Jumamosi, 16 Jumada al-thani 1447 | 2025/12/06
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Kukabiliana na Mayahudi ni jambo la Aqidah. Kujitayarisha kwa ajili yake Ni Faradhi ya Shariah, na Kuliepuka ni Maangamivu

Baadhi ya wanasiasa wa Syria hivi majuzi wamekuwa wakiendeleza wazo kwamba “hatutauza udanganyifu kwa watu wetu, na kwamba lazima tuchukue hatua ya kweli ili kujenga upya serikali.” Hili linafanywa kwa kisingizio kwamba “tunafahamu uwezo wetu wa kweli, na lugha ya vitisho haitakuwa na manufaa yoyote katika kukabiliana na uvamizi wa Kizayuni,” na kwamba “mazungumzo nao yanaendelea ili kuregea kwenye makubaliano ya 1974!”

Soma zaidi...

Maandamano ya Umwagaji damu nchini Indonesia na Chanzo Chake

Tangu tarehe 25 Agosti, 2025, Indonesia imekuwa ikishuhudia wimbi la maandamano makubwa yaliyorekodiwa katika maeneo 107 katika mikoa 32. Huku baadhi ya maandamano yakiendelea kuwa ya amani, mengi yalizidi kuwa ghasia zilizohusisha uharibifu na uchomaji moto. Maeneo kadhaa yalishuhudia machafuko makubwa zaidi, ikiwemo mji mkuu Jakarta, Java ya Kati, Java Mashariki, Java Magharibi, Yogyakarta, Sumatra Kaskazini, Nusa Tenggara Magharibi, Sulawesi Kusini, na Kalimantan Magharibi. Vituo vya umma, afisi za serikali, na hata mali za usalama wa taifa zilipata uharibifu mkubwa. Jijini Jakarta, kwa mfano, vituo 22 vya mabasi ya TransJakarta na vituo vya treni ya chini ya ardhi vya MRT viliharibiwa, huku hasara ikikadiriwa kuwa karibu rupiah bilioni 50.4 za Indonesia.

Soma zaidi...

Matukio ya Kisiasa ya Hivi Majuzi nchini Yemen Yanaonyesha Nini?

Mnamo Alhamisi, 28 Agosti, Waziri Mkuu wa Wizara ya Mabadiliko na Ujenzi, Ahmed Ghaleb Al-Rahwi, aliuawa, pamoja na mawaziri wengine tisa: Waziri wa Sheria na Haki za Binadamu Mujahid Ahmed Abdullah Ali; Waziri wa Uchumi, Viwanda na Uwekezaji Moeen Hashim Ahmed Al-Mahaqri; Waziri wa Kilimo, Uvuvi na Rasilimali za Maji Radwan Ali Ali Al-Rubai; Waziri wa Mambo ya Nje na Wageni Jamal Ahmed Ali Amer; Waziri wa Umeme, Nishati na Maji Ali Seif Mohammed Hassan; Waziri wa Utamaduni na Utalii Ali Qasim Hussein Al-Yafei; Waziri wa Masuala ya Jamii na Leba Samir Mohammed Ahmed Bajaala; Waziri wa Habari Hashim Ahmed Abdul Rahman Sharaf Al-Din; na Waziri wa Vijana na Michezo Mohammed Ali Ahmed Al-Mawlid. Mawaziri wengine kadhaa bado wako katika hali mbaya na ya wastani, akiwemo Jalal Al-Ruwaishan, Naibu Waziri Mkuu wa Masuala ya Ulinzi na Usalama. Umbile la Kiyahudi limeeleza kuwa lilifanya shambulizi hilo, likiwalenga Waziri wa Ulinzi Mohammed Al-Atifi na Mkuu wa Majeshi Mohammed Abdul Karim Al-Ghamari.

Soma zaidi...

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu