Alhamisi, 22 Shawwal 1447 | 2026/04/09
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu
kesho kutwa

kesho kutwa

Wanachama wa Hizb ut Tahrir huko Abbasiya Watangaza: Tibueni Mpango wa Amerika wa Kutenganisha Darfur

Kama sehemu ya kampeni iliyoandaliwa na Hizb ut Tahrir/Wilayah Sudan kutibua mpango wa kuichana Sudan kwa kutenganisha eneo la Darfur, na kwa kuzingatia kwamba umoja wa Ummah ni suala nyeti, ambalo ni lazima hatua za uhai au kifo zichukuliwe, Mashababu (wanachama) wa Hizb ut Tahrir walifanya mkutano mnamo Ijumaa, 6 Rabi’ al-Awwal 1447 H, sawia 29 Agosti 2025 M, baada ya swala ya Ijumaa, katika Msikiti wa Sheikh Yahya wa Kuhifadhi Qur'an. Walitoa wito wa dhati kwa Waislamu wa makundi yote, wakiwemo wanasiasa, wanahabari, maulamaa, maafisa na wanajeshi, na wengineo, wakiwataka watimize wajibu wao wa Shariah wa kuzuia kujitenga kwa Darfur.

Matarajio Yasio na Msingi: Nchini Uzbekistan, Mhubiri Aliyetoka Nchini Uturuki Ashtakiwa

Mahakama ya Jinai ya Wilaya ya Uchtepa ya Tashkent ilianza kusikiliza mnamo Agosti 19 kesi ya jinai dhidi ya mtu wa dini Alisher Tursunov, anayejulikana kwa umma kwa jina bandia la Mubashshir Ahmad. Habari hiyo iliripotiwa na Aziz Abidov, mkuu wa huduma ya vyombo vya habari wa Mahakama ya Upeo ya Uzbekistan. Kulingana na tuhuma ya mashtaka, Tursunov anashtakiwa chini ya vifungu vitatu vya Kanuni ya Jinai ya Uzbekistan.

Wahanga wa Vita Wanaoteseka Zaidi ni Watoto wa Gaza wenye Ulemavu

Vita vya maafa dhidi ya Gaza, vilivyoanza mnamo Oktoba 7, 2023, vimeathiri kila nyanja ya maisha huko: watu, miti, mawe, na rasilimali, hasa wanawake na watoto. Vifo na uharibifu vimeenea kila mahali. Kulingana na Wizara ya Afya mjini Gaza, vimesababisha vifo vya zaidi ya watu 63,000, kujeruhiwa kwa wengine 160,000, na mamia ya maelfu ya watu kuyahama makaazi yao, huku kukiwa na janga kubwa la kibinadamu linalojumuisha uhaba wa chakula, dawa, na maji safi ya kunywa.

Upenyaji wa Mayahudi wa Jeshi la Misri

Tangu serikali ya Misri itie saini Makubaliano ya Camp David mwaka 1979, jeshi la Misri limeingia katika njia ya utegemezi na upenywaji, likijitenga na kanuni yake ya awali ya kuulinda Ummah na kulinda mipaka yake dhidi ya maadui wake wa kweli, wa kwanza miongoni mwao ni Mayahudi walioinyakua Palestina. Hatua kwa hatua, taasisi hii imebadilika na kuwa chombo kilichozuiliwa, chini ya masharti ya adui, hata kushiriki katika kuilinda na kuiwezesha kupitia mikataba ya kijeshi, usalama, kiuchumi, na ushauri ambayo iliunda utaratibu kamili wa ushawishi wa Kiyahudi, ndani ya jeshi na dola.

Jiunge kwa hii RSS feed

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu