Ijumaa, 07 Dhu al-Qi'dah 1447 | 2026/04/24
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu
kesho kutwa

kesho kutwa

Amerika Yala Sanamu Lake Yenyewe!

Katika Arabuni ya kabla ya Uislamu, baadhi ya Waarabu walikuwa wakitengeneza masanamu yao kutokana na tende; walipohisi njaa, wangekula miungu yao! Leo, historia inajirudia yenyewe, lakini kwa umbo gumu zaidi. Mfumo wa Kimagharibi ambao hapo awali uliinyanyua fahamu ya uhuru hadi kwenye hadhi takatifu—uhuru wa fikra, dhamiri, na dini; uhuru wa kuzungumza na kujieleza; uhuru wa kukongamana kwa amani; ushiriki wa kisiasa; ulinzi wa haki za walio wachache; na kukataza utesaji na kutendewa kikatili – sasa unasaliti maadili haya haya yanapokinzana na maslahi ya mabepari na kipote cha watawala.

Watawala Vibaraka Wamefichua Udanganyifu wa Ubwana wa Kitaifa na Maslahi ya Kitaifa. Ni Hoja Gani iliyopo ya Kuzuia Kukomeshwa kwa Mfumo wa uliopo Sasa?

Mnamo tarehe 11 Februari 2025, taarifa kwa vyombo vya habari ilitolewa kwenye tovuti ya Mahakama ya Upeo ya Pakistan, ambayo ilifichua mabaki ya udanganyifu wa ubwana wa kitaifa. Taarifa hiyo kwa vyombo vya habari ilisema kuwa Jaji Mkuu na maafisa wengine wa mahakama walikutana na ujumbe wa Mfuko wa Fedha wa Kimataifa (IMF) na kuwaeleza kuhusu masuala ya Mahakama ya Upeo. Katika taarifa hiyo, Jaji Mkuu alithibitisha kuwa Mahakama ya Upeo inakamilisha ajenda ya kikao cha Kamati ya Kitaifa ya Mahakama ya Utungaji Sera (NJPMC) katika wiki ya mwisho ya Februari. Hata aliwaalika wajumbe wa wakoloni pia kutoa mapendekezo yao katika suala hili.

Bajeti ya kila Mwaka ya Serikali: Utumwa wa Kudumu wa Kikoloni

Dola za kiliberali za kirasilimali zimeundwa kupitia mpango wa kifedha wa kila mwaka wa uendeshaji wa mapato na matumizi ya serikali. Sera hii ya kifedha ambayo inashirikisha nchi za ulimwengu wa tatu katika shinikizo kubwa la kuweka usawa kati ya usimamizi wa serikali wa mambo ya watu na utawala wa kikoloni. Sera ya fedha ya kimataifa (mfumo wa fedha zisizo na thamani ya dhati (fiat)) ambazo thamani zake zimeegemezwa kwa dolari kwa Petroli lazima zisawazishe biashara (mahuruji na maduhuli) ili kuelea thamani ya sarafu ya ndani kutokana na kuzama kwenye dimbwi la mporomoko wa kiuchumi.

Jiunge kwa hii RSS feed

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu