- |
- Kuwa wa kwanza kutoa maoni!
- ukubwa wa font punguza ukubwa wa font zidisha ukubwa wa font
بسم الله الرحمن الرحيم
Hizb ut Tahrir / Wilayah Sudan:
Amali na Shughuli Wakati wa Mwezi wa Julai 2026 M
Hizb ut Tahrir/Wilayah Sudan iliimarisha shughuli zake za umma wakati wa mwezi Julai 2026, ikihimiza jamii ya Waislamu kufanya kazi nayo ili kuanzisha jengo kubwa la Uislamu: Khilafah Rashida kwa njia ya Utume. Shughuli maarufu zaidi za Hizb ut Tahrir katika Wilayah Sudan zilikuwa kama ifuatavyo:
1) Ujumbe kutoka Hizb ut Tahrir/Sudan:
Watu Mashuhuri wa Kabila la Amarar huko Sudan Mashariki Ulioandaliwa na Hizb ut Tahrir
Mnamo Julai 1, 2026, Hizb ut Tahrir ilipokea ujumbe wa watu mashuhuri kutoka kabila la Amarar katika afisi yake mjini Port Sudan. Walikutana na Ustadh Nasser Ridha, Mkuu wa Kamati Kuu ya Mawasiliano, akifuatana na msemaji rasmi, Ustadh Abu Khalil. Mkuu wa Kamati Kuu ya Mawasiliano aliwasilisha mtazamo wa hizb kuhusu matukio ya sasa, akielezea kwamba masuluhisho lazima yapatikane kutoka kwa Uislamu. Mazungumzo ya kina kisha yalifanyika na ujumbe uliokuwa umetembelea kuhusu masuala muhimu yanayowakabili Waislamu. Kwa kumalizia, pande zote mbili zilikubaliana kudumisha mawasiliano na mashauriano kuhusu masuala yanayohusu jamii ya Waislamu.
Kukutana na Mkuu wa Chama cha Wanasheria cha Sudan na Viongozi wake
Mnamo siku ya Alhamisi, Julai 9, 2026, ujumbe ulioongozwa na Ustadh Nasser Ridha ulitembelea afisi ya Chama cha Wanasheria wa Sudan huko Port Sudan, ambapo walikutana na Mkuu wa Chama cha Wanasheria na wanachama wa afisi yake. Ujumbe huo uliwasilisha mukhtasari wa Hizb ut Tahrir na lengo lake kwa jamii ya Waislamu: kusimamishwa kwa Khilafah Rashida ya pili kwa njia ya Utume. Walisisitiza kwamba kufanya kazi kutekeleza sheria ya Kiislamu na kuanzisha mamlaka juu ya msingi wa Uislamu ni faradhi kwa Waislamu wote, wakiunga mkono hoja yao kwa dalili za kisheria. Kila mwanachama wa ujumbe wa Chama cha Wanasheria kisha akazungumza, na Mkuu wa Chama cha Wanasheria akahitimisha mkutano kwa kuushukuru ujumbe huo kwa ziara yao na kwa hamu wa Hizb ut Tahrir kwa masuala yanayoikabili jamii ya Waislamu. Alisema kwamba hakukuwa na kutokubaliana na Hizb ut Tahrir kuhusu suala la Khilafah, ambalo ndilo lengo kuu la kila Muislamu, na akathibitisha umuhimu wa mawasiliano endelevu.
2) Shughuli za Msemaji Rasmi wa Hizb ut Tahrir katika Wilayah ya Sudan:
Waraka wenye sumu wa Paul Mwenye Sumu wa Paul na Dori ya Marekani ya Kutiliwa Shaka nchini Sudan
Afisi ya Habari ilifanya mkutano na waandishi wa habari mjini Port Sudan mnamo siku ya Jumamosi, tarehe 4 Safar 1448 H (Julai 18, 2026 M), ikimkaribisha msemaji rasmi, Ustadh Ibrahim Othman Abu Khalil, ambaye alizungumzia kuhusu uhalisia wa mipango ya sumu ya Marekani, ikiwa ni pamoja na waraka wa hivi karibuni wa Massad Paul. Alisema kwamba uwezo mkubwa wa kijeshi, kisiasa, na kiuchumi wa Amerika umeiwezesha kufuata sera ya utawala juu ya nchi zote, kuunda migogoro, kuanzisha matatizo, na kusababisha mivutano, kisha kusimamia migogoro hii na kutafuta suluhu. Hivi ndivyo hasa Amerika inavyofanya Sudan; inatafuta kuigawanya Sudan katika nchi dhaifu, zilizogawanyika. Aliongeza kuwa huu ndio uhalisia wa kile ambacho Amerika inatamani, na kwamba watawala wanatii sera zake za njama dhidi ya Sudan.
Taarifa kwa Vyombo vya Habari
Msemaji huyo rasmi alitoa taarifa kadhaa kwa vyombo vya habari akifafanua msimamo wa Hizb ut Tahrir kuhusu masuala yanayoikabili Sudan, akielezea hukmu ya Kiislamu juu yake. Miongoni mwa taarifa hizi kwa vyombo vya habari ni yafuatayo: (Sudan Kusini Yavuka Mistari Mekundu na Viambatisho vya Abyei; Mwitikio wa Serikali ya Sudan ni Dhaifu) Dola ya Sudan Kusini imechukua hatua za kuiunganisha eneo la Abyei; Kwa kuijumuisha katika uchaguzi uliopangwa kufanyika Disemba 2026, msemaji rasmi alitoa taarifa ambapo alisema: "Kitendo hiki cha serikali ya Sudan Kusini ni kuvuka mipaka mikubwa, na hata kutangaza vita!… Msimamo unaopaswa kuchukuliwa ni angalau kutishia kufuta makubaliano yote na Sudan Kusini, ikiwa ni pamoja na Mkataba wa Naivasha ambao haujafanikiwa, na kuzingatia Sudan Kusini kama sehemu ya Sudan; ambayo ndiyo hali ya asili,
﴿وَإِمَّا تَخَافَنَّ مِن قَوْمٍ خِيَانَةً فَانبِذْ إِلَيْهِمْ عَلَىٰ سَوَاءٍ إِنَّ اللَّهَ لَا يُحِبُّ الْخَائِنِينَ﴾.
“Na ukichelea khiana kwa watu fulani basi watupilie ahadi yao kwa usawa. Hakika Mwenyezi Mungu hawapendi makhaini.” [Anfal: 58]
Bwawa la Grand Renaissance la Ethiopia (GERD) na athari zake mbaya kwa Sudan
Kwa kuwa viwango vya maji vya Mto Nile vinapungua na vituo vingi vya maji vinakatika kutokana na kuzuiliwa kwa maji nyuma ya Bwawa la Grand Renaissance la Ethiopia, msemaji rasmi alitoa taarifa yenye kichwa: "Kile ambacho Hizb ut Tahrir ilionya yapata miaka tisa iliyopita kimekuwa ukweli... GERD inasababisha Mto Nile kupungua na vituo vya maji vinakatika." Taarifa hiyo ilisomeka: "Hili lilitarajiwa... Tulielezea hatari ya Bwawa la Grand Renaissance la Ethiopia kwa usalama wa maji wa Sudan na Misri, na jinsi watawala wa Misri na Sudan wamepoteza haki za taifa walipokubali ujenzi wa bwawa hili baya kwa kusaini Mkataba wa Azimio la Kanuni huko Khartoum mnamo Machi 23, 2015." Msemaji huyo aliongeza: "Ili kupinga bwawa hili, tulifanya semina na vikao vingi, tukiwakaribisha wataalamu wa maji waaminifu ambao walielezea hatari ambayo bwawa hili linaleta kwa usalama wa maji wa Sudan na Misri." Lakini ni kama kuzungumza na ukuta wa matofali! Watawala hawa hawajali mambo ya umma; bali wanapoteza haki zake!
Vikosi vya usalama vyamkamata mwanachama wa Hizb ut Tahrir katika mji wa Al-Shawwak kutokana na chapisho la mitandao ya kijamii!
Kufuatia chapisho la Nasr al-Din, mmoja wa wabebaji dawah mjini Al-Shawwak, kwenye ukurasa wake wa Facebook, ambapo alitoa wito kwa serikali kulinda maisha, kudumisha usalama, na kuwalinda vijana kutokana na dawa za kulevya, vikosi vya usalama vilimkamata na kumtungia mashtaka chini ya Kifungu cha 69 (Utaratibu wa Umma). Kujibu, msemaji huyo alitoa taarifa kwa vyombo vya habari yenye maneno makali, akifafanua kwamba vitendo vya Nasr al-Din vilikuwa vya waumini wanaoamrisha mema na kukataza maovu, huku vitendo vya ujasusi wa kijeshi vikiwa vya wanafiki. Taarifa hiyo iliionya serikali na vyombo vyake vya usalama na kijeshi kuhusu hatima inayowasubiri wale wanaozuia njia ya Mwenyezi Mungu na kutafuta kuipotosha. Iliwahimiza watubu kwa Mwenyezi Mungu, kumwachilia huru Nasr al-Din mara moja, na kumuomba msamaha. Badala ya kutii maonyo, watawala walirekebisha Kifungu cha 25, kinachohusu kuwatukana watu binafsi. Kisha msemaji huyo alitoa taarifa nyengine akishutumu mwenendo wa vyombo vya usalama vya utawala, akisisitiza msisitizo wake wa kufuata njia ya upotoshaji, kutunga mashtaka, na kuwasilisha ripoti mbaya dhidi ya wanachama waaminifu wa umma huu wanaotamani mema kwa nchi na watu wake na kujitahidi kubadilisha uhalisia huu mbovu kwa msingi wa Uislamu. Alisisitiza kwamba kukamatwa na kufungwa kutaimarisha tu azma ya mashababu wa Hizb ut Tahrir ya kutetea haki na kubaki imara katika njia hiyo, hata kama wachache wataifuata.
Hii ni pamoja na taarifa zengine, habari kwa vyombo vya habari, na makala zinazozungumzia masuala muhimu katika uwanja wa kisiasa wa Sudan.
3) Majukwaa ya Hizb ut Tahrir / Wilayah ya Sudan:
Changamoto za Uhalisia: Kati ya Masuluhisho ya Dola za Kiraia na Khilafah
Afisi ya Habari ya Hizb ut Tahrir katika Wilayah ya Sudan ilifanya majukwaa yake ya kawaida mwezi huu katika afisi zake mbalimbali. Mjini Port Sudan, jukwaa lilishughulikia masuala yanayoukabili Ummah, haswa changamoto za uhalisia na masuluhisho yanayotolewa na dola ya kiraia na Khilafah. Katika uwasilishaji wa kwanza, Ustadh Nasser Ridha, Mkuu wa Kamati Kuu ya Mawasiliano, alifafanua dol ya kiraia na kuelezea kushindwa kwake kushughulikia changamoto za kisiasa na kiuchumi za hali ya sasa. Kisha, Ustadh Ibrahim Mushrif, mjumbe wa Afisi ya Habari katika Wilayah ya Sudan, alizungumza, akifafanua Khilafah, msingi wake, na jinsi inavyokabiliana na kutatua changamoto hizi kwa hukmu za Sharia kutoka kwa Muumba wa Wanadamu.
Matatizo ya Kilimo mjini Al-Qadharif:
Katika jukwaa la kawaida lililofanyika Al-Qadharif siku ya Jumamosi, 4 Safar 1448 H (Julai 18, 2026), lenye kichwa "Kilimo mjini Al-Qadharif: Kati ya Uhalisia Uliofeli na Masuluhisho ya Kiislamu," Ustadh Awad Muhajir alishughulikia matatizo yanayokabili kilimo na wakulima mjini Al-Qadharif. Alielezea matatizo haya kama yanayojirudia, hata ya makusudi, akifichua kupuuza kwa serikali kilimo na ukosefu wa usaidizi, hasa mwanzoni mwa msimu wa mvua.
Ustadh Nasr al-Din al-Hajj kisha aliwasilisha masuluhisho ya Kiislamu kwa matatizo ya kilimo. Alisema kwamba katika Uislamu, dola huwafadhili wakulima bila riba na hata huwasamehe madeni yao ili kuwatia moyo. Hii inalenga kufikia kujitosheleza na matumizi bora ya ardhi. Alitaja matendo ya Makhalifa Waongofu na utunzaji wao bora kwa wakulima katika Khilafah.
4) Hotuba za Kisiasa:
Mbinu za Uislamu za Kukabiliana na Tatizo la Ukosefu wa Usalama
Hizb ut Tahrir/Wilayah Sudan ilifanya hotuba zake za kisiasa za kila wiki katika soko kuu la Port Sudan. Katika hotuba ya kwanza, Ustadh Hussein al-Hadi alielezea kwamba ukosefu wa usalama ni matokeo yasiyoepukika ya kutokuwepo kwa sheria za Kiislamu zinazozuia maisha, na kwamba watu hupata usalama chini ya Uislamu. Kisha aliwataka waliokuwepo kufanya kazi kuelekea kusimamishwa kwa Khilafah Rashida, ili watu waweze kuishi maisha ya Kiislamu ambayo usalama na utulivu vitatawala.
Tatizo la Dawa za Kulevya: Sababu na Suluhisho
Katika hotuba ya pili, Ustadh Adel Ibrahim alizungumzia kuhusu uharamu wa dawa za kulevya na athari zake mbaya kwa jamii, hasa kwa vijana, ambao ndio uti wa mgongo wa mwamko wa umma. Aliona kuenea kwa dawa za kulevya za kila aina kuwa sehemu ya vita vya kizazi cha nne vinavyofadhiliwa na Magharibi ya kikoloni ya kikafiri. Alisema kwamba vyombo vyenye ushawishi vinaweza kuleta idadi kubwa ya dawa hizi. Alisisitiza kwamba kampeni za kuwafuata wafanyibiashara wadogo hazitatui tatizo; badala yake, suluhisho msingi liko katika sheria za kuzuia ambazo zitawafanya wafanyibiashara wa dawa za kulevya kusahau minong'ono ya Shetani.
Mwenye heshima zaidi miongoni mwenu mbele ya Mwenyezi Mungu ni mchamungu zaidi kati yenu.
Katika hotuba hii, Ustadh Adel Ibrahim alizungumzia kuhusu dori ya kabila, akisisitiza kwamba ni kwa ajili ya uelewano wa pande zote, si kwa ajili ya kujisifu. Alieleza kwamba kuhimiza upatanifu wa kikabila na kujihami husababisha chuki na vita. Pia alisisitiza hatari ya kuwahamasisha watu kwa misingi ya kikabila, mbinu inayotumiwa na mkoloni kafiri kupanda mgawanyiko miongoni mwa Waislamu huku wakati huo huo akifanya kazi ya kuimarisha safu zake mwenyewe. Alimalizia kwa kutoa wito kwa makabila haya kuunganishwa ili kunusuru Uislamu na kufanya kazi ya kusimamisha dini ya Mwenyezi Mungu duniani chini ya Khilafah Rashida, kwa njia ya Utume, kama Ansar walivyofanya.
Sababu Halali za Kumiliki Utajiri katika Uislamu
Hotuba ya Jumatatu, 13 Safar 1448 H (Julai 27, 2026 M), ililenga umiliki wa mtu binafsi katika Uislamu. Ustadh Adel Ibrahim alifafanua sababu halali za watu kumiliki mali ili kukidhi mahitaji ya msingi, akielezea kwamba Uislamu umerahisisha njia za kupata riziki yenye heshima. Kisha akawasihi watu kupuuza sheria zilizotungwa na wanadamu zinazowazuia na kuwanyima haki ya kutafuta mapato halali.
5) Kikao cha Kisiasa:
Ukweli wa Dori ya Marekani katika Vita vya Sudan
Kikao cha Kisiasa cha mwezi huu kilimkaribisha Ustadh Ibrahim Mushrif katika kipindi kilichoitwa: "Ukweli wa Dori ya Marekani katika Vita vya Sudan." Alijadili dori ya Marekani nchini Sudan, akifafanua dhana potofu inayoshikiliwa na taasisi ya kisiasa kwamba Amerika ni mpatanishi tu katika vita vya Sudan. Alitaja ushahidi wa kushawishi kwamba Amerika ilichochea vita hivi ili kuondoa, iwezekanavyo, ushawishi wa Ulaya, unaowakilishwa na raia na harakati za kijeshi za Darfur. Amerika pia inatafuta kutenganisha Darfur na mwili wa Sudan. Inasimamia vita hivi ili kufikia malengo yake, na ni Khilafah Rashida pekee, iliyoanzishwa kwa njia ya Utume, ndiyo itakayoizuia.
Miongoni mwa shughuli katika Wilayah ya Sudan ni makumi ya khutba na mihadhara kadhaa katika miji mbalimbali ya Sudan, ikiutaka Ummah kufanya kazi kuelekea Khilafah Rashida kwa njia ya Utume, ambayo itarudi hivi karibuni, Mwenyezi Mungu akipenda.
(إِنَّهُ لَقَوْلٌ فَصْلٌ * وَمَا هُوَ بِالْهَزْلِ)
“Hakika hii ni kauli ya kupambanua. Wala si mzaha.” [Al-Tariq: 13-14]
Mjumbe wa Afisi Kuu ya Habari ya Hizb ut Tahrir katika Wilayah ya Sudan
Ijumaa, 17 Safar 1448 H, sawia na 31 Julai 2026 M

-
Click to open image!
Click to open image!
-
Click to open image!
Click to open image!
-
Click to open image!
Click to open image!
-
Click to open image!
Click to open image!
-
Click to open image!
Click to open image!
-
Click to open image!
Click to open image!
-
Click to open image!
Click to open image!
-
Click to open image!
Click to open image!
-
Click to open image!
Click to open image!
-
Click to open image!
Click to open image!
-
Click to open image!
Click to open image!
https://www.hizb-ut-tahrir.info/sw/index.php/dawah/sudan/5422.html#sigProIdc7e9481e06

Kwa Maelezo Zaidi Tafadhali Zuru Mitandao ya Hizb ut Tahrir / Wilayah Sudan:
Tovuti Rasmi ya Hizb ut Tahrir / Wilayah Sudan
Ukurasa wa Facebook wa Hizb ut Tahrir / Wilayah Sudan
Chaneli ya YouTube ya Hizb ut Tahrir / Wilayah Sudan




