Jumamosi, 29 Safar 1447 | 2025/08/23
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Ufuatiliaji Mkubwa wa Mkoloni Amerika juu ya kile kinachoitwa “Mageuzi” sio Chengine ila ni Jaribio la kupanua Udhibiti wake nchini Bangladesh

Balozi Mdogo wa Marekani jijini Dhaka, Tracy Ann Jacobson, alifanya mkutano na Profesa Ali Riaz, Makamu Mwenyekiti wa Tume ya Kitaifa ya Maridhiano wiki iliyopita ili kuuliza kuhusu mipango ya mageuzi inayoendelea na maendeleo yake. Jacobson na manaibu wake wamekuwa wakifanya mfululizo wa mikutano na wawakilishi wa vyama vikuu vya kisiasa. Kama sehemu ya ushirikiano wa Marekani ‘kukuza demokrasia’ nchini Bangladesh, tunaona mikutano na taarifa za mara kwa mara kutoka kwa Ubalozi wa Marekani nchini Bangladesh na Wizara ya Mambo ya Nje ya Marekani zinazohimiza marekebisho katika utawala. Kusiwe na shaka kwamba msukumo wa Marekani wa kuleta mageuzi na kile kinachoitwa ‘uwajibikaji wa kidemokrasia’ haukusudiwi kheri ya watu wetu. Katika historia, mbeberu mamboleo Marekani imekuwa ikiunga mkono madikteta kwa maslahi yake huku ikitetea ‘demokrasia’ na ‘haki za binadamu’.

Soma zaidi...

Ni Wakati sasa wa Kugeuza Ukurasa wa Giza wa Oslo

Smotrich alitangaza kuangamia kwa mradi wa Dola ya Palestina kwa kuzinduliwa kwa mradi wa E1 au East One, ambao unachukuliwa kuwa utekelezaji wa kinachojulikana kama Mpango wa Jerusalem Kuu. Mpango huu unatenganisha Ukingo wa Magharibi wa Kaskazini kutoka Ukingo wa Magharibi wa Kusini, na, sambamba na hatua zilizochukuliwa na umbile la Kiyahudi uwanjani, unaunda viunga vilivyotengwa ndani yake ambavyo vinawazingira watu wa Ukingo wa Magharibi. Hili lilitanguliwa na kubomolewa kwa kambi kaskazini mwa Ukingo wa Magharibi na kuorodheshwa kwa UNRWA kama shirika lisilo halali, ili suala la wakimbizi libaki kuwa lisilo na umuhimu wowote.

Soma zaidi...

Hotuba ya Msemaji Rasmi wa Hizb ut Tahrir katika Wilayah ya Sudan katika Mkutano na Waandishi wa Habari mnamo Jumamosi, 22 Safar 1447 H sawia na 16/08/2025 M, yenye kichwa: “Wito kwa Watu wa Sudan... Ikamateni Darfur Ili Isiungane na Kusini”

Mnamo Jumamosi, 26/7/2025, Vikosi vya Msaada wa Haraka (RSF) vilitangaza kuundwa kwa serikali sambamba na serikali iliyopo nchini Sudan, katika mji mkuu wa Darfur Kusini (Nyala). Hatua hii ya RSF ni hatua ya juu katika kutenganisha eneo la Darfur, ambalo inalidhibiti, isipokuwa sehemu za mji wa El Fasher, ambao mzingiro wa kukandamiza umewekwa juu yake kwa zaidi ya mwaka mmoja, na kuanzisha mashambulizi mfululizo dhidi yake ili kuuangusha, ili eneo zima la Darfur liwe chini ya udhibiti wake.

Soma zaidi...

Enyi Watu! Je, bado mungali na matumaini kwa Watawala na Wanasiasa Watepetevu (Ruwaibidha) wa Sasa?!

Baada ya kuanguka kwa dhalimu Hasina, watu walitarajia Profesa Yunus achukue hatua madhubuti za kukabiliana na udhibiti wa Marekani-Uingereza-India kwa kutumia ushawishi wake wa kimataifa. Angeweza kuunda mjadala huo na mazingira ya kisiasa nchini humo ambayo kwayo watu wangeweza kuunda suluhisho jipya la kisiasa ili kulinda maslahi ya Uislamu, maslahi ya watu na ubwana wa nchi katika Bangladesh mpya. Ijapokuwa idadi kubwa ya wakaazi wa nchi hii ni Waislamu, serikali ya mpito, kuuondoa Uislamu katika masuluhisho ya kisiasa, haijaondoa marufuku iliyowekwa na dhalimu Hasina kwa chama cha kisiasa cha Hizb ut Tahrir kwa kujisalimisha kwa Marekani-India. Pamoja na hayo, kupitia makongamano ya mtandaoni Hizb ut Tahrir imewasilisha muundo wa dola ya Kiislamu, njia ya kuasisi uchumi unaojitegemea na kuwa na jeshi thabiti kwa ajili ya kulinda ubwana wa nchi hii kwa kuzingatia katiba ya Kiislamu ili kutekeleza matumaini na matarajio ya wananchi wa Bangladesh mpya.

Soma zaidi...

Iwapo Kuanguka kwa ‘Jamhuri’ Hakukupelekea Kusimamishwa kwa Khilafah, Ni lazima Kutumike kama Hatua ya Mpito kuelekea Khilafah Rashida

Kuporomoka kwa serikali ya Jamhuri nchini Afghanistan ni moja ya matukio muhimu zaidi kwa watu wa Afghanistan na Umma mpana wa Kiislamu katika karne ya 21. Serikali hii sio tu kwamba haikuwa na mizizi yoyote katika itikadi ya Kiislamu, bali ilikuwa ni zao la muundo wa ukoloni mamboleo - mfumo ulioagizwa kutoka nje uliojengwa ili kurasimisha ufisadi, utegemezi, na dhulma. Kuanguka kwake lilikuwa ni mwisho wa kimaumbile na usioepukika wa mfumo ambao, tangu kuanzishwa kwake, ulikuwa ngeni kwa kitambulisho cha Kiislamu na kupingana na maadili ya Uislamu.

Soma zaidi...

Kauli za Netanyahu kuhusu "Israel Kubwa" ni Tangazo la Vita ambalo linafuta Mikataba, na, kwa sababu hiyo, Majeshi Yanasonge, na Jambo jengine lolote lisokuwa hilo ni Usaliti

Huyu hapa mhalifu wa kivita Netanyahu anatangaza waziwazi na bila kufasiriwa kwa watawala waoga wa Kiarabu na wasemaji wao, akisema katika mahojiano na chaneli ya Kiebrania i24: “Mimi niko kwenye misheni ya vizazi na kwa jukumu la kihistoria na la kiroho, ninaamini kwa dhati ruwaza ya Israel Kubwa, ambayo ni pamoja na Palestina ya kihistoria na sehemu za Jordan na Misri.” Mhalifu Smotrich alikuwa amemtangulia kwa kauli zile zile na kunyakua sehemu za nchi za Kiarabu zinazoizunguka Palestina, ikiwemo Jordan. Katika muktadha huo huo, adui namba moja wa Uislamu na Waislamu, Rais Trump wa Marekani, alimpa idhini ya upanuzi wake akisema, “Israel ni sehemu ndogo sana ikilinganishwa na ukubwa wa ardhi hizo, na najiuliza ikiwa inaweza kupata ardhi zaidi kwa sababu kweli ni ndogo sana.”

Soma zaidi...

Msako Mkali wa Amerika dhidi ya Mashirika ya Kiislamu

Katika mahojiano ya hivi majuzi na mtangazaji wa redio Sid Rosenberg, Katibu wa Waziri wa Mambo ya Nje Marco Rubio alionyesha mchakato unaoendelea wa kuiorodhesha Ikhwan al-Muslimin na CAIR kama mashirika ya kigaidi. Waziri Rubio alisema kwamba uorodheshaji kama huo ulikuwa "katika kazi zao, na ni wazi kuna matawi tofauti tofauti ya Ikhwan al-Muslimin, kwa hivyo itabidi uliorodheshe kila moja yao."

Soma zaidi...

Kauli za Netanyahu baina ya Uhalisia wa Umbile lake na Msimamo Unaofifia wa Serikali ya Misri

Kauli za Waziri Mkuu wa umbile la Kiyahudi, Benjamin Netanyahu, ambazo alizungumza moja kwa moja kuhusu kile kiitwacho “Israel Kubwa zaidi” na kuhusu mipango ya uhamishaji na upanuzi, zinafichua kwa mara nyengine tena itikadi iliyokita mizizi ndani ya nyoyo za viongozi wa umbile hili; itikadi ya khiyana, usaliti, na ulafi wa ardhi ya Waislamu. Matamshi haya si kuteleza kwa ulimi, bali ni tafsiri ya kivitendo ya mipango iliyoandikwa katika fikra ya kisiasa ya Kizayuni, na mipango inayotekelezwa uwanjani hatua kwa hatua.

Soma zaidi...

Hizb ut Tahrir / Wilayah Sudan: Mwaliko wa Kuhudhuria Mkutano na Waandishi wa Habari

Sisi, katika Hizb ut Tahrir / Wilayah ya Sudan, tuna furaha kuwaalika ndugu zetu katika vyombo vya habari, wanasiasa, na wale wenye hamu na mambo ya umma kuhudhuria kwenye mkutano na waandishi wa habari, ambapo msemaji rasmi wa Hizb ut Tahrir / Wilayah ya Sudan atatoa hotuba kwa anwani: "Wito kwa Watu wa Sudan: Ikamateni Darfur ili Isijiunge na Kusin"

Soma zaidi...

Kuundwa kwa cheo cha "Mufti Muongofu" katika Zama za Akili Bandia Kuunda Sheria Inayoafikiana na Magharibi na Watawala wake Vibaraka

Katikati ya mporomoko wa kisiasa na kifikra wa Umma wa Kiislamu, na wakati ambapo njama dhidi ya dini yake na hukmu zake zikiongezeka, serikali tawala na zana zao - taasisi rasmi za kidini - zinazindua makongamano yenye kauli mbiu za kustaajabisha na misamiati ya uchochezi ya kiteknolojia, wakikopesha mradi wao wa kupotosha kuwa dini ni kero kwa “usasa” na “maendeleo”. Hii ni pamoja na kongamano la "Kuunda cheo cha Mufti Sahihi Katika Zama za Akili Bandia,” lililoandaliwa na Dar al-Ifta ya Misri chini ya udhamini wa moja kwa moja wa Rais Abdel Fattah el-Sisi.

Soma zaidi...

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu