Jumatano, 05 Dhu al-Qi'dah 1447 | 2026/04/22
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu
kesho kutwa

kesho kutwa

Umbile la Kiyahudi Linatekeleza Mauaji ya Halaiki na Unyanyasaji wa Kijinsia mjini Gaza. Je, Kuna Njia ya Kuamsha Uzembe Huu?

Tangu kutekelezwa Operesheni ya Kimbunga cha Al-Aqsa mnamo 7 Oktoba 2023, umbile la Kiyahudi limewatenga watu walio na msimamo thabiti wa Gaza na kumwaga chuki yake juu yao. Limefanya mauaji ya mfululizo ambayo yamesababisha makumi ya maelfu kuuawa shahidi, huku Umma wa Kiislamu ukiwa bado umefungwa pingu na majeshi yake yamenyamaza kimya kama watu wa makaburini! Lilianza tena mauaji yake baada ya kukiuka usitishaji vita, kwa uungaji mkono wa wazi wa Magharibi na ushirikiano wa wazi na wa aibu wa tawala angamivu katika nchi za Waislamu.

Leo Gaza na Yemen, na Kesho nchi zengine za Waislamu, Isipokuwa Majeshi yao Yatangaze Kusonga

Kamandi Kuu ya Ulinzi ya Marekani (CENTCOM) ilitangaza kwamba jioni ya Jumamosi, 15 Machi 2025, ilianzisha msururu wa mashambulizi ya anga dhidi ya maeneo lengwa ya Mahouthi nchini Yemen. Ilidai kuwa ilifanya mashambulizi sahihi dhidi ya maeneo lengwa ya kundi hilo kote Yemen, ikihalalisha mashambulizi hayo kama utetezi wa maslahi ya Marekani, kuzuia dhidi ya maadui, na kuregesha uhuru wa bahari, kulingana na taarifa yake. Kufikia Alhamisi jioni, Machi 20, makumi ya mashambulizi ya anga ya Marekani dhidi ya Yemen yalikuwa yameripotiwa, na kusababisha vifo vya watu 53 na wengine zaidi ya 100 kujeruhiwa, wengi wao wakiwa wanawake na watoto. Kuna matarajio kwamba operesheni zitaendelea kwa wiki kadhaa. Haya ni mashambulizi ya kwanza dhidi ya Yemen tangu makubaliano ya kusitisha mapigano kati ya umbile la Kiyahudi na Hamas mjini Gaza Januari iliyopita, kufuatia kiapo cha Trump cha "kuwamaliza kabisa."

Hizb ut Tahrir / Wilayah Uturuki: Dua ya Kunut “Kwa ajili ya Gaza... Mikono Imeinuliwa Mbinguni?!”

Kwa kuzingatia mauaji ya kikatili ya halaiki ambayo yamekuwa yakiendelea kwa zaidi ya miezi 17, yanayofanywa na umbile halifu la Kiyahudi dhidi ya Waislamu wasio na ulinzi katika Ukanda wa Gaza, ambayo yamesababisha kuuawa shahidi na kujeruhiwa kwa Waislamu zaidi ya 170,000, wanaume na wanawake hadi sasa, Hizb ut Tahrir / Wilayah ya Uturuki iliandaa amali “Dua ya Kunut” kufuatia umbile halifu la Kiyahudi kukiuka makubaliano dhaifu ya kusitisha mapigano alfajiri ya Jumanne, 18 Machi 2025, na kuanza tena mauaji yake ya kimpangilio ya Waislamu wasio na ulinzi, ambao wengi wao wakiwa ni wanawake, watoto na wazee, chini ya kichwa: Dua ya Kunut “Kwa ajili ya Gaza... Mikono Imeinuliwa Mbinguni?!”

Jiunge kwa hii RSS feed

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu