Hawajaridhika na Uharibifu wa Gaza, Wazayuni Sasa Wanaendeleza Uhalifu Wao hadi Lebanon
- Imepeperushwa katika Australia
- Kuwa wa kwanza kutoa maoni!
- |
Baada ya mwaka mmoja wa kampeni ya wazi ya mauaji ya halaiki dhidi ya watu wa Palestina, iliyofanywa mchana kweupe kwa ushirikiano wa dola za kimataifa na watawala wa Waislamu wanaowazunguka, Wazayuni hivi sasa wameendeleza jinai zao hadi Lebanon kwa kulipua mabomu kiholela katika makaazi yenye wakaazi wengi, na kuua maelfu ya watu tayari, kwa matumaini wanaweza kurekebisha sura yao iliyoshindwa baada ya kampeni yake angamivu mjini Gaza.