Watawala wa Bara Arabu Wanashindana katika Ufisadi na Utiifu kwa Maadui wa Ummah!
- Imepeperushwa katika Afisi Kuu ya Habari
- Kuwa wa kwanza kutoa maoni!
- |
Siku chache zilizopita, watawala wa Imarati walijigamba juu ya uhamasishaji wao mkubwa wa kuwafikia wauaji wa Rabbi wa Kiyahudi, Zvi Kogan, kwenye ardhi zao, na kupongeza umakini wa vyombo vya usalama na kasi ya taratibu zao zilizochangia kufichua tukio hilo, baada ya huduma hizi zote kufanya kwa muda wote, kulingana na yale yaliyoelezwa katika taarifa ya Wizara ya Mambo ya Ndani. Wakati huo huo, Imarati na Wizara yake ya Ulinzi haikujitolea kuwanusuru zaidi ya mashahidi elfu 44 na elfu 104 waliojeruhiwa huko Gaza, ingawa muuaji wao anajulikana na haihitaji uchunguzi au umakini wa vyombo vya usalama kumfikia.