. Hali ya kijeshi na kiuchumi ya India haiiwezeshi kuhimili shambulizi makini la ghafla la jeshi la Pakistan kwa ajili ya ukombozi wa Kashmir.  Waislamu wa Pakistan wanayataka Majeshi ya Pakistan yasukumwe na ghera ya Dini yao, historia tukufu ya Waislamu, na moyo wa kuwasaidia ndugu zao Waislamu. Yapasa Majeshi haya kukumbuka makamanda wa majeshi ya Khilafah na kuamua kujipanga kwa ajili ya kuikomboa Kashmir kwa kufuata nyayo za Sultan Salahuddin Ayubi na Sultan Muhammad Fateh.

وَمَا لَكُمْ لاَ تُقَاتِلُونَ فِي سَبِيلِ اللَّهِ وَالْمُسْتَضْعَفِينَ مِنْ الرِّجَالِ وَالنِّسَاءِ وَالْوِلْدَانِ الَّذِينَ يَقُولُونَ رَبَّنَا أَخْرِجْنَا مِنْ هَذِهِ الْقَرْيَةِ الظَّالِمِ أَهْلُهَا وَاجْعَل لَنَا مِنْ لَدُنْكَ وَلِيًّا وَاجْعَل لَنَا مِنْ لَدُنْكَ نَصِيرًا (النساء: 75(

"Na mna nini msipigane katika Njia ya Mwenyezi Mungu na ya wale wanaoonewa, wanaume na wanawake na watoto, ambao husema: Mola Mlezi wetu! Tutoe katika mji huu ambao watu wake ni madhalimu, na tujaalie tuwe na mlinzi anaye toka kwako, na tujaalie tuwe na wakutunusuru anaye toka kwako." [An-nisaa 4:75]

Jumamosi, Ramadhan Mubarak 19, 1442 H – 01 Mei, 2021 M

#Time4Khilafah

 

Andika maoni

Hakikisha umejaza (*) habari zinazohitajika palipoashiriwa. Kodi za HTML haziruhusiwi.

rudi juu

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu