Gazeti la Al-Raya: Vichwa Vikuu vya Toleo 569
- Imepeperushwa katika Al-Rayah
- Kuwa wa kwanza kutoa maoni!
Vichwa Vikuu vya Toleo 569
Vichwa Vikuu vya Toleo 569
Mnamo Jumapili, 12 Oktoba 2025, Hizb ut Tahrir/Wilayah ya Tunisia iliandaa kikao cha mazungumzo kwa kichwa “Mradi wa Ukombozi... Katika Mizani ya Hukmu za Sheria ya Kiislamu” katika eneo la Kairouan. Kikao hicho kilihudhuriwa na idadi kubwa ya wakaazi wa eneo hilo.
Mnamo tarehe 9 Oktoba, Gazeti la ‘the Guardian’ liliripoti kwamba mkuu wa shirika la kutoa misaada la Waislamu wa Uingereza Shaista Gohir, alikuwa na 'wasiwasi mkubwa' huku uhalifu wa chuki dhidi ya Uislamu ukiongezeka kwa theluthi moja kulingana na takwimu za hivi punde za serikali. Alisisitiza kuwa hata takwimu hizi zinazosumbua pengine ni ‘sio halisi’ kwani matukio mengi hayaripotiwi.
Uhalisia wa sasa wa Waislamu leo ni sawa na awamu ya Makka ya ujumbe wa Mtume, kwani wanaishi katika “Dar ul-Kufr” (Nyumba ya Ukafiri) kutokana na kutawaliwa na sheria zisizokuwa zile zilizoteremshwa na Mwenyezi Mungu (swt) na neno “Dar” ni istilahi ya kifiqhi iliyofafanuliwa kwa kina katika vitabu vya fiqh (Fiqh ya Shariah). Hili linalazimu kufuata njia ya mabadiliko ya Makka. Mtume (saw) alifuata hatua tatu kuu katika njia yake ya kusimamisha dola ya Kiislamu.