Alhamisi, 18 Ramadan 1445 | 2024/03/28
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

بسم الله الرحمن الرحيم

 Vichwa vya Habari: 10/08/2022

Vichwa vya Habari:

• Kupanda kwa Bei ya Mafuta Kwa Zusha Hatari ya Machafuko ya Kijamii

• Amerika Yaichochea China kwenye Vita

• Amerika Yamwaga Pesa nchini Ukraine

Maelezo:

Kupanda kwa Bei ya Mafuta Kwa Zusha Hatari ya Machafuko ya Kijamii

Serikali ya Bangladesh ilipandisha bei ya mafuta kwa asilimia 42 hadi 51, ambalo ndilo ongezeko kubwa zaidi katika historia ya nchi hiyo. Kupanda kwa bei kutaongeza mfumko wa bei ambao tayari uko juu nchini Bangladesh kwani kupanda kwa bei ya mafuta kunaathiri sekta kama vile kilimo na usafirishaji. Bangladesh imeshuhudia maandamano ya hapa na pale tangu ongezeko hilo la bei. Bangladesh hivi majuzi iliwasiliana na IMF, Benki ya Dunia na Benki ya Maendeleo ya Asia kuhusu kuimarisha akiba yake ya fedha za kigeni inayopungua. Serikali hiyo pia imeweka hatua kadhaa za kubana matumizi kama vile kusitisha uagizaji wa gesi asilia, kukatwa kwa umeme katika mikoa mbalimbali, vikwazo juu ya uagizaji bidhaa za anasa kutoka nje na kupunguza gharama kwa matumizi ya serikali.

Amerika Yaichochea China kwenye Vita

China imejibu ziara ya Spika wa Bunge la Marekani Nancy Pelosi nchini Taiwan mnamo tarehe 3 Agosti. Wizara ya ulinzi ya China ilitangaza mazoezi ya silaha halisi kuanzia Agosti 4 hadi 7 katika maeneo sita katika habari zinazoizunguka Taiwan. Kisha mnamo Agosti 4, Afisi ya Bahari na Bandari ya Taiwan ilidai kuwa China ilikuwa imeongeza eneo la saba na kuongeza mazoezi ya baharini. Mazoezi hayo kufikia sasa yamehusisha uvamizi wa wanamaji wa China na angani katika njia ya wastani ya Taiwan (laini inayotenganisha nchi hizo mbili) na majaribio ya makombora katika maeneo yaliyotengwa. Hili lilikuwa jibu lisilo na maana kutoka kwa China. Manuari na ndege nyingi zilirusha mashambulizi mengi, ambayo hakuna hata moja lililoipiga Taiwan au chombo cha uadui. Jibu hilo lilionyesha kuwa China ina jeshi la wanamaji, lakini haikuonyesha jinsi mizani ya utawala huenda ikabadilika endapo China itatungua kombora linalokuja. Jambo baya zaidi kwa China litakuwa kuingia vitani na kutumbukia katika uchochezi wa Marekani, ushawishi wa China wa kiuchumi na kibiashara juu ya Taiwan na imekiunganisha kisiwa hicho ndani ya Bara la China na hatua zozote za masikitiko zinaweza kuiona China ikikwama kwa vile Urusi sasa iko Ukraine.

Amerika Yamwaga Pesa nchini Ukraine

Marekani itatuma dolari bilioni 1 kama msaada wa ziada wa kijeshi kwa Ukraine, ikiwa ni sehemu kubwa zaidi ya kupunguza vifaa tangu kuanza kwa vita hivyo. Kifurushi cha hivi punde zaidi kitajumuisha silaha za ziada kwa mifumo ya roketi ya kivita yenye uhamaji wa hali ya juu (Himars), makumi ya maelfu ya mizinga na bunduki, mifumo ya kuzuia silaha na magari ya matibabu ya kivita. Ikiwemo pamoja na kifurushi hiki, Marekani sasa imetoa takriban dolari bilioni 9.8 kama msaada wa kiusalama kwa Ukraine tangu Rais Joe Biden aingie madarakani. Msaada huo mpya wa Marekani unakuja wakati Kyiv inajiandaa kuanzisha mashambulizi mapya kusini, ambapo inatarajia kurudisha mji wa Kherson na kukomesha matumizi ya Urusi ya mto Dnipro kama kizuizi cha kimaumbile. Kando na hayo, Shirika la Marekani la Maendeleo ya Kimataifa lilitangaza kuwa litatoa dolari bilioni 4.5 kwa serikali ya Ukraine ili kufidia sehemu ya nakisi ya bajeti yake. Marekani inaendelea kumwaga pesa katika mzozo huo huku mataifa ya magharibi yakijiandaa kukabiliana na uhaba wa nishati na msimu wa baridi usioridhisha. Urusi inaendelea kutumia rasilimali zake za nishati  kama silaha na mataifa mengi ya Ulaya, ikiwemo Ujerumani yanategemea nishati ya Urusi. Ingawa Marekani imeweza kuichochea Urusi kuanzisha vita, Marekani haimiliki karata zozote za ace katika mzozo huo.

Andika maoni

Hakikisha umejaza (*) habari zinazohitajika palipoashiriwa. Kodi za HTML haziruhusiwi.

rudi juu

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu