Jumamosi, 24 Shawwal 1447 | 2026/04/11
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu
kesho kutwa

kesho kutwa

Tanzia ya Mwanachama wa Afisi ya Amiri, Ustadh Ahmad Bakr (Abu Osama)

Amiri wa Hizb ut Tahrir, Wanachama wa Afisi ya Amiri, Diwani ya Al-Madhalim (Malalamiko), na Afisi Kuu ya Habari na Hizb ut Tahrir kwa jumla wanaomboleza kwa Umma wa Kiislamu Mwanachama wa Afisi ya AmIrI, Ustadh Ahmad Bakr (Abu Osama) aliyefariki dunia asubuhi ya leo, 22 Rabi’ Al-Awwal 1447 H sawia na tarehe 14 Septemba 2025 M, akiwa na umri wa miaka themanini na saba.

Mateso ya watu wa Palestina kwenye Daraja la Mfalme Hussein (Allenby) Kati ya Msongamano, Ufisadi, na Mfumo wa Hatari wa Tabaka la VIP

Kwa kuzingatia njama ya dola jirani  za eneo dhidi ya Ardhi Iliyobarikiwa ya Palestina ili kukaza mzingiro dhidi ya watu wake, kuwadhuru, na kuwasukuma kuiacha ardhi yao na kuikabidhi kwa Mayahudi, Daraja la Mfalme Hussein (Allenby au Karameh) linaunda njia kuu ya maisha ya watu wa Palestina kwa ulimwengu wa nje. Hata hivyo, kivuko hiki, ambacho kinapaswa kuwa njia ya usafiri, kimekuwa chanzo cha mateso ya kila siku kwa wasafiri, hasa upande wa Jordan, ambapo mambo ya kibinadamu, ya kiutawala, na ya kisiasa yanaingiliana na kuunda mandhari katili sana.

Enyi Watu wa Jordan na Wanajeshi Wake: Jihadharini na Kundi la Kitengo cha Gilead, Vitisho vya Umbile la Kiyahudi kwa Nchi yenu, na Ushiriki na Utiifu wa Serikali!

Jana, 10 Septemba 2025, kamanda wa Kamandi Kuu ya jeshi la umbile la Kiyahudi alitangaza kuundwa kwa kitengo kipya cha kijeshi, kinachoitwa “Kitengo cha Gilead,” katika Bonde la Jordan, kitakacho kaa kwenye Bonde la Jordan. Kitengo hichi cha kikanda kina jukumu la kulinda mipaka ya mashariki ya Mayahudi katika Bonde la Jordan na Bahari ya Dead. Aliashiria kuwa kuanzishwa kwa kitengo hicho kunajiri ndani ya muundo wa kile alichoelezea kama “masomo ya kujifunza kutokana na kushindwa kugumu kwa Israel mnamo Oktoba 7, 2023.” Uundaji huu mpya unakuja baada ya vitisho vya viongozi wa umbile la Kiyahudi kupanuka hadi nchini Jordan na kwengineko chini ya mwavuli wa mradi wa “Israel Kubwa”, uliotangazwa na Netanyahu, uliobarikiwa na Trump, na kutangazwa wazi na Smotrich, Waziri wa Fedha wa umbile la Kiyahudi.

Jiunge kwa hii RSS feed

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu