Ijumaa, 16 Shawwal 1447 | 2026/04/03
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Kati ya Magereza ya Wahubiri na Bandari za Silaha…Je, ni Upi Msingi wa Hukumu wa Utawala Huu?

Huku magereza na vituo vya uzuizini vikiwa wazi kwa wabebaji wa Dawah wanaotaka utabikishwaji wa Uislamu, na huku wakiteswa kwa ajili ya riziki zao, wakinyamazishwa, na fikra zao zikikandamizwa—si kwa uhalifu wowote walioufanya, wala uchokozi wowote walioufanya, bali kwa sababu tu wanasema kwamba Uislamu lazima utabikishwe maishani, na kwamba Ummah lazima utawaliwe na sheria ya Mola wake Mlezi—wakati huo huo, bandari zinafunguliwa, barabara zinarahisishwa, na huduma zote zinatolewa kwa kila kitu kinachowatumikia maadui wa Ummah na kuimarisha nguvu zao!

Soma zaidi...

Tangazo la Matokeo ya Uchunguzi wa Mwezi Mwandamo wa Shawwal 1447 H na Hongera kwa Idd Al-Fitr Iliyobarikiwa

Baada ya kuchunguza mwezi mwandamo wa Shawwal katika usiku huu mtukufu, usiku wa Alhamisi, kuonekana kwa mwezi mwandamo kumethibitishwa kwa kuonekana halali kisharia katika baadhi ya nchi za Waislamu. Kwa hivyo, kesho Alhamisi itakuwa siku ya kwanza ya mwezi wa Shawwal na siku ya kwanza ya Idd al-Fitr iliyobarikiwa.

Soma zaidi...

Tangazo la Matokeo ya Kuutafuta Mwezi Mwandamo wa Ramadhan Iliyobarikiwa ya Mwaka 1447 H

Ramadhan inakuja mwaka huu huku Ummah ukisimama kwenye njia panda mpya; kwa upande mmoja unageuka kwenye makaa ya hali ya ukoloni na miiba ya usaliti wa watawala, na kwa upande mwingine hali mpya zinazoibuka za kimataifa, haswa migogoro ya kafiri Magharibi ya kikoloni imetoa fursa mpya ambazo, ikiwa zitakamatwa, zingesababisha Ummah wa Kiislamu kuinuka kwa muda mrefu.

Soma zaidi...

Kuikaribisha Ziara ya Modi: Khiyana ya Wazi kwa Damu na Heshima ya Umma wa Kiislamu

Waziri Mkuu wa India Narendra Modi amepangwa kufanya ziara ya kikazi nchini Malaysia mnamo Februari 7-8, 2026, na inaripotiwa kwamba anatarajiwa kupokea mapokezi makubwa kutoka kwa serikali na jamii ya Mabaniani nchini Malaysia. Kibaraka huyu wa Amerika mara nyingi hupokea mapokezi ya heshima katika nchi nyingi kote duniani na hupewa tuzo nyingi na nchi anazotembelea, wakiwemo watawala Ruwaibidha wa Waislamu, kiasi kwamba baadhi wako tayari kukita masanamu ili tu kumfurahisha kiongozi huyu mshirikina.

Soma zaidi...

Hitimisho la Kampeni “Khilafah sio Ndoto… Bali, ni Kilio cha Ulimwengu Unaowaka Moto!”

Leo, kwa Msaada Wake, tunahitimisha kampeni ya kimataifa iliyozinduliwa na Afisi Kuu ya Habari ya Hizb ut Tahrir, kwa maelekezo ya Amiri wa Hizb ut Tahrir, mwanachuoni mkubwa Ata Bin Khalil Abu Al-Rashtah, katika kumbukumbu ya miaka 105 ya kuvunjwa kwa Khilafah, ambayo iliamshwa na wanaume na wanawake wa Hizb ut Tahrir kote ulimwenguni.

Soma zaidi...

Hizb ut Tahrir / Tanzania Yafanya Semina kwa Mnasaba wa Kumbukumbu ya Miaka 105 ya Kuvunjwa kwa Khilafah

Katika kumbukumbu ya miaka 105 ya kuvunjwa kwa Dola ya Khilafah iliyotokea mnamo Rajab 1342 H / Machi 1924 M, jana, Jumapili, 29 Rajab 1447 H / 18 Januari 2026 m, Hizb ut Tahrir / Tanzania ilifanya semina fupi katika Masjid Taqwa, Ilala Bungoni katika jiji la Dar es Salaam.

Soma zaidi...

Kutoka Mgawanyiko hadi Umoja Kongamano la Khilafah 2026

Hizb ut Tahrir / Amerika ilifanya kwa mafanikio Kongamano lake la kila mwaka la Khilafah kama sehemu ya kampeni ya kimataifa kwa mnasaba wa kumbukumbu ya kufutwa kwa Khilafah mnamo tarehe 28 Rajab, 1342 H. Kongamano hilo lilitumika kama wito kwa Waislamu kote duniani kutambua na kutimiza wajibu wa kuregesha mfumo kamili wa maisha wa Kiislamu, kama ulivyoamriwa na Mwenyezi Mungu (swt), kupitia kusimamisha tena Khilafah kwa njia ya Mtume wetu Muhammad (saw).

Soma zaidi...

Kongamano la kila Mwaka la Hizb ut Tahrir katika Wilayah Lebanon Kwa Mnasaba wa Kumbukumbu ya Miaka 105 ya Kuvunjwa kwa Khilafah “Kuhalalisha Mahusiano na Kujisalimisha, au Ahadi ya Mwenyezi Mungu na Dola ya Uislamu?!”

Kwa mnasaba wa kumbukumbu ya miaka 105 ya kuvunjwa kwa Khilafah, Hizb ut Tahrir katika Wilayah ya Lebanon ilifanya kongamano lake la kila mwaka la kisiasa kwa kichwa: “Kuhalalisha Mahusiano na Kujisalimisha, au Ahadi ya Mwenyezi Mungu na Dola ya Uislamu?!”, ambapo wazungumzaji kutoka Lebanon, Syria, Uturuki, na Gaza walishiriki.

Soma zaidi...

Mapendekezo ya Kongamano Lililofanywa na Hizb ut Tahrir / Wilayah ya Sudan Kukumbuka 105 Hijri Tangu Kuvunjwa kwa Khilafah

Mnamo Jumamosi, tarehe 28 Rajab 1447 H, sambamba na tarehe 17 Januari 2026 M, Hizb ut Tahrir / Wilayah ya Sudan ilifanya kongamano la kumbukumbu ya miaka 105 tangu kuvunjwa kwa dola ya Kiislamu ya Khilafah. Kongamano hilo lilihudhuriwa na watu mashuhuri, wakiwemo wanasiasa, watu mashuhuri wa vyombo vya habari, wasomi, na viongozi wa jamii. Kwa kuzingatia kwamba kumbukumbu hii chungu inakuja huku sisi nchini Sudan tukiteseka kutokana na vita vilivyowashwa na ubeberu wa Marekani, ikiwatumia vibaraka wake wa ndani kusambaratisha kile kilichobaki cha umoja wa nchi yetu chini ya sera yake inayoitwa “Mipaka ya Damu”. Hivyo, kichwa cha kongamano letu kilikuwa: “Sudan Kati ya Sera za Mipaka ya Damu na Kuunganisha Watu Kuwa Umma Mmoja.”

Soma zaidi...

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu