Mambo Muhimu Kuhusu Ziara ya Rais wa Syria, Ahmad al-Shara, jijini Moscow
- Imepeperushwa katika Al-Rayah
- Kuwa wa kwanza kutoa maoni!
- |
Rais wa mpito wa Syria, Ahmad al-Sharaa, akifuatana na ujumbe rasmi uliojumuisha waziri wake wa mambo ya nje, Asaad Al-Shaibani, walizuru mji mkuu wa Urusi, Moscow, mnamo 15 Oktoba 2025. Walikutana na Rais wa Urusi Putin katika ziara yao ya kwanza rasmi tangu kuanguka kwa utawala wa Assad, mwishoni mwa mwaka jana.



