Ufuatiliaji Mkubwa wa Mkoloni Amerika juu ya kile kinachoitwa “Mageuzi” sio Chengine ila ni Jaribio la kupanua Udhibiti wake nchini Bangladesh
- Imepeperushwa katika Bangladesh
- Kuwa wa kwanza kutoa maoni!
- |
Balozi Mdogo wa Marekani jijini Dhaka, Tracy Ann Jacobson, alifanya mkutano na Profesa Ali Riaz, Makamu Mwenyekiti wa Tume ya Kitaifa ya Maridhiano wiki iliyopita ili kuuliza kuhusu mipango ya mageuzi inayoendelea na maendeleo yake. Jacobson na manaibu wake wamekuwa wakifanya mfululizo wa mikutano na wawakilishi wa vyama vikuu vya kisiasa. Kama sehemu ya ushirikiano wa Marekani ‘kukuza demokrasia’ nchini Bangladesh, tunaona mikutano na taarifa za mara kwa mara kutoka kwa Ubalozi wa Marekani nchini Bangladesh na Wizara ya Mambo ya Nje ya Marekani zinazohimiza marekebisho katika utawala. Kusiwe na shaka kwamba msukumo wa Marekani wa kuleta mageuzi na kile kinachoitwa ‘uwajibikaji wa kidemokrasia’ haukusudiwi kheri ya watu wetu. Katika historia, mbeberu mamboleo Marekani imekuwa ikiunga mkono madikteta kwa maslahi yake huku ikitetea ‘demokrasia’ na ‘haki za binadamu’.