Kati ya Magereza ya Wahubiri na Bandari za Silaha…Je, ni Upi Msingi wa Hukumu wa Utawala Huu?
- Imepeperushwa katika Misri
- Kuwa wa kwanza kutoa maoni!
- |
Huku magereza na vituo vya uzuizini vikiwa wazi kwa wabebaji wa Dawah wanaotaka utabikishwaji wa Uislamu, na huku wakiteswa kwa ajili ya riziki zao, wakinyamazishwa, na fikra zao zikikandamizwa—si kwa uhalifu wowote walioufanya, wala uchokozi wowote walioufanya, bali kwa sababu tu wanasema kwamba Uislamu lazima utabikishwe maishani, na kwamba Ummah lazima utawaliwe na sheria ya Mola wake Mlezi—wakati huo huo, bandari zinafunguliwa, barabara zinarahisishwa, na huduma zote zinatolewa kwa kila kitu kinachowatumikia maadui wa Ummah na kuimarisha nguvu zao!



