Alhamisi, 18 Ramadan 1445 | 2024/03/28
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

بسم الله الرحمن الرحيم

 Vichwa vya Habari 23/11/2022

Vichwa vya Habari:

  • China Yafunga Mkataba wa Gesi pamoja na Qatar
  • COP27: Lakini Hakuna Maendeleo kwa Mafuta ya Kisukuku

Maelezo:

China Yafunga Mkataba wa Gesi pamoja na Qatar

China imefunga moja ya mikataba mikubwa zaidi ya gesi asilia majimaji (LNG) pamoja na Qatar yenye thamani ya dolari bilioni 60, Shirika la Habari la Qatar lilitangaza. Mkataba huo wa kihistoria na nchi yenye uchumi wa pili kwa ukubwa duniani unatazamiwa kuimarisha usalama wa kawi wa Beijing kwa miongo kadhaa na ni mapinduzi makubwa kwa China huku nchi zikikimbilia kufunga mikataba ya kawi kutokana na uhaba unaosababishwa na vita vya Urusi na Ukraine.

Nchi kote ulimwenguni, haswa Ulaya, zimekuwa zikikimbilia kupata mahitaji ya kawi kutoka kwa wazalishaji wakuu wa Qatar na Amerika, na kusababisha bei kupanda kwa kiasi kikubwa. Vyanzo vilivyopo vya gesi ya bomba na LNG tayari vimetolewa kwa ajili ya mustakbali wa karibu, na makubaliano kati ya Qatar na China yanatarajiwa kuongeza bei ya juu ya saruji.

COP27: Lakini Hakuna Maendeleo kwa Mafuta ya Kisukuku

Mnamo Novemba 20, wajumbe katika Kongamano la Tabianchi la COP27 nchini Misri walifikia makubaliano ya kuunda hazina inayoitwa "hasara na uharibifu" ambapo nchi tajiri zitasaidia kifedha nchi maskini zilizoathiriwa sana na athari za mabadiliko ya tabianchi, kama vile vimbunga usumbufu na ukame unaoharibu. Ingawa hazina hiyo ni hatua muhimu, makubaliano ya COP27 hayakujumuisha maandishi makali zaidi juu ya kukomesha miradi ya mafuta ya kisukuku na badala yake yalijumuisha tu kukomesha kawi ya makaa ya mawe - ahadi ambayo nchi zilikuwa tayari zimekubaliana kabla ya kongamano la mwaka huu. Mkataba huo pia haujumuishi ahadi mpya za kuharakisha upunguzaji wa hewa chafu. Ukosefu wa maendeleo katika kukata uzalishaji wa kaboni na kuongeza kasi ya mpito kutoka kwa mafuta ya kisukuku katika COP27 unaonyesha kuwa mchakato wa sasa wa mazungumzo ya Umoja wa Mataifa unaweza kufikia kikomo, ambapo itawalazimisha wajumbe kupunguza matarajio.

Andika maoni

Hakikisha umejaza (*) habari zinazohitajika palipoashiriwa. Kodi za HTML haziruhusiwi.

rudi juu

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu